Hivi kuna uhusiano wa kwenda Ulaya na kufeli maisha?

Hivi kuna uhusiano wa kwenda Ulaya na kufeli maisha?

Nina washkaji zangu kama 11 hivi, Mmoja yuko JAPAN, Kyoto, Mmoja yuko UK, Brmingham, Mmoja yuko CANADA, Toronto, Mmoja yuko Denmark, Oslo, m1 yuko Namibia, Windhoek, Wa3 wako USA, Texas, California na Las Vegas Nevada, mwingine yuko zake South Africa, Cape town na mwingine anaishi TURKEY, Instanbul na wa Mwisho yuko Sehemu matata sana ARGENTINA, Iruya (Andes). Wote wana maisha mazuri tena sana wanasaidia sana ndugu zao. Ikumbukwe hawa wametokea maisha magumu tu, walikwenda huko kimasomo lkn wakabahatika kupata kazi.
Nilipata bahati ya kufika nchi 7 kati ya hizo, na niseme wazi anayeishi ARGENTINA yuko njema zaidi, yeye anafanya kazi kwenye hotel za hapo IRUYA, ana mke na watoto wa3 wazungu as You know Argentina haina wazawa weusi.

Wengi wanaotoka maisha safi kwenda nje kusoma wakirudi home wanakuwa tegemezi mifano iko mingi sana JUX ni mfano hai kabisa.

Wengi hawajitumi kwakuwa wanajua home kwao kuko njema.

Kuna jamaa tulikuwa nae Chuoni yeye Degree alichukulia Copenhagen Norway yaan hajielewi na sijui shida nini, na mwingine alitokaga kitambo ni kama bro kwangu alienda URUSI kusoma Udaktari ni mlevi sana, na ajabu anaijua dini (Muslim) ambapo aliwahi tuambia kuwa Russia kuna waislam wengi kuliko wakristo RC.

Kikubwa ni kujitambua tu. Mimi ni familia tu ila niliwahi kukaa Brazil miezi 6, nchi iko njema sana kazi nyingi nk sema changamoto ni kwamba mimi ni Muislam hivyo nililazimika kuhamia mji wa Rio de Janeiro ambako kidogo kuna misikiti angalua niweze kula chakula halali kwangu.

Vijana mupatapo fursa nje ya nchi ni muhimu sana kukumbuka shida za nyumbani na kujisevia kihela kidogo. Trick nzuri ni kutafuta demu wa kizungu afu unakuwa mwaminifu kwake maisha utayaona mtelezooooooo. Ref, MAD ICE yuko zake FINLAND, RAMA DEE Australia wanakula shushu kisa mbunye za kizungu.

Kuwa na maisha mabovu ni kujitakia.
Chief nakukumbusha kubet pia ni haramu.
 
Sasa mkuu we unadhani mtu mwenye maisha magumu Tz atakuwa na maisha mazuri akienda huko Ulaya Marekani etc?
Mtu anapigwa na maisha hapa Tz je huko? Si yatamua kabisa?

Your reasoning is illogical.

So mtu kama ni maskini kijijini akifika mjini lazima maisha yamchape pia? Ingekua hivyo watu wangeacha kufurika Dar kila siku.
 
Your reasoning is illogical.

So mtu kama ni maskini kijijini akifika mjini lazima maisha yamchape pia? Ingekua hivyo watu wangeacha kufurika Dar kila siku.
Huyu Wordsworth namkubali sana nimeshindwa kumjibu hapo.
 
Wasalaam wanajamvi.

Jamani kuna jambo linanifikirisha kwa muda sasa, hivi kuna uhusiano wowote kwa vijana wa makamo wanaorudi toka ughaibuni na kufeli maisha? Nimekutana na case Kama tatu hivi ambazo zimenivuruga kichwa. Nitazielezea kiufupi.

1. Katika hekaheka za humu duniani nilikaribishwa kwenye house party moja maeneo ya Salasala, ilisheheni mbwembwe za kila aina, nilikuwa na wadada warembo na wakaka wamotoo, kila mtu alijifanyia ni mmarekani, Siku hiyo nilijiona nimeokota dodo chini ya mchongoma kwani Kuna jamaa very presentable aliyetambulishwa Kama ndio fresh karudi zake kutoka ughaibuni alitokea kunitunuku. Hapo ndio ulikuwa mwanzo wa penzi tamu nikiwa na matarajio kibao.

Picha linaanzia huyu Bwana hana hata nyumba, kapewa nyumba na wazazi wake maeneo ya Tangi bovu ndio anaishi hapo, huyu Bwana sifa ya umalaya hakubarikiwa, yeye ni mlevi hujapata ona, akiamka asubuhi anaoga, anawasha zake muziki anaanza kunywa whiskey jamani ni asubuhi ya saa tatu, hiyo Ni mpera mpera mpaka atavyolala Sasa sita. Alikuwa anapenda kupika mwenyewe, anapika anakula kidogooo vyote najilia mie yeye anatwanga mipombe yake.. Baada ya miezi kadhaa nikaanza muuliza ana mpango gani wa maisha? Kazi au biashara hana jibu sahihi.. Nina search zoom namuonyesha nafasi za kazi jibu lake sawa nita apply, miezi inayoyoma yule bwana hastuki wala nini. Imagine mtu ana 41 anapewa pocket money na mama..

Nikaanza lalamika kwa ndugu zake wa karibu, mtoto wa baba yake mdogo akaniita faragha "Kama kweli una ndoto na maisha yako hapo unapoteza muda wako buree huyo hajarudi na kitu chochote zaidi ya begi lake na picha za kwenye barafu, huko Germany hajasoma chochote na wala huku nyumbani hajainvest kitu chochote kufupi Ni kwamba"Kaenda KUZURURA miaka Saba halafu karudi hoi.. Nikachoka na penzi likafa.. Ila penzi lake lilikuwa tamu sana hana kero, muelewa, romantic kwa kweli abarikiwe Sana na atolewe tozo kwenye kila muamala ataofanya.

2. Huyu ni kaka wa best friend wangu, siku anaondoka hadi airport tumemsindikiza akielekea UK akiahidi ahadi kedekede lazima apambane atoke kimaisha kwamba nafasi aliyoipata hawezi chezea. Jamani kaenda huko miaka sita baadae hata nauli ya kurudi ilibidi atumiwe, karudi hana hata mia yupo tu amekuwa mwamba wa kupiga virungu.

3. Huyu wa tatu nahisi ndio kamaliza Ulaya yoteee kikubwa anachomiliki Ni saa aina Seiko anadai Ni original alinunua Milan, simu yake ya smartphone, kiingereza kilichonyooka na album yake ya Google photos ikiwa imesheheni picha pambe kabisa zenye mandhali ya kuvutia sana. Nae kwa virungu na uchawa hajambo.

Sasa Hawa Ni mfano tu wa wengi wanaokwenda huko ughaibuni na kurudi tee. Hebu tuwaulize nyie mnaojiita Diaspora huko huwa mnafanya nini? Wenzenu huku nyumbani Mambo yetu ni bambam tumeoana, tuna watoto, tunaishi vizuri. Sasa huko jamani mbona Kama mnapoteza muda Ila mkitupia picha mnatuvimbia kwelikweli ilihali si uhalisia.

My Take Kama huko Mambo meusi rudini nyumbani tujenge nchi. Nyie vijana wenye ndoto za kwenda kusaka tonge huko ughaibuni nawashauri mpambane tu hapa nyumbani mtatoboa unless mkachukue elimu mrudi.
Siyo wote wanaoenda Ughaibuni wanatoboa Maisha,wapo wanao toboa,na vilevile wapo wanaofeli! Ni Kama huku Nyumbani,siyo wote uliosoma nao wametoboa life!! Maisha ndivyo yalivyo,Muwombe Mungu akupe mwisho mwema!!
 
Wasalaam wanajamvi.

Jamani kuna jambo linanifikirisha kwa muda sasa, hivi kuna uhusiano wowote kwa vijana wa makamo wanaorudi toka ughaibuni na kufeli maisha? Nimekutana na case Kama tatu hivi ambazo zimenivuruga kichwa. Nitazielezea kiufupi.

1. Katika hekaheka za humu duniani nilikaribishwa kwenye house party moja maeneo ya Salasala, ilisheheni mbwembwe za kila aina, nilikuwa na wadada warembo na wakaka wamotoo, kila mtu alijifanyia ni mmarekani, Siku hiyo nilijiona nimeokota dodo chini ya mchongoma kwani Kuna jamaa very presentable aliyetambulishwa Kama ndio fresh karudi zake kutoka ughaibuni alitokea kunitunuku. Hapo ndio ulikuwa mwanzo wa penzi tamu nikiwa na matarajio kibao.

Picha linaanzia huyu Bwana hana hata nyumba, kapewa nyumba na wazazi wake maeneo ya Tangi bovu ndio anaishi hapo, huyu Bwana sifa ya umalaya hakubarikiwa, yeye ni mlevi hujapata ona, akiamka asubuhi anaoga, anawasha zake muziki anaanza kunywa whiskey jamani ni asubuhi ya saa tatu, hiyo Ni mpera mpera mpaka atavyolala Sasa sita. Alikuwa anapenda kupika mwenyewe, anapika anakula kidogooo vyote najilia mie yeye anatwanga mipombe yake.. Baada ya miezi kadhaa nikaanza muuliza ana mpango gani wa maisha? Kazi au biashara hana jibu sahihi.. Nina search zoom namuonyesha nafasi za kazi jibu lake sawa nita apply, miezi inayoyoma yule bwana hastuki wala nini. Imagine mtu ana 41 anapewa pocket money na mama..

Nikaanza lalamika kwa ndugu zake wa karibu, mtoto wa baba yake mdogo akaniita faragha "Kama kweli una ndoto na maisha yako hapo unapoteza muda wako buree huyo hajarudi na kitu chochote zaidi ya begi lake na picha za kwenye barafu, huko Germany hajasoma chochote na wala huku nyumbani hajainvest kitu chochote kufupi Ni kwamba"Kaenda KUZURURA miaka Saba halafu karudi hoi.. Nikachoka na penzi likafa.. Ila penzi lake lilikuwa tamu sana hana kero, muelewa, romantic kwa kweli abarikiwe Sana na atolewe tozo kwenye kila muamala ataofanya.

2. Huyu ni kaka wa best friend wangu, siku anaondoka hadi airport tumemsindikiza akielekea UK akiahidi ahadi kedekede lazima apambane atoke kimaisha kwamba nafasi aliyoipata hawezi chezea. Jamani kaenda huko miaka sita baadae hata nauli ya kurudi ilibidi atumiwe, karudi hana hata mia yupo tu amekuwa mwamba wa kupiga virungu.

3. Huyu wa tatu nahisi ndio kamaliza Ulaya yoteee kikubwa anachomiliki Ni saa aina Seiko anadai Ni original alinunua Milan, simu yake ya smartphone, kiingereza kilichonyooka na album yake ya Google photos ikiwa imesheheni picha pambe kabisa zenye mandhali ya kuvutia sana. Nae kwa virungu na uchawa hajambo.

Sasa Hawa Ni mfano tu wa wengi wanaokwenda huko ughaibuni na kurudi tee. Hebu tuwaulize nyie mnaojiita Diaspora huko huwa mnafanya nini? Wenzenu huku nyumbani Mambo yetu ni bambam tumeoana, tuna watoto, tunaishi vizuri. Sasa huko jamani mbona Kama mnapoteza muda Ila mkitupia picha mnatuvimbia kwelikweli ilihali si uhalisia.

My Take Kama huko Mambo meusi rudini nyumbani tujenge nchi. Nyie vijana wenye ndoto za kwenda kusaka tonge huko ughaibuni nawashauri mpambane tu hapa nyumbani mtatoboa unless mkachukue elimu mrudi.
mtoto wa mwenye nyumba wangu karudi ana kama week 2 hapa, amekaa miaka 10 nje na yeye hivyo hivyo picha kibaoo alichorudi nacho ni rasta na kingereza tu bas zaidi kila siku ananipiga virungu.

Ni kweli ulaya shughuli ni nyingi na mtu kuingiza 500$ ni kawaida na wengi ukiwaambia hivi wakiwa bongo wanaipigia hesabu wanaona ni bonge la hela lakini kwa nje ni hela ndogo tu.

hivyo unakuta mtu anaingiza mathalani 10000$ per month lakini anataka kuishi maisha ya starehe na sawa kama wenyeji

hivyo kujikuta mwezi mzma hana anacho save na kujikuta anabakia na 100$ au zero kabisa,maana ulaya ugali nyama tu unaweza range mpka 50 -100$

hapo bado hujala milo mitatu,transport,gesi,kodi, nk maana kila kitu ni hela ndo maana kule kama ukioa kila mmoja kwenye ndoa anachangia 50/50
 
Sio kweli kwamba kila anaye kwenda ulaya hafanikiwi, inategemea ulienda kwa malengo gani.

Mfano mzuri ni mimi mwenyewe kabla sijaenda US nilikuwa nimeajiriwa Bongo kipato changu kilikuwa cha kawaida sana, mara baada ya kwenda huko na kukaa kwa muda usiozidi hata miaka minne maisha yangu niliyabadilisha kwa kiasi kikubwa… hivi tunavyoongea nimeweza kujenga nyumba mbili za kisasa na viwanja kadhaa mjini, nasomesha wadogo zangu shule za private nina usafiri mzuri ambao vijana wengi wa mjini wanautolea macho. Kitu nilichojifunza wengi wakifika nje hubweteka na kuiga maisha ya watu wa ulaya na kusahau walipotoka.
Kitu kingine wabongo wengi wanapokwenda nje huwa hawaendi kwa kufuata utaratibu wa nchi husika wao huwa wanajiripua mara baada ya kufika huko huwachukua muda mrefu kutafuta makaratasi ya kuwawezesha kuishi kihalali, kwa muda wote ambao wanafight kupata hayo makaratasi huishia kufanya kazi za kawaida ambazo kipato chake ni kidogo hivyo wanashindwa kufanya saving.
 
Tatizo kubwa ambalo nafaham lilimpata jamaa mtaani alienda majuu kufika kule badala ya kusoma akaanza kufanya kazi, hizi wanaita box, kapiga box wee lakini bills pia zipo juu, kwahiyo pesa anayopata inaishia kwenye bills, baada ya miaka kadhaa visa ikaisha akarudi.

Alirudi na computers na vifaa kadhaa akafungua biashara ya ki-stationery ambayo baada ya muda ikafeli.

Miaka na miaka bado anapambana kujitafuta kurudi katika mstari, waliobaki hapa walisoma chuo wakapata kazi/biashara wamemuacha mbali sana....

Kwahiyo tuseme wasio na kazi profesisonal huko majuu wanastruggle sana ila wenye kazi professional nadhani ndio wanatoboa.
 
Kwahiyo Joannah jamaa likiamka asubuhi linawasha redio na kuweka mizinga yake mezani. Linapiga Vodka moja linakuita linawasha kimoja linapumzika. Anapiga bia kadhaa anakuita tena anawasha cha pili mwendo ni huo hadi usiku.
Fedha zikiisha anapiga simu kwa mama yake hahaaa.
 
Waarabu wenyewe wanazimia Ulaya na NA. Ushawahi ona mtu anatoka nchi za ME au North Africa au Somalia anataka kwenda arabuni? Wanazikandia wakiwa kwao ila Wote wanataka Kuja kiwanja Mzee. Kiwanja is where it's at.
Nchi zenye amani Kama UAE,OMAN,QATAR kwa mtafutaji wa kazi naona Kama zinafaa au nakosea mkuu?
 
Inategemea na nchi…mchiz wangu alikaa UK akasema pale ni shidaaa ila alipo hamia norway akatoboa..ana mawe balaa
 
Kuwin maisha inategemea na akili ya mtu na malengo yake aliyojiwekea haijalishi yupo nchi gani,discipline,attitude na kumtegemea mwenyezi Mungu ndio kila kitu katika maisha,

Mleta mada anaposema "wengi" walioenda nje wamefeli ni anatumia hisia tu kufikia hiyo conclusion yake,au itakua ameamua tu kujifariji,hiyo reseach kaifanyia wapi na sample yake ilikua watu wangapi?

Kama mleta mada umetendwa na diaspora hilo ni tatizo lako pambana,kuponda diaspora hapa hakuwezi kuyabadili maisha yako,mind ur own business.
 
Nchi zenye amani Kama UAE,OMAN,QATAR kwa mtafutaji wa kazi naona Kama zinafaa au nakosea mkuu?

Huwezi linganisha uchumi wake na nchi kama USA au CA. Wengi wanaenda hizo nchi kufanya kazi za ndani na ujenzi kwa malipo madogo sana.

Watu wengi kwenye hizo nchi nao wanawish kwenda mbele kwenye fursa zaidi but it's a start kama uwezo wako unaishia hapo.
 
Back
Top Bottom