Hivi kuna maisha baada ya kifo?

Hivi kuna maisha baada ya kifo?

BU LA BIBLIA: “Walio hai wanajua kwamba watakufa; lakini wafu, hawajui lolote kamwe, wala hawana malipo tena, kwa maana kumbukumbu lao limesahauliwa. Yote ambayo mkono wako unapata kufanya, yafanye kwa nguvu zako zote, kwa maana hakuna kazi, wala utungaji wala ujuzi wala hekima katika Kaburi, mahali unapokwenda.” *—Mhubiri 9:5, 10.

Siku ya ufufuo au kiama utafufuliwa
ni kama tu ulikuwa umelala kidogo hata kama ni miaka elfu moja imepita
Na hapo mbivu na mbichi zitafahamika
 
Broo; Kwani nzi na plasmodium wameumbwa kwa mfano na sura ya Mungu?
Nzi na Plasmodium ni viumbe hai i.e. Wana uhai lakini wakifa ndo bas tena. Ukiondoa binadamu, viumbe wote tumepewa ruksa sisi binadamu tuwatawale na kuwatumia kwa mustakabali wa maisha yetu (Mwanzo 1:26-28).
BTW: Wewe hangaikia yale yanayokuhusu ww binadamu achana na habari za hao viumbe wengine kama wana roho au la na wakifa wanaenda wapi. Mtakutana huko-huko kama nao huwa wanaenda huko tunakokwenda sisi. Hahahahaaaa.
Asa hujajibu swali unaleta tu maneno walioandika binadamu kama wewe tofauti Yao ni wayahudi wa kale bac....hujasema why nzi hajaumbwa mfano wa Mungu ..hujaprove hata Kama wewe umeumbwa isitoshe mfano wa Mungu...unaleta tu hekaya za kale
 
Mkuu, hoja ya kuishi baada ya kufa imekaa kiimani zaidi.Kama huamini hivyo ni sawa Hakuna kuishi baada ya kifo. Lakini kama unaamini, basi jibu ni Ndio kuna maisha baada ya kifo.
Maana ya kufa ni pale Kitendo cha mwili kutengana na Roho iliyo ndani mwako. Ni pale mwili wako unapotwaa hali ya Umauti. Baada ya Umauti watu wenzako wanakufukia ardhini (wanakuzika) kwani huna tena maslahi/faida kwao. Mwili wako ni maiti na punde utaingia katika mchakato wa kuyarudia mavumbi(utaoza).
Roho sio kiumbe bali ni Nafsi hai au unaweza kusema roho ndiyo UZIMA.
Paka ana roho? Roho yake ikifa inaenda wapi...
 
Mkuu, sio lazima uone kila kitu ili uamini kipo. Hivi (kwa utani lakini) unapoongea na simu unaamini kwamba huyo unayeongea naye ndiye kweli yeye?
Kwa habari za roho mm naamini ipo kutokana na matendo yake yanayoonekana. e.g. Umewahi kujiuliza hivi Wale watoto /wanafunzi wanaokimbia-kimbia na kupagawa wanaona au wanasikia nini hadi wafanye hivyo? Nina hakika Umewahi kusikia mara nyingi watu wakisema ''Aisee, Huyo jamaa ana roho mbaya sana kaa naye mabali" Je, kwa nini wasiseme ana moyo mbaya? Hiyo roho wanamaanisha waliionaje/nini? hata wakaithaminisha (grade) kuwa ni mbaya?
Wewe kama ni mtu wa imani Mkristo, soma Math 15:18-20 i.e. "kile" kilicho ndani ya mtu kinajidhihirisha kwa matendo tunayoyaona kwa macho yetu kama ushuhuda.
Mkuu, inawezekana kabisa ninaunda dhana za kufikirika (Imaginations) lakini mm ninaamini sio mtu wa kwanza kukubali kwamba kuna kitu kinaitwa Roho.
Je mm ni mjanja kuliko hao wengine? Kila mtu anaweza kuamini kile anachoona ni sahihi au ni cha ukweli kwake.
Asante.
Wanafunzi wanakimbia🤣🤣mtu anaroho mbaya ..si terms tu hizo jamani... 🤣🤣Hebu tupe evidence za msingi kuhusu Simu kweli tuanze kubishana ndo maana Africa tutaendelea kuoza
 
Hii Kwa wasioamini dini(wazee wa logic and seenable things)
💥Kama umezaliwa hukuwa unajua utaish ,vip useme hamna maisha baada ya kifo ,we unatakiwa useme tu sijui maana ukisema hamna maisha manake ushajua na una elimu ingali hujakufa ukafika huko ukapata experience.
Na usijiaminishee unajua kila ktu Mana Kuna vtu vingi tu vimewashinda mfano mpak leo hamuwez hta kutibu vidonda vya tumbo kwa logic zenu kazi tu kutupa miji-antiacid,cancer imewashinda pia manake kumbe mna upungufu wa elimu .so atheist mkiulizwa kuhusu kifo mjibu hamjui.
💥Wenye Imani zetu(mnaotukebehi mkatuita wafia dini).
Tunaamini maisha yapo kwa kutumia mitume na vitabu ambavyo vimeshushwa kutupa muongozo.
Mfano waislamu sisi Tuamini hivi kuhusu kifo:
a)siku yako ya kufa watakuja malaika wengne watasimama kulia kwako na kushoto kwako haf Yule anaetoa roho atasimama sehemu ya kichwa ataamuru roho itoke na ikitoka wale malaika wengne wataichukua na kuivisha vazi flani (halijulikan namna yake) Kisha watapaa na roho kuelekea mbinguni.
b)kwa sisi waislamu mbigu zpo tabaka Saba ,so watapaa kuelekea tabaka la Saba kuipeleke hyo roho ambapo Kuna vtabu viwil Cha watu wema na waovu,na kila mbigu Ina malaika ambapo roho inapokuwa inapitishwa huulizana Ni Nani (baadhi ya malaika watakutaja kwa jina lako ulokuwa waitwa duniani)Mana lile vazi roho huvishwa huwa na harufu mbaya kwa muovu na nzuri kwa mwema.
C)Kama Ni mwema roho huenda mpak tabaka la Saba na huuandikwa kweny ktabu kinaitwa "iliyyin" ktabu ambacho huuandikwa watu wema tuu. Kama muovu huishia mbigu ya kwanza tu na hutupwa ardhini Mana Allah ameahid milango ya mbigu haitofunguliwa kwa watu waovu(mbigu kiimani Zina milango Ila haimanishi Kama hii ya nyumbani Yani Ni jina tu lakushabihisha,NB:vtu vyote ambavyo vpo baada ya kufa havifanan na hivi vyetu Ila Ni majina tu ili tuelewe Mana hakuna aliyewahi viona kwa macho). kwahyo muovu ataandkwa kweny ktabu Cha waovu kinachoitwa "sijjin".
c)uwe muovu au mwema wote roho zao ztarudishwa ardhini kweny miili yao baad ya kuzikwa Mana Allah katika suratul-twaha amesema "kutokana na hyo ardhi tmuekuumbeni(Yani adamu Mana ya ndo wa kwanza na asili yetu) na humo tutakurejesheni na tutakutoeni kwa Mara nyengne Tena (ufufuo)".
Roho zikirudishwa Kuna malaika watakuja kaburini kukuuliza maswali matatu tuu 1.Nani mola wako 2.Muhammad Ni Nani 3.umemjuaje Muhammad.
d)Kama Ni mwema,atajibu maswali yote na atakapoulizwa amemjuaje Muhammad atasema alisoma Quran.
Hvyo malaika watamuonyesha Moto aloambiwa na pepo aloahidiwa na Yale matendo mema alofanya duniani yatamjia Ni Kama kiumbe flani umbile la binadamu ,Yani kitaumbwa kiumbe kibinadamu lakini Ni matendo yake mema ili kumfariji yeye na upweke. Basi mtu mwema ataomba kiama kisimame mana ameona mambo yote na yey Ni katika walofaulu ili alipwe pepo yake.
d) Kama Ni muovu atashindwa kujibu maswali Mana atapatwa na uoga na haya maswali hujibu kwa ujanja Bali vle we ni muovu au mwema tu, akiulizwa kuhusu Muhammad atasema alikuwa anaskia watu wakisema Yani hamjui ,hvyo malaika watamuadhibu vikali , na Kuna adhabu mbalimbali Kama Kuna majoka ambayo Kama sumu yake itafika ardhini hakuna mmea utaota na Ni wakubwa wanatisha na matendo yake maovu yataubwa kuwa kiumbe kitakacho muadhibu ,na ataomba kiama kisisimame Mana atonyeshwa Moto na utafunguliwa milango yake hivyo joto lake na mrindimo wake utamfikia.
💥Haya maisha ya Kaburini yanaitwa maisha ya barzakh na Ni endelevu mpak siku ya hukumu.
NB: 1.maelezo Ni marefu nkipata mda ntaandika Uzi wa maisha ya milele kulingana na Imani yangu Mimi inshallah.
2.namsikitikia mtu anaye tarajia kufa haamini chochote manake anakufa Kama mnyama ambaye Hana akili ya kufikirii , hajipangii future yake anasubir future impangie.
Kitabu hakijashushwa kimetamkwa na muarabu mmoja wa kale aliyekuwa mjanja mjanja...Hana tofauti na tb Joshua
 
KUNA MAISHA BAADA YA KUFA KWA MUJIBU WA VITABU VITAKATIFU

Kwa mfano, tunaposoma Injili ya MATHAYO 17:3-7 katika Biblia; tunajifunza kwamba mahali hapa, Mungu alituthibitishia juu ya maisha baada ya kufa.

Musa alikuwa amekufa yapata miaka 1,700 na Eliya alikuwa ametoweka yapata miaka 1,000, lakini hapa wanaonekana wakiwa hai. .

Yesu Kristo alitoa mfano wa waliokuwa kama Tajiri yule akiongea kule Kuzimu na Ibrahimu akiomba maskini Lazaro arudi duniani kuwashudia nduguze wasiende kuteseka motoni kama Yeye ! Hapa tunafundisha kuna maisha baada ya kufariki dunia tukirejea maandiko kitabu Injili ya LUKA 16:19-31

Pia tunajifunza kwamba mwili unaweza kufa na kuoza kaburini, lakini NAFSI YA MTU HAIFI bali inaishi milele (ZABURI 16:10)

Tukumbuke Mungu ni Mungu akazidi walio hai kule mbinguni alipo Yeye
na wakatifu wake (LUKA 20:37-38).

Ni hakika kuna maisha baada ya kufa (Soma UFUNUO 6:9-11; WAFILIPI 1:21-23)
So wayahudi tu ndo Wana vitabu vitakatifu..why usituletee vya wahindi, wachina, waarabu, wagiriki na si tuone
 
Wanafunzi wanakimbia🤣🤣mtu anaroho mbaya ..si terms tu hizo jamani... 🤣🤣Hebu tupe evidence za msingi kuhusu Simu kweli tuanze kubishana ndo maana Africa tutaendelea kuoza
Mkuu; Unasema wanafunzi kukimbia ni terms tu? Kwanini wasitumie terms nyingine? Inamaana hakuna ka-ukweli fulani hapo?
Kuhusu simu nilitumia kama utani lakini ni kukuonesha tu kwamba sio lazima kila kitu uone ndo uamini. Simu yako ikidukuliwa, unaweza kuongea na mtu ambaye sio mlengwa wako. Hilo hulijui?
Hivi na wewe unaona kweli Africa tutaendelea kuoza? Mbona umetumia neno zito hivyo kana kwamba ww sio Mwafrica? Waafrica tunayo mengi ya kujivunia japokuwa ukitulinganisha na wenzetu tunaonekana bado hatujawafikia - Tunakaza mwendo broo.
 
Paka ana roho? Roho yake ikifa inaenda wapi...
Mkuu, mbona nilisema roho huwa haifi? Kama unaamini paka ana Roho hilo ni ww unaamini hivyo. Mimi siamini hivyo. Labda unieleweshe/uniaminishe vinginevyo.
Ni hayo tu.
 
Asa hujajibu swali unaleta tu maneno walioandika binadamu kama wewe tofauti Yao ni wayahudi wa kale bac....hujasema why nzi hajaumbwa mfano wa Mungu ..hujaprove hata Kama wewe umeumbwa isitoshe mfano wa Mungu...unaleta tu hekaya za kale
Labda tukubaliane kutokukubaliana kuhusu uwepo wa roho.
Tukirudi kwenye maswali yako ya msingi kwamba eti 1. Nzi na Plasmodium wana Roho? Jibu langu ni Hapana. Wewe unasemaje hapo?
2. Wanaishi vipi bila roho?
Chagua: Nikujibu kisayansi au Kiimani au vyote kwa pamoja?. Lakini uzingatie kama tumekubaliana kutokukubaliana kuwepo kwa roho.
Karibu mkuu tujadili.
 
Uoneshe hiyo roho uli iona wapi na kujua ipo.

Vinginevyo roho hiyo ni dhana ya kufikirika tu haipo katika uhalisia.
Quote1. "Uoneshe hiyo roho uli iona wapi na kujua ipo."
Hakuna mahali (Place/Space)ila najua ipo kutokana na matokeo ya matendo au Utendaji wake.
Quote 2. "Vinginevyo roho hiyo ni dhana ya kufikirika tu haipo katika uhalisia". Jibu: Sawa kabisa
Sasa wewe Je, unaweza kuthibitisha hilo?
NB: Katika hoja kama hizi ni lazima kuwe na kigezo/vigezo vya kusimamia(Terms of reference) 1. Kama hoja inajadiliwa kwa mtizamo wa Kiimani au Kisayansi.
2. Wahusika katika mjadala wanalenga hatima gani (Target). Kama ni kubishana tu for the sake of Kubishana au ni Kushirikishana mang'amuzi (Experiance)
Kwamba ni Dhana (Hypothesis) ni lazima kuwepo na proof evidence ili ku-Nullify hiyo hiyo dhana kwamba kinachoaminiwa sio cha kweli, na hakipo. Basi tukuombe sasa ww utuwekee hiyo proof hapa kwa sababu mm naamini kichwa-kichwa tu.
 
Kwanini usiishi Sasa ndugu!? Kwan usubiri mpaka ufe!?.…Maisha ndio Haya, HAKUNA MAISHA BAADA YA KIFO!
Tena akae kwa kujua kuna watu washazikwa mamilioni ya miaka huko hata huenda tunapoishi na kujenga nyumba zetu miaka hii ni maeneo ya makaburi ya hao watu ila hatujui..
 
Quote1. "Uoneshe hiyo roho uli iona wapi na kujua ipo."
Hakuna mahali (Place/Space)ila najua ipo kutokana na matokeo ya matendo au Utendaji wake.
Quote 2. "Vinginevyo roho hiyo ni dhana ya kufikirika tu haipo katika uhalisia". Jibu: Sawa kabisa
Sasa wewe Je, unaweza kuthibitisha hilo?
NB: Katika hoja kama hizi ni lazima kuwe na kigezo/vigezo vya kusimamia(Terms of reference) 1. Kama hoja inajadiliwa kwa mtizamo wa Kiimani au Kisayansi.
2. Wahusika katika mjadala wanalenga hatima gani (Target). Kama ni kubishana tu for the sake of Kubishana au ni Kushirikishana mang'amuzi (Experiance)
Kwamba ni Dhana (Hypothesis) ni lazima kuwepo na proof evidence ili ku-Nullify hiyo hiyo dhana kwamba kinachoaminiwa sio cha kweli, na hakipo. Basi tukuombe sasa ww utuwekee hiyo proof hapa kwa sababu mm naamini kichwa-kichwa tu.
Kisicho kuwepo Hakihitaji uthibitisho wa kutokuwepo kwake kwa vile hakipo kwa namna yoyote ile ya kuthibitishika.

Angalau kitu kinaweza kuwepo kwa namna mojawapo ya kuonekana, kushikika, kusikika au kuhisika.

Sasa roho haipo kwa namna yoyote ile zaidi ya mawazo ya kufikirika tu.

Haionekani, Haishikiki, Haihisiki wala haisikiki
 
Kisicho kuwepo Hakihitaji uthibitisho wa kutokuwepo kwake kwa vile hakipo kwa namna yoyote ile ya kuthibitishika.

Angalau kitu kinaweza kuwepo kwa namna mojawapo ya kuonekana, kushikika, kusikika au kuhisika.

Sasa roho haipo kwa namna yoyote ile zaidi ya mawazo ya kufikirika tu.

Haionekani, Haishikiki, Haihisiki wala haisikiki
Kisicho kuwepo Hakihitaji uthibitisho wa kutokuwepo kwake kwa vile hakipo kwa namna yoyote ile ya kuthibitishika.

Angalau kitu kinaweza kuwepo kwa namna mojawapo ya kuonekana, kushikika, kusikika au kuhisika.

Sasa roho haipo kwa namna yoyote ile zaidi ya mawazo ya kufikirika tu.

Haionekani, Haishikiki, Haihisiki wala haisikiki
Nukuu 1. " Kisicho kuwepo Hakihitaji uthibitisho wa kutokuwepo kwake kwa vile hakipo kwa namna yoyote ile ya kuthibitishika".
Mhhhh! Sio kweli mkuu. Mbona mahakamani inathibitishwa kwamba Kosa linalodaiwa kutendwa na Mtuhumiwa halikutendeka? Wewe unashindwaje kututhibitishia hilo?
Nukuu 2. "Angalau kitu kinaweza kuwepo kwa namna mojawapo ya kuonekana, kushikika, kusikika au kuhisika".
Duh! Hapana sio kweli mkuu. Mbona hatujaweza kuona mawazo, kuyashika, kuyasikia au kuyahisi? Ila tunajua yapo na yanatumiwa na watu ili kupambana na changamoto za maisha (Usiniambie habari za sonona/msongo wa mawazo)
 
Nukuu 1. " Kisicho kuwepo Hakihitaji uthibitisho wa kutokuwepo kwake kwa vile hakipo kwa namna yoyote ile ya kuthibitishika".
Mhhhh! Sio kweli mkuu. Mbona mahakamani inathibitishwa kwamba Kosa linalodaiwa kutendwa na Mtuhumiwa halikutendeka? Wewe unashindwaje kututhibitishia hilo?
Mahakamani wanajua jambo fulani limetendeka kwamba lipo ndio maana wanahitaji uthibitisho.

Kama hamna jambo lolote lililotendeka ni kwamba halipo na haina haja ya kwenda mahakamani kutaka uthibitisho.
Nukuu 2. "Angalau kitu kinaweza kuwepo kwa namna mojawapo ya kuonekana, kushikika, kusikika au kuhisika".
Duh! Hapana sio kweli mkuu. Mbona hatujaweza kuona mawazo, kuyashika, kuyasikia au kuyahisi? Ila tunajua yapo na yanatumiwa na watu ili kupambana na changamoto za maisha (Usiniambie habari za sonona/msongo wa mawazo)
Mawazo yapo kwa kuhisika, sio kwamba hayapo.

Roho haipo kwa namna yoyote ile.
 
Mkuu, hoja ya kuishi baada ya kufa imekaa kiimani zaidi.Kama huamini hivyo ni sawa Hakuna kuishi baada ya kifo. Lakini kama unaamini, basi jibu ni Ndio kuna maisha baada ya kifo.
Maana ya kufa ni pale Kitendo cha mwili kutengana na Roho iliyo ndani mwako. Ni pale mwili wako unapotwaa hali ya Umauti. Baada ya Umauti watu wenzako wanakufukia ardhini (wanakuzika) kwani huna tena maslahi/faida kwao. Mwili wako ni maiti na punde utaingia katika mchakato wa kuyarudia mavumbi(utaoza).
Roho sio kiumbe bali ni Nafsi hai au unaweza kusema roho ndiyo UZIMA.
Hapana, hii research ilifanywa na nani? Kwamba mtu akifa roho inatengana na mwili?
 
Mkuu, sio lazima uone kila kitu ili uamini kipo. Hivi (kwa utani lakini) unapoongea na simu unaamini kwamba huyo unayeongea naye ndiye kweli yeye?
Kwa habari za roho mm naamini ipo kutokana na matendo yake yanayoonekana. e.g. Umewahi kujiuliza hivi Wale watoto /wanafunzi wanaokimbia-kimbia na kupagawa wanaona au wanasikia nini hadi wafanye hivyo? Nina hakika Umewahi kusikia mara nyingi watu wakisema ''Aisee, Huyo jamaa ana roho mbaya sana kaa naye mabali" Je, kwa nini wasiseme ana moyo mbaya? Hiyo roho wanamaanisha waliionaje/nini? hata wakaithaminisha (grade) kuwa ni mbaya?
Wewe kama ni mtu wa imani Mkristo, soma Math 15:18-20 i.e. "kile" kilicho ndani ya mtu kinajidhihirisha kwa matendo tunayoyaona kwa macho yetu kama ushuhuda.
Mkuu, inawezekana kabisa ninaunda dhana za kufikirika (Imaginations) lakini mm ninaamini sio mtu wa kwanza kukubali kwamba kuna kitu kinaitwa Roho.
Je mm ni mjanja kuliko hao wengine? Kila mtu anaweza kuamini kile anachoona ni sahihi au ni cha ukweli kwake.
Asante.
Acha utani watu wapo kwenye majadiliano.
Tabia ni nini?
 
Back
Top Bottom