Hivi kuna wanaoamini mapenzi ya kweli kama mimi?

Mapenzi ya kweli yapo na ni matamu sana , ni namna ya kumpata huyo mwenzi
 
Reactions: BAK
Sijawahi kukutana nayo , siamini sana kama yapo!
Ni bahati tu kukutana na mume au mke wa kufanana naye mkawa na "love chemistry", pia kuondoa imani moyo ya kuamini kwamba mapenzi ya kweli hayapo wakati si kweli .

Mapenzi ya kweli yapo , mume mwema yupo na mke mwema yupo kabisa na tupo nao mitaani, kwenye mitandao, mfano jamiiforum, Facebook n.k., makazini, kila mahali, swali ni utamjuaje, ukimjua kumpata ni rahisi sana.
Na ni vizuri sana wakati mwingine kujichanganya kuwepo kwenye matamasha, kwenye ibada, huko pia unaweza kutana na mume wako au mke wako mwema.

Kuna watu wengi wapo wanajiheshimu sana pia wakisubiria wenzi wema wa maisha yao .
Pia usiwe muoga kumwambia mtu ukweli wako juu yake kama ndiye unaye shuhudiwa kuwa ndiye mke wako au mume wako.

Woga huwa unatufanya watu wengi tupishanishwe na yule ambaye MUNGU amekusudia kuwa naye kwenye mahusiano ya kindoa.

Kwenye kitabu cha Isaya 34:16- imeandikwa hivi ," Tafuteni katika kitabu cha BWANA mkasome, hapana katika hao wote atakayekosa kuwepo, hapana mmoja atakayemkosa mwenzake, kwa maana kinywa changu kimeamuru, na roho yake imewakusanya.
Maana yake ndiyo kama nilivyoeleza hapo juu, umuhimu wa kutoka na kujichanganya kwenye ibada, mikusanyiko na matamasha , mfano ya injili nk.
 
naamini hii kitu 100%
 
sio kweli
 
Bill gate anavyote hivyo na ameachwa mkuu....hayo madudu hayana formula chief.
 
Naamini mapenzi ya kweli yapo. Yapo kabisa yapo.

Tatizo linakuja mmojawapo anapokua na ubinafsi, ama kuona mapenzi ni hisani. Yaani ni kama anafanya msaada ama faviur kuwa na wewe. Na wakati mwingine kuviziana makosa. Yaan mtu anakua amekaa kivita muda wote. Mtu anakua kwenye mahusiano kwa kujihami. Si sawa kabisa. Mtu anapaswa kuachilia moyo wake. Mapenzi si huruma wala hisani.

I love you my eternal partner. All will be well[emoji120][emoji120]
 
Reactions: BAK
NIKIRI UKWELI. NATURALLY NILIZALIWA KUPENDA, YAANI NILIANZA KUPENDA (Upendo wa kawaida) NIKIWA MDOGO SANA. kuna mgeni alikuja kututembelea akaja na binti yake, aisee nilimpenda sana ndani ya masaa tu.

ila walimwengu wameuspoil moyo wangu

Sent from my Infinix X572 using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…