Hivi inawezekana kwa Waislamu kuwa na hesabu hususa ya siku za kufunga badala ya kutegemea kuonekana au kutoonekana kwa mwezi?

Hivi inawezekana kwa Waislamu kuwa na hesabu hususa ya siku za kufunga badala ya kutegemea kuonekana au kutoonekana kwa mwezi?

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Ni kitu ambacho siku zote sijakielewa, na labda ndugu zangu Waislamu watanisaidia hapa. Kufunga najua ni suala la kujipa muda wa kutafakari matendo na maisha yako na kuboresha uhusiano wako na Mwenyezi Mungu. Sasa sielewi kwa nini jambo hili lihusianishwe na kuonekana au kutoonekana kwa mwezi? Kwa nini isijulikane kwamba ukianza kufunga leo, basi utakuwa katika mfungo kwa siku 30, na zikiisha basi, mwezi uwepo au usiwepo, unakuwa umemaliza kipindi chako cha utafakari, kwa kuwa kutoonekana au kuonekana kwa mwezi katika siku fulani ni jambo tu la kijiografia katika mizunguko ya sayari.

Najua kwa Waislamu mwezi na alama yake ni muhimu kama ilivyo msalaba kwa Wakristo, ambapo kwa Waislamu mwezi huwakilisha mwongozo wa Mwenyezi Mungu katika njia ya maisha, wakati Wakristo huuona msalaba kama ishara ya ukombozi wa dhambi kupitia Yesu, na ndio maana alama ya mwezi na msalaba vina sehemu kubwa katika dini hizi mbili.
 
Zipo nchi zinafanya hivyo na bado makosa yanajitokeza
 
Kufunga kunafuata kalenda ya kiislam,
Kalenda ya kiislam inafuata muandamo wa mwezi.
Sasa wewe ulitaka wafuate kalenda ya wapagani!? Au ulitaka utaratibu wote wakufunga uwe umetengenezwa na makafiri?
Lakini wewe kinakuuma nn?
 
Utaratibu wote wa dini upo kwenye maandiko ambayo ni qur an na sunna hakuna wa kuibadilisha kama wewe unataka din ya mtu kujibadilishia anavyopenda yeye basi sio uislamu,
 
Kufunga na kufungua kunafuata muandamo wa mwezi wa kiislamu.
Utaratibu huu umekuwepo toka enzi . Kwakuwa wakisasa tunataka kila kitu kiwe kama marekani baaasi imekuwa kero
 
Back
Top Bottom