Hivi kati ya Ottoman empire na Roman empire ipi ilitumia zaidi nguvu na kuua watu wengi per time it ruled?

Ya sure ni kama umelala kwenye nyumba yako unaamka asubuhi unakuta mtu anaishi na vitu vyako vyote kavitoa ndani na kaweka vyake na wewe umekua mfanyakazi kwa lazima. Huku ukiwa umefungwa minyororo.
Cha kufanya hapo ni kua mpole kwanza na kujifanya mjinga. Ili akikosea tu akakupa chance ya kukufungua minyororo unatumia opportunity effectively. Na asipokosea ni kuendelea kumuwekea mitego itakayomfanya akosee.
 
so ingekuwa 'god's plan' kuunganisha dunia under 1 religion then asingeruhusu ottoman empire ianguke kwasababu mpaka leo muslims wako divided na nchi mbali mbali za kiislam ziko divided..only under ottoman empire were they truly united


Wewe nani kakuambia kwamba Waisilamu wataunganishwa chini ya empire???
 


Swali halikuwa ni vipi mgawanyiko wa waisilamu ulivyotokea!!--- juu ya yote mgawanyiko ulitokea baada ya waisilamu KUACHA MAFUNDISHO YA DINI YAO, sababu zote hizo ulizozitaja MSINGI WAKE NI KUACHA MAFUNDISHO YA DINI, Kama Waisilamu wangalishikamana na kamba ya Allah kamwe wasingemuua Seydna Uthman na Seydna Ally (ra), uroho wa madaraka na magomvi miongoni mwao maana yake ni Kukosa mafundisho ya dini. Na Allah ameshasema ndani ya Qur'an kwamba hawezi kuwaacha waaminio katika hali hiyo ya kufarakana ni lazima awapambanue nani muovu na nani ni safi kwa kumtuma mtume aje kuwaonya mtume huyo ndiye Hadhrat Mirza Ghulam Ahmad (as), huyo ni mtume mfuasi wa Mtume Muhammad (saw), huyo kaja kufundisha Uisilamu uleule aliofundisha mtume (saw). Yeye ni mujjadid.

Unasema Waahmadiyya wanaitwa makafiri na majority ya waislamu, nasema hivi; Mtume (saw) alisema umati wake utagawanyika makundi 73 yote yataingia motoni isipokuwa kundi moja tu, sasa wewe huoni kwamba makundi yote hayo inapokuja Ahmadiyya wote wanaungana dhidi ya Ahmadiyya!!, huoni kwamba ni makundi 72 dhidi ya kundi moja??!!, huoni kwamba hilo kundi moja ndiyo Ahmadiyya??

Niliposema kwamba Roman empire ilikuwepo kabla ya Yesu kuzaliwa, maana yangu ni Roman empire chini ya Emperor Caesar na siyo Roman empire chini ya Emperor Constatine na hata chini ya huyo Emperor Constatine bado hakuna ushahidi kwamba Ukristo ndiyo ulijenga hiyo Empire bali ni Empire ndiyo ilifanya ukristo uwe dini yake. Halikadhalika katika Uisilamu ni Ottoman empire ndiyo iliyokumbatia Uislam (viongozi) wake na sio vinginevyo ndipo nikasema Ukristo na Uisilamu haukuzijenga hizo Empire bali hizo empire zilijijenga zenyewe na kwakuwa wafuasi wake walikuwa na dini zao outmatically sentiments zao zikaingizwa katika empire zao, msingi wangu ulikuwa ni huo.
 
Rafiki haupo serious , unaongelea Anglican church iliyokuja juzi juzi hapa, basically most parts of western europe was under Catholic church.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nani kamsahau ?
Kama tunajua amesahaulika, nani anatuzuia sisi waafrika kum promote mwafrika mwenzetu ?


We, Africans like excuses

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Katika watu tunaosema walisaini mikataba feki ni huyo Carl Peters but hapa unam portray kama someone trustworthy

Sent using Jamii Forums mobile app
 
400 years ni 8 generations

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yaani Tyson Mayweather na MJ ndio mifano yako katika ku justify hoja yako, Big NOOOOO.

Ipo hiviiii, kule marekani kutokana na mbinyo uliokuwepo katika jamii za watu weusi vs watu weupe, weusi wengi walikosa fursa ya kujiunga na sekta ambazo ni za white collar jobs ambazo zilihitaji wasomi unlike entertainment industry ambayo ever since haikuwa strict hivyo kufanya iwe sehemu ya blacks kupumulia na ku make a living.

Utakuja kutoa tena mifano ya richest rappers like Sean Comb na Shawn Cutter. Hawa again chimbuko la muziki wao ni struggle za slaves kule America ambao walikuwa wana compose nyimbo ambazo tunaziita za miondoko ya hip hop katika hatua zao za ku claim better living standard in the Us, but later on until todate their purpose has no longer being an issue of claiming better living standard but rather entertaining people worldwide.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Katika watu tunaosema walisaini mikataba feki ni huyo Carl Peters but hapa unam portray kama someone trustworthy

Sent using Jamii Forums mobile app
Mikataba ya hovyo inakuwa dhana . subjective. Kwa wajerumani waliohitaji makoloni ilikuwa mikataba mizuri... Kwa sisi watawaliwa haikuwa mizuri.. na Carl kwa Wajerumani was a smart man.. na Kwetu he was smart but evil

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Wewe nani kakuambia kwamba Waisilamu wataunganishwa chini ya empire???
historia ndo imenambia hakuna kipindi waislam walikuwa wamoja kama kipindi cha empires baada yapo kila siku wanazidi kutengana na kuuana....

Sasa hizi stori za uahmadiyya hazina maana eti kwasababu waahmad wanapingwa sana basi ndo wa kweli kwa maana vikundi vipo vingi vidogo vinavyopingwa na waislam wengi na kuchukuliwa kama makafir...
hata wasunni wanawapinga washia na kuwaita makafir.Hivyo kupingwa haimaanishi uko sahihi

BTW kila kundi linajiona lenyewe ndo lile la ukweli 1 out of 73

Although ni kweli ahmaddiya ni most peaceful sect na ndo sababu wanapingwa sana na waislam wengine Lakini haimaanishi wao ndo waislam wa kwel.

Tena u'peacefulness wao unahesabiwa kama ukafir maana wanaweza kwenda hata kusali kanisani hao
 


Kwanza lazima ujue mafundisho Yote ya Uisilamu yanapatikana katika Qur'an na Hadithi za mtume Muhammad (saw), hivyo ili waisilamu waungane ni lazima waunganishwe chini ya Imam Mahd (kiongozi anayeongozwa ) na sio chini ya Empire yoyote, hakuna kitu kama hicho kwamba Empire ndiyo itawaleta pamoja waisilamu, kama unaoushahidi kutoka katika hizo Sources mbili yaani Qur'an na Hadithi lete hapa. Imam Mahd ndiye Muanzilishi mtukufu wa Jumuiyya ya waislamu wa Ahmadiyya.

Umesema kweli kwamba dhehebu la Sunni wanawaita Mashia Makafiri na Mashia hivyo hivyo huwaita Masunni makafiri, Answar sunna pia huwaita Mashia makafiri na hivyohivyo mashia huwaita Answar makafiri ilmuradi wote wanaitana makafiri, lakini jifunze jambo hili; wanapotokea Ahmadiyya mbele ya hayo madhehebu mengine hayo madhehebu huungana na huweka tofauti zao pembeni na kuwa kitu kimoja dhidi ya Ahmadiyya, mfano wake ni huu Simba na Swala ni maadui lakini ukiwaweka katika chumba kimoja na ukawasha moto hapo uadui wao huisha na kuanza kupambana na moto kwanza, hapo Ahmadiyya ni kama moto na hayo madhehebu mengine ni kama simba na swala, hapo ndipo ile hadithi ya mtume (saw) inapofanya kazi pale aliposema kwamba; "Umati wake utagawanyika makundi 73 yote yataingia motoni isipokuwa kundi moja".

Umesema kweli kwamba waisilamu wa Waahmadiyya ni watu wa amani lakini hujasema kweli unaposema kwamba waisilamu -Waahmadiyya huswali kanisani, karibu kila nchi duniani kuna Waahmadiyya na kuna Misikiti ya Ahmadiyya imejengwa sasa inakuaje unadanganya kwamba Waahmadiyya huswali kanisani??.

Of all religions sects, Ahmadiyya sect is in Islam is the fastest growing sect of all sects , Chukua madhehebu ya dini zote duniani Ahmadiyya ndiyo dhehebu linalokuwa kwa kasi kubwa kupita madhehebu ya dini zote na hii ni moja ya sababu ya Ahmadiyya kuchukiwa na madhebu mengine ya Waisilamu, licha ya juhudi za hali na mali zinazofanywa na hao waisilamu wengine kuzuia Jumuiyya ya Waisilamu wa Ahmadiyya lakini wao wenyewe wanakiri; Ahmadiyya is unstopable.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…