Hivi kuchoma moto noti (Pesa) kama hivi inaruhusiwa??

Hizo noti za usa hata huko kwao huonekana. Wakizichoma na sijawahi kusikia wamekamatwa ila kuhusu bendera aisee hilo ni tatizo. Lil Wayne akiwa anafanya shooting alikanyaga bendera ya marekani ikabidi aombe msamaha.

Kwa sisi Tanzania ukiichora noti au kuichoma kazi unayo. Ukiichoma bendera kazi unayo.

NB. Wewe ni Mirindimo ninayekujua ulikua unakaa Mwananyamala ukahamia Kigamboni?
 
Ukiichoma bendera kazi unayo.
Bendera ni tambara tu wewe kama matambara mengine. Mbona watu wanachoma magauni ,suruali na nguo zao nyingine hawakamatwi?

Kwann ukamatwe ukiichoma bendera ambayo ni nguo tu? Usikariri wewe! Hatuko Korea Kaskazini hapa.

Yaani unamkamata anayechoma bendera unamwacha mama Samia anayevunja katiba?

Mimi juzi juzi tu hapa nimechoma bendera na sijakamtwa.
 
Huu ni uhalifu kama uhalifu mwingine. Usijaribu kwa Tanzania unless unafanya hivyo sirini
 
Hii koment imeandikwa na K-vant na si mtu..USIKU HUUUU[emoji15][emoji15][emoji15]
 
Ingekuwa vizuri ukiwauliza Bot.Swali langu ni kwanini uchome pesa halali?
 
View attachment 1839347
Naomba kuuliza naweza kua mshamba hivi kuchoma hela hadharani au bendera ni sahihi ??
Kifupi ni kosa la jinai na inakifungo chake.

Na siyo tu kuchoma moto bali hata kuandika maandishi yoyote au kuichakaza kwa makusudi ni kosa la jinai na ikibainika unaweza kufungwa miaka kadha.

Pesa ni mojawapo ya alama za Taifa kama ilivyo bendera ya Taifa, Wimbo wa Taifa, Katiba ya Nchi,n.k .Huruhusiwi kufanyia mzaha wowote ule.
 
Acha pang'ang'a.

Jichukue shooting ukiwa unachoma bendera. Kwakua una uhakika ni tambara tupu taja na eneo unalopatikana na jina lako, onyesha na sura.

Kama hautafanya hivyo hii mada mimi na wewe iishie hapa.
 
Hela za kufanya kazi hiyo hua ni fake na hua wanazi print kwa ruhusa maalum,hizo hela sio original,hiyo inafanyika sana USA kwenye movies na kwenye nyimbo kama hizo,

Kuchoma hela halali ni kosa la jinai na utashtakiwa na nchi husika haijalishi wewe muhusika unaishi nchi gani kwani hela hua ni mali ya nchi husika,

Hela hata ikiwa mfukoni mwako bado ni mali ya Serikali,wewe unaimiliki kwa matumizi tu,ni kama ilivyo kwa Passport kua ni mali ya Serikali.
 
Umemaliza kazi, uzi ufungwe tu.
Ndio raha ya kuwa na GT jukwaani
 

Kuna kajamaa ka USA juzi amepost akiflush dollar chooni
Nyingine anatupa kwenye maji

Ila nikafikiria labda ni printed tu hazina uhalisia
 
Nimekudharau sana leo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…