Uchaguzi 2020 Hivi inakuwaje kuanza kwa kampeni kwa CCM kuwa ruksa na kwa wapinzani kuwe haramu?

Uchaguzi 2020 Hivi inakuwaje kuanza kwa kampeni kwa CCM kuwa ruksa na kwa wapinzani kuwe haramu?

Tatizo sio polisi wala CCM.
Tatizo upinzani hauna viongozi waliokomaa kisiasa ,kijamii na kiusalama.
Kidogo ACT naona kuna uongozi makini kiasi Fulani lakini pia wajitahidi kuwa na intelijensia ya kutosha.

Wakubali kuwa Kufa kwa CUF na Chadema ni mpango wa Mungu kwani hivyo vyama viliwaabudu wenyeviti wao wakasahau kuwa mageuzi na mabadiliko sio suala la Mbowe na Lipumba bali ni suala la Watanzania wenyewe.
Mbowe kujitapa kuwa yeye ndiye Chadema na Lipumba kuwa yeye ndiye CUF ,mwenyezi Mungu amewaumbua na vyama vyao vimesambaritika wakiwa wanaviongoza huku wakibaki na aibu kubwa na ACT na NCCR vikichanja Mbuga.

Nawashauri ACT na NCCR wazingatie sheria na kanuni za Jeshi la Polisi zinazowataka kutoa taarifa polisi wakati wa shughuli zote za kisiasa kwenye maeneo ya nchi yetu.
Hii ni kwa faida yao wenyewe.
Mfano kwa sasa ni wazi kuwa kuna uadui mkubwa sana kwa wanasiasa ndani na nje ya vyama vyao.
CUF una uhasama na ACT.
Chadema ya Mbowe inauhasama na CCM inayoshikiliwa na waasisi wa mageuzi ndani ya nchi hii na wapinga ufisadi. Kumuunga mkono Mbowe ni kuunga mkono Ubeberu, ulevi wa pombe,ulevi wa madaraka , uongo, udikteta , umangi meza ,ubinafsi ,uchoyo ,ufuska,uhuni,usaliti, kuabudu mizimu , ubabe na wizi. Huyu na wote wanaomuunga mkono mwisho wao ni Mwaka huu.
Hatutaki kusikia Chadema ikiwa chini ya huyu Mtu mwovu.
Salama ya Chadema ni kumtoa msaliti wa Demokrasia Mbowe.

Zito Kabwe wajenge vijana wako wawe Jasiri lakini wafuate sheria na kuhakikisha hawakwaruzani na vyombo vya Dola.
Kutoa taarifa kunawafanya watu wa ulinzi kuwa na utayari wa kuhakikisha hakuna chama kinachovamiwa na wahuni wa vyama vingine.
Hivi ni Mkuu gani wa Polisi atakubali kuona wanasiasa wanaopanga mikakati ya kushika dola wanaifanya kwenye eneo lake na kutoa matamko makali bila kujua kuwa walikuja lini na wanaifanyia wapi na kwa muda gani?
Haiwezekani tukubali tu kuwa ni busara kwa kipindi hiki vyama vyote vitoe taarifa na sio kuomba kibali Bali ni kutoa taarifa iwe ni kikoa cha ndani au cha nje. Hii itaepusha vurugu za polisi na wanasiasa.

Zito amekomaa kisiasa nadhani anaelewa umuhimu wa kuepuka hii mitego.
ACT imewashika pabaya wote ikiwemo Chadema na Msaliti Mbowe na wasaliti wenzake akina Lipumba ,Mrema,Cheyo,Mbatia, Rungwe, na wengineo wanaongangania uenyekiti wa maisha.

Asiyetaka kutoa taarifa polisi basi ajue ataendelea kula Bakora mwanzo Mwisho Mwaka huu.

Toeni Taarifa,kisha simamieni haki yenu ikiwezekana mfikisheni mahakamani kwa mtu yeyote anayekiuka katiba na anayewazuia wakati mna nakala ya barua ya taarifa na haki ya kukusanyika kwa amani.
 
Nenda ukashtaki kwa msajili wa vyama sio jukwaani!
kipara kipya
Wewe ambaye umejiunga katika ile "Praise & worship team for Magufuli" kwa kila analolifanya, hata liwe baya kiasi gani, ni vyema na wewe ukatambua kuwa kilio na kusaga meno kwetu sote watanzania, bila kujali Itikadi zetu za kisiasa zitakuwa kubwa mno!

Na wewe wakati huo uta-realize kuwa imekuwa too late, kuweza kukemea tena!
 
Daudi Mchambuzi
Hao CCM wanaojitapa kuwa wamewafanyia mambo mengi sana mazuri wananchi, kwa hiyo hawaogopi wapinzani katika uchaguzi mkuu ujao.........

Hivi kama mna uhakika wa kupata ushindi mkubwa kiasi hiko, mna haja gani ya kufanya figisu figisu hizi zote, zinazoongozwa na Jeshi letu la Polisi?
tunahakikisha tu sio magoli pekeyake pamoja na chenga twawala..tunaiga kotekote kaka
 
tusisahau maombi ya wengi swala la katiba mpya..ndo ingejibu haya sasa hata mkurugenzi wa uchaguzi anachaguliwa na boss unategemea nn
 
Walishaeleza mkuu, watatumia dola kuendelea kubaki madarakani.
Daudi Mchambuzi
Hao CCM wanaojitapa kuwa wamewafanyia mambo mengi sana mazuri wananchi, kwa hiyo hawaogopi wapinzani katika uchaguzi mkuu ujao.........

Hivi kama mna uhakika wa kupata ushindi mkubwa kiasi hiko, mna haja gani ya kufanya figisu figisu hizi zote, zinazoongozwa na Jeshi letu la Polisi?
 
kipara kipya
Wewe ambaye umejiunga katika ile "Praise & worship team for Magufuli" kwa kila analolifanya, hata liwe baya kiasi gani, ni vyema na wewe ukatambua kuwa kilio na kusaga meno kwetu sote watanzania, bila kujali Itikadi zetu za kisiasa zitakuwa kubwa mno!

Na wewe wakati huo uta-realize kuwa imekuwa too late, kuweza kukemea tena!
vijana wa ufipa mna tatizo kubwa sana,wewe hapo ulipo Lissu au Mdee akisema kitu hata kwa asilimia mia ni cha uongo na kutunga bado utatetea bila aibu bila kujali ubaya wa ule uzushi je wewe tukuiteje!
 
Lakini lazima watekeleze majukumu yao kwa mujibu wa viapo vyao.

Viapo vyao vinawataka wao wasijuhusishe na mambo ya siasa na jukumu lao kubwa liwe kulinda usalama wa raia na Mali zao na wawe "fair" katika utekelezaji wa majukumu yao.

Wajiulize hao Polisi wetu, hivi ni kweli wanatekeleza majukumu yao kwa mujibu wa viapo vyao au wamejitumbukiza kwenye ulingo wa kisiasa, wakijiegemeza kwa upande wa CCM?
Hapo sasa ndipo utagundua unafiki wa hali ya juu kwa Kiongozi Mkuu wa ccm alipotoa tamko la kuwakemea Wanausalama wa Mkoa wa Arusha. Eti alikuwa hajawatuma kwenda kutenda waliokuwa wakiyatenda.
 
Wewe ungekuwa polisi ungeweza kumkamata Waziri mkuu au Rais kwa hicho unachokiita kufanya kampeni kabla ya wakati?

Pili, unawezaji kutenganisha CCM na serikali, au Rais na mwenyekiti wa CCM? Mbona matatizo yakitokea mnasema ni CCM kisa tu serikali inaongozwa na CCM?
 
Wewe ungekuwa polisi ungeweza kumkamata Waziri mkuu au Rais kwa hicho unachokiita kufanya kampeni kabla ya wakati?

Pili, unawezaji kutenganisha CCM na serikali, au Rais na mwenyekiti wa CCM? Mbona matatizo yakitokea mnasema ni CCM kisa tu serikali inaongozwa na CCM?
Ninachokataa Mimi ni kwa Jeshi la Polisi kutumika kwa ajili ya kulinda utawala huu wa mabavu

Wanatakiwa wao watekeleze majukumu yao kama walicyokula viapo vyao, kuwa watakuwa "fair" na hawatajihusisha na siasa
 
Lakini lazima watekeleze majukumu yao kwa mujibu wa viapo vyao.

Viapo vyao vinawataka wao wasijuhusishe na mambo ya siasa na jukumu lao kubwa liwe kulinda usalama wa raia na Mali zao na wawe "fair" katika utekelezaji wa majukumu yao.

Wajiulize hao Polisi wetu, hivi ni kweli wanatekeleza majukumu yao kwa mujibu wa viapo vyao au wamejitumbukiza kwenye ulingo wa kisiasa, wakijiegemeza kwa upande wa CCM?
Potelea mbali kiapo. Hawawezi kuuma mkono unaowalisha. Tumefika pabaya. Nani atabadili hali hii?
 
Back
Top Bottom