Hivi kwanini Nahreel na Aika hawapati sapoti ya kutosha Bongo ili hali wako na sound ya tofauti kuzidi wasanii wengi wa kwenye A list

wanaishi bila drama hawaendi misiba ya wasanii,sherekhe wao wapo kivyao
 
Haiwezekani iwe watu wengi wapende kitu kibaya na waache kitu kizuri
Wanaozipenda ni watoto 😃 the songs are catchy. Come on bwana...
Chapati.. cha pa ti
Kwi kwi kwi kwiii nitaliaaa
Sukari nampatia sugar sukari
Unataka kuniambia kuna watu wazima wanafurahia?😂
 
Wanaozipenda ni watoto 😃 the songs are catchy. Come on bwana...
Chapati.. cha pa ti
Kwi kwi kwi kwiii nitaliaaa
Sukari nampatia sugar sukari
Unataka kuniambia kuna watu wazima wanafurahia?😂
Sasa hizo unazosema ni za watoto mbona ndio zina idadi kubwa ya streams kwenye platforms zote.
Sasa hao watoto wanasikiliza nyimbo boomplay,audiomack,YouTube na Spotify kuliko watu wazima?
 
Muziki wa bongo kizunguzungu sana, imagine singeli ndio inataka kufanywa utambulisho wa muziki ya taifa
Sema singeli iko na kitu hasa hii ya sasa ambayo waimbaji wanaandika vyakueleweka, midundo yake iko na vibe fulani hivi, ukiwa na maadali unaweza kukaza ile kikaksi ila huwezi kuipotezea ile vibe yake.
 
Sasa hizo unazosema ni za watoto mbona ndio zina idadi kubwa ya streams kwenye platforms zote.
Sasa hao watoto wanasikiliza nyimbo boomplay,audiomack,YouTube na Spotify kuliko watu wazima?
Hahahaa...ndugu mdau, hizo nyimbo zinautofauti gani na nyimbo za watoto mf. ukuti ukuti wa mnazi wa mnzai. Ni aina ambayo kabisa Bi Zuhura anaweza kuimba ikahit wiki 1 tukasahau. There's nothing special or memorable about the music they make. It lacks dimension. Haiwezi kukufanya ukawa nostalgic kama baadhi ya nyimbo nyingine

Kuhusu views nyingi, hiyo sio hoja. Ni mambo ya usasa..nyimbo nyingi mpya za sasa zinaangaliwa kwenye hizo streaming platforms kuliko za zamani au watu wenye following ambazo si kubwa
 
Hata wao wenyewe hawatulii na muziki. Labda ndiyo shida ya kufanya muziki ndani ya uhusiano wa kimapenzi.

Wakitibuana ratiba zinasimama hadi waweke mambo sawa. Ndiyo maana wanawaka na kuzima mara kwa mara.

Hata Pa One ilipotea kwa mapenzi ya hawa wawili.

Ova
 
Duh hapo nasikiliza Usinibwage nasikia kila kitu hadi back vocals.
 
Nahisi hilo kundi combination yao haikuwa perfect sana, wakibaki wawili yeye na mkewe inanoga zaidi kuliko walivyokua na wale jamaa
 
Kuna kitu unajaribu kushindana nacho na hutakuja kufanikiwa hata siku moja. Kujaribu kumuelewa na kufuatilia kila aina ya mziki ukiwa na lengo la kutafuta ukuburudishe.

Simuelewi Khadija Kopa anachoimba na Taarabu kiujumla ila haimaanishi ni mziki mbaya na msanii mbaya pia.

Pale Wasafi wana msanii anaitwa D Voice mimi simuelewi ila naamini ana fanbase yake.

Kuna rapa Marekani aliwahi sema "This shit is not for everybody.".

Don't try to be everybody, utakosoa hata pazuri.
 
Unacho kiona wewe kizuri haimanishi kilamtu anaona hivyo...
Uzuri wa kitu au mtu upo machoni au masikioni mwa mtu...
Kwahio usilazimishe mwingine aone au asikie unavyohisi wewe...
 
Itakua issue n mitonyo tu.. wasanii wa kibongo kumlipa producer hua mbinde.
. .. Joh Makin alipotea mara tu baada ya Nahreal kuacha kumpigia midundo n issue inasemekana ilikua mitonyo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…