Hivi kuna vyombo Tanzania vinavyotetea haki za vibarua (deiwaka) ambao hawana mkataba?

Idrissou02

JF-Expert Member
Joined
Jul 31, 2018
Posts
354
Reaction score
656
Habarini wakuu,
Naombeni msaada kujibiwa swali hili
Hivi kuna vyombo vya kisheria vinavyotetea haki za kibarua almaarufu deiwaka? Naombeni mnitajie tafadhali.

Nimejaribu kuchunguza nimeona vibarua hawa wananyanyasika sana kutokana na shida zao za maisha kwa kutopewa vifaa vya kuwaweka salama wakiwa makazini, kulipwa hela ndogo sana kulingana na kazi ngumu na za muda mrefu wanazofanya na mengine mengi.

Naam watu mnaofahamu naomba mnijibu
 
Makampuni binafsi ndo wanawatesa vibarua tofauti na mashirika ya serikali ambayo angalau malipo Yao yanaafadhali, kazi masaaa nane ya kurusha kreti za soda unalipwa 6000
 

Nahisi kutakuwa na Health and Safety bodies (Mamlaka ya Afya na usalama kazini)

Muhimu serikali iweke minimum wage( mshahara wa chini kabisa) kwa kila Mtanzania, haki zake, kufanya kazi kwenye mazingira ya usalama.
 
mkuu samahani, hii ishu ina uhusiano na wewe kwa namna moja au nyingine?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…