Hivi kweli kuna watu wanapona kwa maombi?

Hivi kweli kuna watu wanapona kwa maombi?

Kaka yangu alipona, alianza kuumwa macho akiwa form one. Alikua anatumia miwani alivyofika form four macho yakagoma kabsa kuona hata kwa miwani. Jumapili moja alikuja kuchukuliwa na mchungaji wa kanisa fulan la kilokole. Siku hiyo alirudi anaona vizuri. Nilichojifunza
1. Maombi yanaponya maradhi Ila hasa maradhi ya kurogwa.Maradhi yanayoingia mwilini kiroho Kama kurogwa hayawez kutibiwa hospital, maombi ndio suluhisho

2.Imani kwamba Mungu atakuponya ni muhimu sana, Kaka yangu yule alikua haamin kbs ktk maombi. Sisi ni wakatoliki hivyo bro alikua haamin kbs makanisa mengine. Alikua akisisitiza maneno ya kanuni ya Iman" nasadiki kwa kanisa moja takatifu katoliki la mitume" hivyo tulikua tukimlazimisha kwenda kuombewa bila yeye kupenda na hakupona. Siku aliyopona aliamua mwenyewe kwenda kuombewa na aliondoka home anasema anakwenda kuona.

3. Kama umeponywa maradhi ya kichawi inabidi uwe karibu Sana na Mungu Kwan wachawi wataendelea kukusumbua. Ndugu yangu huyu aliendelea kusumbuliwa na wachawi. Alikuja kupata homa Kali akakimbizwa akalazwa hospital Ila ajabu asubuhi yake hakuwepo hospital akaja kuokotwa porini akiwa hoi na akafariki akiwa anarudishwa hospital. Yapo matukio mengi kwake yalomkuta mpaka tukahis anarogwa, sijayaandika hapa.

4. Kuna nguvu kubwa Sana ktk maombi. Nikiwa darasa la 3 nilipoteza viatu shule, tulikua tunavua na kuweka uwanjan Kama magoli ya mpira baada ya mchezo sikuvikuta viatu vyangu. Mama akagoma kuninunulia viatu. Usiku ule nilisali Sana rozali nikamuomba Mungu anisaidie. Asubuhi nilitoka home pekua njiani niliokota elfu kumi. Nikanunua sendoz nikaenda nazo shule na Jumapili mnadani nikanunua viatu. Mara nyingi nilikua nikipata shida naomba na Mungu anajibu. Ila nilipoanza tabia ya kugongana na Mungu akaacha kunisikiliza mpaka leo. Mambo yakitulia ntarudi kanisani kwa nguvu zote.
Uko tayari kuziacha nyapi za kina shilole,lulu nk?
Upo tayari kuwapinga staff member wezi wa mali ya uma?
Upo tayari kuwapinga wafanyabiashara wezi?
Upo tayari kuwapinga wezi wa kura?
 
Hayo magonjwa ya msalaba ya kuzimu hata kama yapo lakini yakishaonyesha dalili za magonjwa ya kawaida ni ngumu kupona kwa maombi ukiona umeenda hospitali na vipimo vikaonyesha huna kitu na ww bado hujisikii vizuri haimanishi umerogwa hii science bado vitu vingi haijui mfano ugonjwa kama shizophrenia medicine inashindwa kutambua why katika ubongo kunakuwa na abnomal neurons sign inayopelekea mtu kupata halllucination na delusion
Kushindwa kwa science kuelewa pathophysiology ya ugonjwa wa shizophrenia haimanishi huyu karogwa au ana mapepo ugonjwa kama huu mtaan watasema karogwa
Nimekuelewa vizuri sana, Magonjwa yapo mengi na yote haya yapo katika magonjwa ambayo yapo hapa duniani! Somo LA msalaba wa kuzimu ni refu kidogo, na huu msalaba wa kuzimu umewekwa katika koo za hapa duniani!! Na huu msalaba una pande NNE kama msalaba wa Kawaida!! (Au yanaitwa Malango makuu manne ya kuzimu) kwa kukutajia moja wapo kuna lango LA mapepo, hili ndio linabeba matatizo mengi katika duniani kwa sasa!! (Pepo LA ulevi, pepo LA ngono, pepo LA magonjwa, nk) Katika lango hili matatizo makubwa sana hutokea katika mwili wa binadamu! Angalia sasa katika pepo LA magonjwa unaweza kuletewa ugonjwa wa aina yoyote na hosipitalini ukaonekana na ukawa unakutesa!! Hakika ugonjwa wa aina hii huponywa katika maombi!! Nitaendelea.......
 
Mkuu hapo kwenye nyapu na hela ndio shida, naamin umri ukisogea nitapokea mabadiliko. Nitaanzia hapo
Uko tayari kuziacha nyapi za kina shilole,lulu nk?
Upo tayari kuwapinga staff member wezi wa mali ya uma?
Upo tayari kuwapinga wafanyabiashara wezi?
Upo tayari kuwapinga wezi wa kura?
 
Sio kupona kwa kuombewa na matapeli kina gwajima,mwingira,mzee wa nyagi lusekelo ,kina flora etc.
 
Mimi naamini uwepo wa Mungu namuabudu pia mfuasi wa dini fulani. Lakin kwa haya mambo ya mtu kupona kwa maombi au dua tu huwa siamini. Inaezekana kweli zamani enzi za manabii watu walikuwa wanapona kweli kwa maombi/ dua lakin kwa dunia ya sasa sidhani kama kuna hki kitu. Yani mtu kupona ugonjwa kwa maombi tu bila kutumia dawa au vtu kama ivi. Ulishwahi kushuhudia mtu aliepona kwa maombi tu? Sio kushuhudia kwnye tv au kuhadithiwa namaanisha kushuhudia kwa macho yko mgonjwa/ mtu alikuwa na matatizo akawa sawa kwa maombi tu? Hpa namaanisha labda mtu ulikuwa unamuona ana struggle kwa muda mrefu baadae akaenda kwenye maombi akawa sawa. Umewai shuhudia ktu km hii?
Wiki iliyopita kaka yangu alikuwa mgonjwa sana.

Alikuwa hawezi kutembea wala kuongea.

Tumbo nalo limevimba kama limejazwa upepo..

Kakimbizwa hospitali ya rufaa ya (mabano)..

Huko vipimo vya gharama kubwa kubwa vikafanyika lakini hakuna UGONJWA WOWOTE ULIOONEKANA!!

Ikabidi awahishwe Muhimbili haraka kwa ndege ya asubuhi ( mpaka haya yote yanaendelea bro hajielewi).

Kufika huko MNH nako vipimo havioneshi kitu..

Dah imetuumiza vichwa sana, imebidi tukae tu bila tumaini.

Mungu ni mwema kwetu, mjumbe mmoja akatoa wazo tumpeleke katika kanisa lolote la walokole angalau aombewe

Taratibu zote za kumpeleka kanisani zilifanyika haraka na akafikishwa kanisani akiwa na hali mbaya sana.

Bro alipokelewa na kanisa zima, maombi yalianza rasmi bila kujali huyu ni mtu wa dini gani wala katokea wapi.

Maombi yalifanyika takribani masaa matatu kwa mgonjwa wetu, ghafla bin vuu mgonjwa alitapika vitu vya ajabu sana (sio vyema kuvielezea hapa).

Muda ule ule tumbo lilipungua, akaongea kiasi hivi na akapata nafuu.

Bado yuko Dar akiendelea na maombi.

Lesson: Mungu Yupo jamani tena anaonekana pale usipotarajia. Omba bila kikomo.
 
Ni uwongo , ni kupiga pesa . Watu walioteshwa manywele ya ajabu eti wamefufuka ! Acheni hizo ! Nafuu huyo mzee kaingia kwenye siasa . Tangu lini mtu ukatumikia mabwana wawili !

Sent from my TECNO-N2 using JamiiForums mobile app
 
Mimi naamini uwepo wa Mungu namuabudu pia mfuasi wa dini fulani. Lakin kwa haya mambo ya mtu kupona kwa maombi au dua tu huwa siamini. Inaezekana kweli zamani enzi za manabii watu walikuwa wanapona kweli kwa maombi/ dua lakin kwa dunia ya sasa sidhani kama kuna hki kitu. Yani mtu kupona ugonjwa kwa maombi tu bila kutumia dawa au vtu kama ivi. Ulishwahi kushuhudia mtu aliepona kwa maombi tu? Sio kushuhudia kwnye tv au kuhadithiwa namaanisha kushuhudia kwa macho yko mgonjwa/ mtu alikuwa na matatizo akawa sawa kwa maombi tu? Hpa namaanisha labda mtu ulikuwa unamuona ana struggle kwa muda mrefu baadae akaenda kwenye maombi akawa sawa. Umewai shuhudia ktu km hii?
Mkuu mimi ni mmoja wapo nimepona kwa maombi ugonjwa wa Pressure,shuhuda ni nyingi sana mkuu za uponyaji kwa njia ya maombi cha muhimu ni kubadilika tu,ukiacha kuishi maisha ya dhambi na kumgeukia Mungu utajua kuwa yupo na anaponya wagonjwa,just turn to God it's nice n easy...
 
Unajuaje kama maombi ndio yalikuponyesha? Hukua ukitumia njia nyingine za kujitibu..?
Kwa sababu immediately after prayer nilipona baada ya dawa za hospital kudunda na baada ya kupitia a certain procedure ambayo haikuzaa matunda
 
Kinachoponesha ni imani yako mwenyewe na wala hayo maombi hayana effect yoyote.
 
Sio kupona kwa kuombewa na matapeli kina gwajima,mwingira,mzee wa nyagi lusekelo ,kina flora etc.

Kupona kunategemea na imani ya mhusika. Unaweza ukajiombea we mwenyewe na ukapona bila kuombewa na wachungaji au mitume na manabii.
 
Kaka yangu alipata ukiziwi baada ya kuigua homa kali sana kw muda mrefu.Alizungushw hospital zote mjin hapa ikashindikana.Muhimbil waka suggest afungiwe mashine ku boost mawimbi ya sauti japo sikio moja kwakua haukua ukiziwi wa kuzaliwa hivyo wakasema ingemsaidia.
AT LAST akaja AKAPONA KWA MAOMBEZI KANISANI.Tena hiv vi kanisa ya mitaani vilivyojengwa kwa mabati hata havina majina.It was 2005 na ni mzima mpaka leo.
 
Mimi naamini uwepo wa Mungu namuabudu pia mfuasi wa dini fulani. Lakin kwa haya mambo ya mtu kupona kwa maombi au dua tu huwa siamini. Inaezekana kweli zamani enzi za manabii watu walikuwa wanapona kweli kwa maombi/ dua lakin kwa dunia ya sasa sidhani kama kuna hki kitu. Yani mtu kupona ugonjwa kwa maombi tu bila kutumia dawa au vtu kama ivi. Ulishwahi kushuhudia mtu aliepona kwa maombi tu? Sio kushuhudia kwnye tv au kuhadithiwa namaanisha kushuhudia kwa macho yko mgonjwa/ mtu alikuwa na matatizo akawa sawa kwa maombi tu? Hpa namaanisha labda mtu ulikuwa unamuona ana struggle kwa muda mrefu baadae akaenda kwenye maombi akawa sawa. Umewai shuhudia ktu km hii?
Si wangemwombea mwendazake?
Nireteeni ngwajima? Nineteen ngwajima! Nireteeni ngwajimaaaaaa
 
Huwezi kua na Imani kwa sababu unaamini tu katika Mungu ila si kuamini na kutenda katika Bwana Wetu Yesu Kristo alie Mungu.
Maana Imani bila Matendo Imekufa. Mungu/ Bwana Mungu anaweza
 
Saa inakuja, wala haiko mbali utakuwa Shuhuda wewe Mwenyewe.
Uwe na Imani, huna Imani ukiombewa unapona tu, kwa Imani ya anaekuombea.
 
Back
Top Bottom