Hivi kwanini Ubunge usiwe na kikomo ili kupisha mawazo mapya?

Hivi kwanini Ubunge usiwe na kikomo ili kupisha mawazo mapya?

Hoja maridhawa sana mkuu.

Kwa uzoefu wako na ukongwe wako katika mambo ya siasa, unadhani nini kifanyike ili kula za wananchi ziheshmiwe kitu ambacho kwa Africa nakiona ni kigumu sana labda kwa miaka mingi ijayo. Huku kwetu Afrika na Tanzania ikiwemo, aliyepo madarakani ana uhakika wa kushinda kwa 75%..Yaani akishinda mpinzani ni habari kubwa sana...nini kifanyike mkuu.
1. Kiwango cha jumla cha elimu kipande. Watu wajinga ni watu ambao ni rahisi kuwadanganya. Hakuna demokrasia kwenye ujinga. Kwa sababu, hata mfumo wa kupiga kura unataka mtu anayeweza kuchambua mambo ili kupiga kura kwa ufanisi.

2. Kiwango cha jumla cha kujiamini na ushupavu kipande. Hata wananchi wakielimika, lakini wakikosa ushupavu na kujiamini, elimu yao wataiweka mfukoni na kukubali ujinga kama tulivyoona kwenye miaka sita iliyopita mtu mmoja mjinga anaamrisha nchi ya mamilioni ya watu kufanya ujinga.

3. Kiwango cha jumla cha ushirikishwaji wa umma (inclusivity) kipande. Ushirikishwaji wa umma si tu jambo zuri kisiasa kwa kuwa litawapa wananchi wengi zaidi nafasi ya kuchangia uendeshwaji wa nchi yao na kujiona wana hisa katika nchi yao, bali pia utasaidia kupata mawazo mengi zaidi na tofauti zaidi kutoka kwa watu wengi zaidi. Mfumo wa sasa ni wa usiri na wa kuongozwa na wachache, kitu kinachopelekea nchi kuacha vipaji vingi. Suala hili limetajwa katika kitabu cha "Why Nations Fail:The Origins of Power, Prosperity and Poverty" cha Daron Acemoglu wa MIT na James A Robinson wa University of Chicago. Hiki ni kitabu kizuri kilichachambua mengi sana kuhusu suala hili.

4. Mabadiliko ya kiutamaduni. Watu wengi wanaongelea mabadiliko ya katiba, wakisema katiba bora itatupa maendeleo na uhakiki mzuri zaidi wa uongozi. Lakini, wengine tunasema, katiba mpya ni jambo zuri, hatupingi, bali, inakuwaje hata mazuri ya katiba ya sasa hatuyatumii? Hivi kweli hapa katiba ndiyo tatizo? Ama utamaduni wa hewala hewala wa watu ndiyo tatizo?

Hivi, katiba yetu mbaya ndiyo imetuletea matatizo? Au matatizo yetu ndiyo yametuletea katiba mbaya?

Sasa, mimi nasema tubadilishe utamaduni. Tuondokane na utamaduni wa hewala hewala. Tujue kudai haki zetu. Tukishaweza hilo, hata tukibadilisha katiba, kwanza tutaibadilisha vizuri. Na zaidi, tutaitumia vizuri.

Tusipoweza hilo la kuji assert, kubadilisha utamaduni na kudai haki zetu, hili la kubadilisha katiba ndugu zangu litabaki kuwa gumzo tu miaka nenda rudi. Na hata kwa muujiza likiwezekana, hiyo katiba mpya itabaki kuwa mapambo tu. Hatutaweza kuitumia.

Si tumeona rais Magufuli kakataza mikutano ya hadhara, kitu ambacho kimeruhusiwa kikatiba under "right to assembly". Wazi kabisa. Katiba, si sheria ya kawaida. Sheria mama. Rais kaja, kaitupilia mbali katiba aliyoapa kuilinda. Na hakuna yeyote aliyembishia na kumuadabisha mpaka kafariki. Sasa kama hii ya sasa wanaivunja, hiyo mpya tutahakikishaje hawataivunja hivyo hivyo bila kubadilisha utamaduni wetu?

Kwa hivyo ni muhimu tubadilishe utamadunin wetu.

5. Katiba mpya itakayoondoa ujinga wa rais kuteua tume ya uchaguzi, na kuwa na miguvu ya ajabu ajabu. Itakayostawisha mfumo wa demokrasia shirikishi zaidi na endelevu. Itakayowapa nguvu zaidi wananchi.

Wewe unaongelea term limits?

Term limit mbona cha mtoto.

Mimi nataka katiba inayoweza kuwapa wananchi nguvu za kufanya recall election.

Yani mmemchagua mbunge kwa kipindi cha miaka mitano, baada ya mwaka mmoja mkamuona huyu ovyo hafai, mkikusanya saini za kutosha mnaitisha uchaguzi nwingine na kumtoa baada ya mwaka huo mmoja!

That's better than term limits.

Mbunge anayependwa anakaa anavyotaka kama watu wanamtaka.

Mbunge asiyependwa hata miaka mitano hamalizi. Anafanyiwa recall ndani ya mwaka mmoja kama kura zinatosha.
 
Subiri yale mataahira ya mwendazake yaje, na story zao za mbowe
 
Posho za wabunge zipunguzwe kwa 80% walipwe sawa na watumishi wengine kama walimu,afisa nyuki n.k
 
1. Kiwango cha jumla cha elimu kipande. Watu wajinga ni watu ambao ni rahisi kuwadanganya. Hakuna demokrasia kwenye ujinga. Kwa sababu, hata mfumo wa kupiga kura unataka mtu anayeweza kuchambua mambo ili kupiga kura kwa ufanisi.

2. Kiwango cha jumla cha kujiamini na ushupavu kipande. Hata wananchi wakielimika, lakini wakikosa ushupavu na kujiamini, elimu yao wataiweka mfukoni na kukubali ujinga kama tulivyoona kwenye miaka sita iliyopita mtu mmoja mjinga anaamrisha nchi ya mamilioni ya watu kufanya ujinga.

3. Kiwango cha jumla cha ushirikishwaji wa umma (inclusivity) kipande. Ushirikishwaji wa umma si tu jambo zuri kisiasa kwa kuwa litawapa wananchi wengi zaidi nafasi ya kuchangia uendeshwaji wa nchi yao na kujiona wana hisa katika nchi yao, bali pia utasaidia kupata mawazo mengi zaidi na tofauti zaidi kutoka kwa watu wengi zaidi. Mfumo wa sasa ni wa usiri na wa kuongozwa na wachache, kitu kinachopelekea nchi kuacha vipaji vingi. Suala hili limetajwa katika kitabu cha "Why Nations Fail:The Origins of Power, Prosperity and Poverty" cha Daron Acemoglu wa MIT na James A Robinson wa University of Chicago. Hiki ni kitabu kizuri kilichachambua mengi sana kuhusu suala hili.

4. Mabadiliko ya kiutamaduni. Watu wengi wanaongelea mabadiliko ya katiba, wakisema katiba bora itatupa maendeleo na uhakiki mzuri zaidi wa uongozi. Lakini, wengine tunasema, katiba mpya ni jambo zuri, hatupingi, bali, inakuwaje hata mazuri ya katiba ya sasa hatuyatumii? Hivi kweli hapa katiba ndiyo tatizo? Ama utamaduni wa hewala hewala wa watu ndiyo tatizo?

Hivi, katiba yetu mbaya ndiyo imetuletea matatizo? Au matatizo yetu ndiyo yametuletea katiba mbaya?

Sasa, mimi nasema tubadilishe utamaduni. Tuondokane na utamaduni wa hewala hewala. Tujue kudai haki zetu. Tukishaweza hilo, hata tukibadilisha katiba, kwanza tutaibadilisha vizuri. Na zaidi, tutaitumia vizuri.

Tusipoweza hilo la kuji assert, kubadilisha utamaduni na kudai haki zetu, hili la kubadilisha katiba ndugu zangu litabaki kuwa gumzo tu miaka nenda rudi. Na hata kwa muujiza likiwezekana, hiyo katiba mpya itabaki kuwa mapambo tu. Hatutaweza kuitumia.

Si tumeona rais Magufuli kakataza mikutano ya hadhara, kitu ambacho kimeruhusiwa kikatiba under "right to assembly". Wazi kabisa. Katiba, si sheria ya kawaida. Sheria mama. Rais kaja, kaitupilia mbali katiba aliyoapa kuilinda. Na hakuna yeyote aliyembishia na kumuadabisha mpaka kafariki. Sasa kama hii ya sasa wanaivunja, hiyo mpya tutahakikishaje hawataivunja hivyo hivyo bila kubadilisha utamaduni wetu?

Kwa hivyo ni muhimu tubadilishe utamadunin wetu.

5. Katiba mpya itakayoondoa ujinga wa rais kuteua tume ya uchaguzi, na kuwa na miguvu ya ajabu ajabu. Itakayostawisha mfumo wa demokrasia shirikishi zaidi na endelevu. Itakayowapa nguvu zaidi wananchi.

Wewe unaongelea term limits?

Term limit mbona cha mtoto.

Mimi nataka katiba inayoweza kuwapa wananchi nguvu za kufanya recall election.

Yani mmemchagua mbunge kwa kipindi cha miaka mitano, baada ya mwaka mmoja mkamuona huyu ovyo hafai, mkikusanya saini za kutosha mnaitisha uchaguzi nwingine na kumtoa baada ya mwaka huo mmoja!

That's better than term limits.

Mbunge anayependwa anakaa anavyotaka kama watu wanamtaka.

Mbunge asiyependwa hata miaka mitano hamalizi. Anafanyiwa recall ndani ya mwaka mmoja kama kura zinatosha.
Kongole mkuu, Binafsi naona kutowajibika ndo shida kubwa Sana katika taifa letu na ugonjwa huu usipo pata dawa hata katiba ikiwa mpya hali itakuwa ile ile tu ila jina litakuwa tuna katiba mpya.

Nakuomba tuambie mifumo ya nchi ya Marekani iliyopo juu ya kufanya ukomo wa rasi katika utendaji kazi yake bila kuathiri cheo chake Kama rais wa nchi

Je mfumo huo tunaweza iga hapa Tanzania sio copy and paste bali kuchukua pointi muhimu ambazo tunaweza kuzifanyia application hapa Tanzania na kuzaa matunda ya utawala bora na uwajibikaji wa viongozi
 
Kongole mkuu, Binafsi naona kutowajibika ndo shida kubwa Sana katika taifa letu na ugonjwa huu usipo pata dawa hata katiba ikiwa mpya hali itakuwa ile ile tu ila jina litakuwa tuna katiba mpya.

Nakuomba tuambie mifumo ya nchi ya Marekani iliyopo juu ya kufanya ukomo wa rasi katika utendaji kazi yake bila kuathiri cheo chake Kama rais wa nchi

Je mfumo huo tunaweza iga hapa Tanzania sio copy and paste bali kuchukua pointi muhimu ambazo tunaweza kuzifanyia application hapa Tanzania na kuzaa matunda ya utawala bora na uwajibikaji wa viongozi
Kuwajibika hakuji hivi hivi. Kunakuja kutokana na mazingira, elimu, utamaduni, teknolojia na sheria kushurutisha watu kuwajibika.

Term limit kwenye urais Marekani ni sawa na Tanzania. Mwisho ni terms mbili.

Kwa mfumo wa Marekani, hususan kwenye urais, wananchi ni term limit tosha, kuna upinzani mkubwa kati ya vyama viwili vikubwa, na sidhani kama hata kusingekuwa na term limits, ingekuwa rahisi kwa rais yeyote kuendelea zaidi ya terms mbili.

Nafikiri, kutokana na nguvu nyingi za urais, na nature ya kazi kuwa ya kitaifa na kimataifa, case ya term limits kwenye urais inaweza kuwa appropriate zaidi ya kwenye ubunge.

Na zaidi ya term limits, tumeona Wamarekani wakitumia nguvu za kujaribu kumu impeach rais hata kabla hajamaliza termnyake ya kwanza.

Kwingine kwenye ma gavana wa majimbo, huko California kuna gavana aliyekuwepo kabla ya Arnold Schwarzenneger, alikuwa anaitwa Gray Davis. Watu wa California walimuondoa kabla hajamaliza term yake kwa kufanya recall election. Walikusanya saini za kutosha kuitisha uchaguzi, wakafanya uchaguzi kabla ya term kuisha, wakamuondoa gavana wao.
 
Sikubaliani na wewe, Kura zinatakiwa kuheshimiwa hilo ndio jambo la muhimu, mbunge hata akikaa miaka 50 kama wananchi ndio wanamtaka hakuna tatizo.
CCM waache kuiba kura tu, kila kitu kitakwenda sawa.
 
......Mkuu wananchi wananunuliwa tena kwa bei ya kutupaaaa.
Wakinunuliwa poa, nayo pia ni demokrasia.Wanakuwa wamekubali mfumo wa kununuliwa.

Demokrasia ni mfumo wa wananchi kujipangia wanachotaka, sasa wakikubali mfumo wa kununuliwa, nayo pia ni demokrasia.

Kibaya wizi wa kura , hiyo si demokrasia.
 
Binafsi sio mpenzi wa chama chochote cha siasa japo nafuatilia siasa kwa sababu siasa ina affect sekta zingine zote za kimaisha hivyo upatikanaji au uwepo wa viongozi bora ni kitu muhimu sana kwa maendeleo. Na ili tupate maendeleo, tunahitaji mawazo mbadala kila kukicha.

Inasikitisha kuona kuna watu wamekuwa 'Monopoly' wa majimbo yao miaka nenda rudi. Na kibaya zaidi kwa miaka yote waliyosimamia majimbo bado matatizo ni yaleyale. Kuna muda unashangaa kuona mbunge amekaaa kwenye hilo jimbo kwa zaidi ya miaka 20 lakini bado kila mwaka wa uchaguzi vipaumbele vyake ni vilevile. Hii ni kwa wabunge wote wa chama tawala na upinzani.

Unakuta mtu toka uchaguzi wa 2005 kwenye jimbo lake hoja zake kuu zilikuwa MAJI, AFYA NA ELIMU. Mtu huyo huyo ndani ya jimbo hilohilo mwaka 2020 anakuja na hoja zilezile na mbaya zaidi anakuwa na nguvu ya kushinda kwa sababu amesha monopolize ile nafasi. Na usishangae 2025 panapo uhai akaja kugombea na hoja zilezile.

Ni vema ukomo kwenye hizi nafasi ukaangaliwa ili kuleta mawazo mapya. Itapendeza kama mtu atakaa jimboni kwa mihula 2 tu kama ilivyo nafasi ya urais. Iwekwe sheria kuwa hairuhusiwi mtu ambae tayari ni mbunge kugombea ubunge zaidi ya mara 2. Hii itasaidia hata watu wengine wawe na access ya kula keki ya taifa na kuwatumikia wananchi. Hii itasaidia kuondoa ile dhana iliyojengeka kuwa jimbo fulani ni la fulani.

Nawasilisha.
Kwanza waulize Chadema kwanini waliondoa ukomo wa uwenyekiti wa Chama chao? Faida hizo hizo tunazitumia kwa Wabunge!
 
Wakinunuliwa poa, nayo pia ni demokrasia.Wanakuwa wamekubali mfumo wa kununuliwa.

Demokrasia ni mfumo wa wananchi kujipangia wanachotaka, sasa wakikubali mfumo wa kununuliwa, nayo pia ni demokrasia.

Kibaya wizi wa kura , hiyo si demokrasia.


Kwenye kununuliwa hapana, itakuwa ni tatizo.

Sasa hiyo itakuwa ni rushwa sasa na rushwa ni kosa!

Je wewe unaafiki uwepo wa rushwa wakati wa uchaguzi kwa kigezo cha democracy kwamba ilimradi wananchi wamekubali kununuliwa?

Ikumbukwe wananchi wengi hawana ufahamu juu ya elimu ya uraia .

Hata mambo ambayo ni haki yao badala ya kudai huomba kwa kubembeleza kana kwamba ni hisani.

Huko mikoani wananchi hawana political awareness sababu ya kukosa kuwa na elimu na maarifa.

Watu wanaishi kama wako enzi za mkoloni.

Bado wanawaogopa askari kama nini.

Mfano ilisemekana wengine wakiambiwa leteni kadi zanu za kura zinakusanywa nakwambia hata bure au kwa kurubuniwa tu.

Hawatambui kuwa Polisi ni watumishi wao wanalipwa kodi zao wawatumikie.

Wakati wa uchaguzi huko mikoani nazani wanafanya watakavyo maana sizani kama kuna raia mwenye ujasiri wa kuhoji chochote.

Umaskiini mbaya kaka.

Watu wanapewa pombe tu au T-shirt moja au mtandio au ubwabwa anauza haki yake kwa kurubuniwa.

Adui ujinga na umakini ni wabaya sana

Sasa sijui tunawaondoaje sababu kuna watu hiyo ndiyo mitaji yao!
 
Kwenye kununuliwa hapana, itakuwa ni tatizo.

Sasa hiyo itakuwa ni rushwa sasa na rushwa ni kosa!

Je wewe unaafiki uwepo wa rushwa wakati wa uchaguzi kwa kigezo cha democracy kwamba ilimradi wananchi wamekubali kununuliwa?

Ikumbukwe wananchi wengi hawana ufahamu juu ya elimu ya uraia .

Hata mambo ambayo ni haki yao badala ya kudai huomba kwa kubembeleza kana kwamba ni hisani.

Huko mikoani wananchi hawana political awareness sababu ya kukosa kuwa na elimu na maarifa.

Watu wanaishi kama wako enzi za mkoloni.

Bado wanawaogopa askari kama nini.

Mfano ilisemekana wengine wakiambiwa leteni kadi zanu za kura zinakusanywa nakwambia hata bure au kwa kurubuniwa tu.

Hawatambui kuwa Polisi ni watumishi wao wanalipwa kodi zao wawatumikie.

Wakati wa uchaguzi huko mikoani nazani wanafanya watakavyo maana sizani kama kuna raia mwenye ujasiri wa kuhoji chochote.

Umaskiini mbaya kaka.

Watu wanapewa pombe tu au T-shirt moja au mtandio au ubwabwa anauza haki yake kwa kurubuniwa.

Adui ujinga na umakini ni wabaya sana

Sasa sijui tunawaondoaje sababu kuna watu hiyo ndiyo mitaji yao!
Mkuu, democracy definition yake ni nini?

Unaelewa kwamba kuna nchi ukienda hotelini unategemewa kumpa waiter tip ya 15% ya order yako, na kuna nchi kutoa tip ni mwiko, wanaandika onyo kabisa "no tip allowed" kwa sababu inahesabiwa kuwa ni rushwa?
 
Mkuu, democracy definition yake ni nini?

Unaelewa kwamba kuna nchi ukienda hotelini unategemewa kumpa waiter tip ya 15% ya order yako, na kuna nchi kutoa tip ni mwiko, wanaandika onyo kabisa "no tip allowed" kwa sababu inahesabiwa kuwa ni rushwa?


Ni sawa lakini hebu tujadili kwa kuangalia muktadha wa mazingira ya nchi yetu.

Kwa kuzingatia kuwa kuna tatizo la adui ujinga kwa kiasi kikubwa, pia kuna tatizo la umaskini ulokithiri,

Iwapo tukiruhusu hicho wanachoita takrima hali itazidi kuwa mbaya.

Maana yake watu watakaoweza kuchaguliwa na kushinda ni wenye hela hata kama hawana Sifa za kutosha za kutumikia wananchi na wakifika kwenye uongozi watafanya wawezavyo warudishe hela zao na kutafuta za ziada wakati wa uchaguzi mwingine washinde kwa nguvu ya pesa ili hali uchumi unazidi kudumaa au kurudi nyuma.

Sikatai hizo tips pengine kwa mazingira ya baadhi ya mataifa ambayo wenzetu hawana maadui kama ujinga , umaskini, maradhi n.k
Wenzetu wako mbali kwenye mambo mengi
 
Back
Top Bottom