Hivi kwanini wasomi wa Tanzania wanaamini kuajiriwa ni Serikalini tu?

Hivi kwanini wasomi wa Tanzania wanaamini kuajiriwa ni Serikalini tu?

Na kuiba serikalini ni rahisi zaidi pia kuliko sekta binafsi.
Serikalini hamna kufukuzana kama unafukuza malaya ndani kwako! Ila sekta binafsi hutegemea na boss kaamka na kisirani kiasi gani!

Benefits ni nyingi serikalini kwa title ya mtumishi wa umma kuna privilege kibao wala huwezi compare!
 
Tatizo kubwa ni mfumo wa elimu yetu,

Tunasoma ili tuwe akina Nani, toka utoto tulishaanza kuaminishwa na wazazi, walimu, rafiki na jamaa wanaotuzunguka kuwa mafanikio ni kuwa na kazi serikalini na walimu wengi wanajivunia tulimfundisha Fulani leo ni katibu Mkuu/mkurugenzi wa wizara au taasisi Fulani kitu ambacho kinajenga mwelekeo wa wahitimu.


Njia nzuri ni Serikalini kuja na mtaala ambao umejikita zaidi kwenye ujasiriamali na ubunifu ili kuwajengea uwezo na Nia ya Kila anayehitimu kuwa na akili ya ubunifu fulani au ujasiriamali/ufanyabiashara na ajira ya Serikalini au taasisi binafsi iwe chaguo la mwisho hapo tutakuwa na Tanzania tunayoitamani.
 
Kazi kubwa ya serikali sio kudhibiti sekta binafsi bali kuitengeneza mazingira mazuri iweze kuwa na ushindani wa wafanyakazi ili waweze kulipwa vizuri.

Kutajirikia katika ajira yoyote ni jambo gumu sana sio sekta binafsi tu hata serikalini ni hivyo hivyo. Wengi wanotajirika serikalini ni wezi na mafisadi na kwa sababu sio rahisi kuwajibishwa serikalini ukifanya ufisadi tofauti na kwenye kampuni binafsi.

Trust me
Nilichokiandika hujaelewa kabisa
 
Kwahiyo tunakubaliana kuwa Tanzania hakuna Tatizo la ajira isipokuwa watu hawathamini ajira kwenye sekta binafsi.
 
Fursa nyingi zipo huko serikalini hata mabenk yangekuwa yanatoa mikopo sawasawa watu wa serikalini na kwenye sector binafsi kungekuwa level fulan ya kutia moyo halafu mikataba na uhakika wa ajira pia lingeangaliwa haiwezakan unaajiriwa unapewa kila mwaka mkataba au miaka miwili miwili huoni kama ni kichomi muda wowote ajira inakufa
Sawa lakini hapa point kubwa ya mleta mada ni kuonesha kuwa TZ hatuna sana tatizo la ajira ila tunataka ajira ya aina moja tu serikalini tu. Waganda na wakenya wanalilia hizi fursa sisi tunazikimbia kwa sababu serikali inatudekeza sana.
 
Kuna mtu wangu wa karibu anapokea 800k Take home 580k Bonus za katikati ya mwezi za kutosha ..yaani inafika mpaka milioni moja ukijumlisha na mshahara .. kasoma diploma pekee,
Shirika binafsi.. ety kwa shinikizo la wazazi kaaply ajira za serikali.. namwangalia nacheka hihiii...
Hivi nurse ngazi ya diploma serikalini analipwa Tsh ngapi vile?
Akiingia serikalini ataambulia laki tano na ushee baada ya makato. Na kibaya zaidi atatupwa vijijini ndani baada ya muda mfupi atakumbuka alipotoka.
 
Serikalini Kuna faida kuu tatu;

1. Usalama wa ajira, mtu hawezi kuwa terminated TU at the will ya mwajiri, Kuna taratibu za kumwajibisha mtumishi, private sector pia zipo Ila hazizingatiwi kama serikalini.

2. Fursa za elimu; serikalini ni rahisi kujiendeleza kielimu kuliko private sector.

3. Mikopo; kwakua serikalini Kuna usalama wa ajira, ni rahisi Kwa Taasisi za kifedha kumpatia mtumishi mkopo ukilinganisha na mwajiriwa mwingine.
 
Kuna tatizo sana kwa watanzania wasomi kuamini kuaijiriwa mpaka upate kazi serikalini. Hii mindset tunaweza kuiondoaje kwa wasomi? Mfano hai ni kwenye hizi ajira za walimu na wafanyakazi afya idadi kubwa imejitokeza kuomba ajira hizo na kupelekea kuonesha kuwa hapa Tanzania kuna tatizo kubwa la ajira kwenye hizo kada kitu ambacho si kweli.

Mimi binafasi kuna jamaa zangu watano wameajiriwa shule binafsi na wengine wana maendeleo mazuri tu mpaka kujenga lakini kila ajira zikitangazwa wanakimbizana kuomba serikalini na kuwaaribia wengine ambao hawajapata pa kujishikiza,kuna mmoja nilimpigia nikamwambia kabisa usithubutu hata kidogo kutoka hapo kibaruani ulipo eti unakuja serikalini utajutia sna,maendeleo aliyonayo mimi niliyepo serikalini hata robo simfikii lakini wazazi wake wanamshinikiza aombe serikalini kila mara. Kuna jamaa wengine tunaofahamiana wapo hospitali binafsi na wana maisha mazuri lakini na wao wana hiyo mindset.

Ushauri kwa serikali. Iandae mpango kazi wa urasimishaji ajira kwenye sekta binafsi na mashirika pamoja na waliopo serikalini. Kwa uchunguzi wangu unaonesha kuwa hawa wafanyakazi waliopo sekta binafsi hawatambuliki popote hata kodi hawalipi lakini wapo wengi sana walioajiriwa sekta binafsi. Mwenye takwimu sahihi ya idadi ya mashule na vituo vya afya binafsi alete hapa uone idadi yao ilivyokubwa na bado shule na hospitali zinaongezeka kila mwaka lakini bado watu wanasema hakuna ajira. Mtu kuajiriwa sekta binafsi anajiona kama vile amejishikiza huku akiwainda kuingia serikalini.

Ushauri mwingine kwa serikali, izidi kuwabana hawa wamiliki wa hizo taasisi binafsi wahakikishe wakitimiza mahitaji yanatakiwa kwa muajiriwa kama bima,mkataba mzuri na usalama kazini.
Swali lako kimsingi kulijibu inatakiwa ufanye utafiti juu ya trend ya ajira hapa nchini.

Na ukifanya hivyo unaweza kuta shida kubwa ilianzia awamu ya tano ambapo;

1. Serikali iliacha kuajiri kama ilivyokuwa hapo awali

Hivyo kusababisha out flow kuwa si sawa na inflow

2. Serikali ilichangia kuua sekta binafsi ambayo ilichangia kuchukua baadhi ya wahitimu.

4. Elimu bure
 
Back
Top Bottom