Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kwel SNA...hi kabila n shida...Nakubali aisee..mimi ni mchaga ila hawa dada zetu hapana.
Kuna dada wa kichaga nilikua nioe alininyoosha mnyoosho mmoja sina hamu naoo aiseee...
Saivi namnyemelea muiraki
Asante sana, mtunzi Mimi nimechota mzigo wote kama wazo la kuzaa jambo fulani ktk sura ya kitabu au funzo ktk moja ya project zangu za saikolojiaHawa wanawake wengine ni shida, ya ndani analeta hapa mtandaoni kweli dah. somenihapo chini (instagram)
View attachment 688048
Nilifikia uamuzi huo baada ya kuona unaficha PESA zako. Ile Siku niliyokubamba unatoa Ela kwenye akauti yako kwa Siri na hapo tulikuwa hatuna ela kabisa NILIUMIA kuliko hata ningekufumania. Yaani nilikuona huna NIA na Mimi, HUNIPENDI, HUNIJALI. Najua Kazi ulizofanya hata kama NI Ndogo hukukosa hata mkate au sukari ya kuleta Nyumbani. Lakini ukaamua kula bata, hutoki na Mimi, Mara nyingi ukiwa na ela unatoka peke yako unarudi mpaka asubuhi... ukijua kuna punda wako hapa nyumbani atafanya kila kitu.
- joycekiriasuperwoman
Kilewo baba Watoto wangu, yaliyotokea ilibidi yatokee ili kila Mmoja aanze upya safari ya Maisha Yake. Wakati tunaanza huu mwaka nilikuambia huenda mwaka huu tukaachana! Unakumbuka? Well, Lakini jambo moja nakusisitiza hapa, Nimekuomba sana uniachie biashara zangu nisimamie, ili na wewe usinamie biashara zako kutokana na Changamoto zetu hasa za kiuchumi. Wewe Pesa zako unazopata kwenye biashara zako hutaki kushea, Ila Pesa zinazotoka kwenye biashara zangu unataka tushee. Najua ni ujinga wangu wa kukupenda sana ndo umeniponza. Labda ningetenganisha Mapenzi na biashara tusingeishia huku.
Wakati mimi nasajili Kampuni Yangu nilikuweka kwenye kampuni bila shida yoyote na wakati nafungua akaunti za bank nilikuweka pia. umekuwa ukijua kila ela inayoingia pamoja na matumizi yote kwa sababu lazima tusaini Wote na ndiyo Raha ya Mapenzi.
Wewe ulipofungua Kampuni yako uliweka pia jina langu kitu ambacho nilipenda sana, lakini ulipokwenda kufungua akaunti ya bank HUKUNIWEKA. Kiukweli SIKUPENDA, mbaya zaidi ukataka kuwa unasaini Pesa zako kivyako.
Japo nilianza kuona mashaka Lakini nilijipa Moyo, labda ukipata utanishirikisha pia kama Mimi nilivyoamua kukushirikisha kila kitu changu. PESA MWANAHARAMU buana, pale tuu ulipoanza kazi na kampuni yako Ndipo SHIIIDA ilipoanzia, hukutaka kushea hata senti Nyumbani wakati biashara zangu kwa Kipindi chote cha Miaka NANE zimeendesha familia yetu bila tatizo.
Kuna Miradi mbalimbali ambayo ulikuwa ukionyesha NIA ya kuifanya lakini yote ilifeli. Hivyo haikuwa rahisi KUKUJUA kwa upande wa KIUCHUMI sura yako ikoje... Ulijaribu biashara hizo kwa mtaji wa Familia bila kuona matokeo chanya, Pesa zikawa hazirudi lakini tukajipa Moyo biashara ndivyo zilivyo. Mwisho nikakushauri mtaji wa biashara tukope Bank labda utakuwa na nidhamu zaidi ya Pesa ya Mkopo kuliko kutoa ela Nyumbani. Hukupenda huo Ushauri, ukaona nakubania.
Sasa MWAKA huu 2018 tuliongea mengi pale Bahari beach, juu ya mahusiano Yetu na Changamoto zake! Pamoja na yote tuliyoongea nikakuomba kila mtu asimamie biashara zake, kisha tukubaliane kwenye MAJUKUMU ya Familia kwamba nani atafanya Kipi. Lakini pia nikakuambia kwamba Niko radhi kuendelea kutimiza hayo majukumu. [HASHTAG]#SIR[/HASHTAG]
Kilewo najua Haya siyo mageni kwako, tumeyaongea kwa muda mrefu sana. Tumewashirikisha watu wa karibu. Pamoja na hayo yote Kilichonishangaza sasa ni wewe kukataa kuniachia biashara zangu wakati wewe una za kwako. Tena unasaini akaunti yako peke yako halafu akaunti Yangu nimekuweka tunasaini Wote.
Kilewo kwa staili hiyo ya maisha nilianza kukosa Furaha sana na wewe kwa kuona unanitumia wala huna NIA Njema na Mimi, HUNIPENDI, HUNIJALI, huku Ndani MAPENZI YAKAPOTEA KABISA. Mpaka juzi birthday yako sikuwa najiskia kukuwish. Lakini kwa ajili ya Watoto nikajilazimisha. Ngoja niishie hapa.
KILEWO baba Watoto wangu, Dunia inajua NINAVYOKUPENDA. Tatizo langu kubwa na wewe unajua fika siyo wewe kutokuwa na Pesa, BALI KUTUSHIRIKISHA KWA KIDOGO UNACHOPATA wewe kama BABA wa Familia. kwa Sasa nina tatizo kubwa na wewe la kunipiga baada ya kuamua 2018 nitakuwa natoka peke yangu kujipa raha. Unajua sehemu ninazokuwaga nikiwa nimetoka na ndo sababu ulikuja ukanikuta, lakini uliamua kunipiga. Kesi ipo Dawati.
Kilewo ningekuwa na NIA mbaya nisingekuweka kwenye biashara Yangu, nimenunua Viwanja Goba na Bagamoyo, bila uwepo wako, lakini nilikuja kukushirikisha na wewe ukaenda kuongeza majina yako. Sikuwahi kulalamika maana NAKUPENDA na wewe ndo Baba Watoto wangu. Nimetamani kuzaa mtoto wa Tatu lakini kwa ambushi zako nimeogopa. Mambo ya KOMAA KAMANDA hapana. Nikasema Wawili wanatosha.
Kilewo wangu nakuomba tena na tena uniachie biashara zangu niweze kuendelea kutunza hawa Watoto wetu. Toka unipige umeondoka siwezi kutoa ela, hatuna Chakula nyumbani, Madeni ya wafanyakazi, Nyumba nadaiwa n.k
[HASHTAG]#SIRIZANDANI[/HASHTAG]
KILEWO atakuwa amebanwa na kazaramo kamoja ka mbagala rangi tatu ni mauno kwenda mbele.Ugali dagaa na mchicha na amani ya roho.Stress ya nini na vijisenti vya masimango hela unatoa kwa MUSHI unaleta tutumie na mimi nikitaka kwenda kula na Zainabu unanitangaza!!! Ngoja nibaki na Zainabu wangu nikiwa na amani na hata instagram hajui na hajasoma hata meseji zenu
Hawa jamaa wanashanHata mimi nawashangaa hawa wanaoangalia upande mmoja tu! Joyce na Kilewo inaonesha wana joint account na hela hazitoki bila saini ya wote, mume kauchuna haweki saini watoto wana njaa!
Kilewo familia imemshinda ndio ubunge atauweza?Ana matatizo ya KISAIJOLOJIA huyu mama jamani asaidiwe maana anaweza letwa MIREMBE kabla KILEWO hajaja MBUNGENI.
KabisaaaaaHAKUNA MWANAMKE HAPA.
Kwenda kusinzia Dodoma kunahitaji ujuzi gani?Hawa jamaa wanashan
Kilewo familia imemshinda ndio ubunge atauweza?
Joyce ni wale watu wanaotaka waonewe huruma na dunia nzima.kupata mtu ambae mna lengo moja nayo changamoto mkuu.kuna watu wabinafsi sana . hv mtu unakuwaje mchoyo hadi kwa damu yako eti.japo tunamuona joyce mbaya ila na huyu kamanda sio kabisa aaah
Hivi kweli unamuamini huyu mama anachosema kuwa Kilewo anakatazia hela isitoke kuwalisha watoto wake na kulipa pango? Huyu mama si angekwishafukuzwa ndani ya nyumba kama pango halipi?Huyu mwanamke anakosea kuyaanika haya. Je vipi huyu anaeng'ang'ania mali za familia wakati watoto wanahitaji kuishi?
Kuna wanaume wanaachana na wake zao wanaacha magorofa for the sake of the kids.
Neno jema sanaJoyce ni wale watu wanaotaka waonewe huruma na dunia nzima.
Atasema chochote tu hata uongo ili aonewe huruma. Nilikwishaiona hali hii kwa rafiki yangu wa karibu sana. Hatari sana.
Kwa kuwa wanaume sio walamikaji basi dunia inasikia upande mmoja tu. Laiti kama Kilewo angeelezea upande wake huyu mama angeumbuka vibaya sana.
Hii ndio sababu ya kuanika hizi siri za ndani huko Insta. Anajua akienda na mumewe kwenye kikao cha familia ili wapatanishwe ataumbuka. Lakini anajua akiyasema huko Insta Kilewo hatamjibu. Bure sana huyu mama.
Ujinga wa mume wa Joyce uko wapi? Ama ume-conclude kuwa ni mjinga kwa kusoma maandiko ya upande mmoja?HUYU MWANAMKE AMEKOSA SIFA YA UTII KAMA AMBAVYO MUME AMEKOSA AKILI. HVYO WOTE NI WAJINGA. KWA KUWA WOTE NI WACHAGA, WACHA TUTIZAME SINEMA.
Hiyo ni old fashion wengine hatuendekezi huu ujinga hutaki kuchangangia akae nyumbani alee watotoJukumu lote la family finances na well being ni BABA.
Hii kugawana ni vituko.Ndio mwanzo wa kudharauliana kama hivi.
Hela ya mwanamke hua ni yake alone,ya sisi Wababa ni ya familia yote!
Ukimya ni jibu la mjingaKwa hoja hizi Kilewo anatakiwa arespond kuondoa shaka kuwa hasingiziwi
Halafu unakuta sio mariaMmmh....insta kuna msaidia nini?
Mambo yako ya familia unaleta social media duuh!
Hii ni aibu kwake, na hamchoreshi huyo marioo, anajichoresha yy mwenyewe, coz now tumejua Joyce ni sugar mumy!
Mafundo ya ki-Tanga hawana huko Machame.Hivi huyu Dada hajafundwa jaman mbona kila kitu anatoa nje kumuacha uchi mume wake siku ya siku kumuacha hawezi anabaki kuaibika tu