Hivi kweli kuna watu wanapona kwa maombi?

Hivi kweli kuna watu wanapona kwa maombi?

Kama hoja ni kushuhudia wapo wengi wanaopona, lakini ni wagonjwa walioandaliwa, kiukweli labda uwe na mapepo au stress ndio maombi yanaweza kukuponyesha lakini kama ugonjwa wako ni ugonjwa halisi,hata waombeaji wote duniani wakuombee hutapona ni mpaka utumie njia halisi kama hospitali au dawa za kienyeji
Unashupaza shingo wakati comment no 1 kajieleza?
 
Kama hoja ni kushuhudia wapo wengi wanaopona, lakini ni wagonjwa walioandaliwa, kiukweli labda uwe na mapepo au stress ndio maombi yanaweza kukuponyesha lakini kama ugonjwa wako ni ugonjwa halisi,hata waombeaji wote duniani wakuombee hutapona ni mpaka utumie njia halisi kama hospitali au dawa za kienyeji

Mimi ni mmoja wa watu niliopona. Inawezekana sana tu. Sema siku zinavyozidi kwenda watu wanafake. Pia hata hawa wanaponya kwa njia ya uchawi mkubwa
 
Mkuu Ni kweli tupu.toka utoto wangu sijawahi shuhudia mtu anae umwa tatizi linalo onekana kwa macho kapona kwa MAOMBI! wengi ya waliopona Ni wale wa kipofu macho yasiyo na dalili za upofu,kiziwi,kilema wa magongo wenye ulemavu usio na dalili za kulemaa na SI wale wenye ulemavu usio na Shaka.

Watu wanapona. Kwa mtu aliezaliwa mbeya basi Hana shaka na kuona majirani walishidikana mahospital na kwawaganga wa kienyeji wakipona.
 
Sure mkuu. Nikiwa mtoto niliwahi kumuuliza Bimkubwa mmoja ambaye alikuwa Mwalimu wangu wa sayansi. Mwalimu huyu alivunjika mguu.
SWALI:
Mwalimu mbona sisi tukiugua unatwambia twende hospitali kisha tulete vyeti shuleni, lakini wewe umevunjika mguu na huendi hospitali unaombewa tuu je utapona bila kula dawa? ALIISHIA KUPATA KILEMA CHA KUDUMU KWA UZEMBE WAKE. Namimi niliangukia kichapo kila akiikumbuka SWALI LANGU Hadi Nika hamishwa shule!
HAKUNA ALIYE WAHI PONA TATIZO LINALO ONEKANA KWA MAOMBI!

Kupona inawezekana kama tatizo litakuwa limeshikiliwa na mtu Ki uchawi.
Kuna kijana alikuwa mtaani kwetu yeye alizariwa akiwa mremavu. Kuna muda walikuja watu wa mikutano ya injili, nae akapelekwa Na wazazi wake. Wazazi hawakuwa ni watu wa kusali kabisa. Walikuwa ni watu wa kuuza pombe za kienyeji.

Basi alifanyiwa maombi siku ya kwanza.
Siku ya pili
Mpka ya nne. Mabadiliko yakaanza kuonekana. Aliacha kutumia magongo na kiasi akaanza kutembea kwa miguu yake jambo kwa shida.

Basi wale waliomwombea wakatoa sharti moja tu.
Ambalo lilikuwa gumu kidog kutekelezwa.

Wao walikuwa na mkutano wa siku 7 tu.
Wazazi waliambiwa waanze kumpeleka kwenye moja ya kanisa la mitaa ya Jirani. Ambako wanamahusiano furan na hawa waliokuja na mkutano.

Sharti hilo lilikuwa gumu sana Kwa wazazi wa huyu kijana kwani ilikuwa Lazima waokoke kisha wabadili maisha yao. Kitu ambacho kilikuwa kigumu sana kwao.

Basi siku zilivyosonga mtoto akaanza kurudi kwenye ile hali yake.

Kuombewa na kupona kupo. Ila si kwa kiasi hicho ambacho tunaonyeshwa.
Mimi ni mmoja ambaepia niliwahi kuombewa na ikawa miujiza kwangu.
 
hiyo style ipo kwa wakristo tu ya kupona kwa maombi cha ajabu hawaendi muhimbili au bugando au kcmc hospital kwenda kuwaombea wote wapone hawa manabii wa kikatolic wanajificha nyuma ya watu waoongo hujifanya nimepona kwa maombi ili wapige pesa wangapi wanaomba ITV wachangiwe wakatibiwe india mbona hawaendi kwa manabii uchwara serikali kamata manabii peleka muhimbili wakawaombee vilema waliokuwa wamepata ajali ya pikipiki wote watoke wanatembea kwa siku moja au wiki sio mbaya
 
Mimi naamini uwepo wa Mungu namuabudu pia mfuasi wa dini fulani. Lakin kwa haya mambo ya mtu kupona kwa maombi au dua tu huwa siamini.

Inaezekana kweli zamani enzi za manabii watu walikuwa wanapona kweli kwa maombi/ dua lakin kwa dunia ya sasa sidhani kama kuna hki kitu. Yani mtu kupona ugonjwa kwa maombi tu bila kutumia dawa au vtu kama hivi.

Ulishwahi kushuhudia mtu aliepona kwa maombi tu? Sio kushuhudia kwnye tv au kuhadithiwa namaanisha kushuhudia kwa macho yko mgonjwa/ mtu alikuwa na matatizo akawa sawa kwa maombi tu?

Hapa namaanisha labda mtu ulikuwa unamuona ana struggle kwa muda mrefu baadae akaenda kwenye maombi akawa sawa. Umewai shuhudia ktu km hii?
Uwepo wa Mungu yupi unaemuabudu maana miungu iko mingi

Sent from my Nokia 8.1 using JamiiForums mobile app
 
Alitumia maombi tu, Kila kitu kinawezekana kama ututumia nguvu za kiroho kupambana na nguvu za mwilini.
Unachotakiwa kuanacho ni imani, Commitment na Subira
Uongo huo wewe....
 
Wengi tu Kuna jamaa alikuwa dereva na muislamu aliletwa kanisani akiwa hawez kuamka, kuongea Wala kusikia na hajitambui hata mke wake na watoto hawajui na hajui watt Ni Nini na maana ya mke!!!
alipigwa fire maombi ya Siku 14 Tena kambi, na akaanza kupona taratibu Sasa hivi mzima anafanya Kazi Yap merkez Morogoro...
Alikuwa anaunwa ugonjwa gani?
 
A
hiyo style ipo kwa wakristo tu ya kupona kwa maombi cha ajabu hawaendi muhimbili au bugando au kcmc hospital kwenda kuwaombea wote wapone hawa manabii wa kikatolic wanajificha nyuma ya watu waoongo hujifanya nimepona kwa maombi ili wapige pesa wangapi wanaomba ITV wachangiwe wakatibiwe india mbona hawaendi kwa manabii uchwara serikali kamata manabii peleka muhimbili wakawaombee vilema waliokuwa wamepata ajali ya pikipiki wote watoke wanatembea kwa siku moja au wiki sio mbaya
AJABU KUU NI KWAMBA WANAO WAOMBEA WENZAO HUENDA MAMLAKA ZA TIBA( HOSPITALI) KUPATA MATIBABU LAKINI WAOMBEWAJI HAWASTUKI
 
Mimi nimepona kwa maombi nilipo kuwa nahalisha na kutapika pia shingo ilikuwa inanisumbua nilivo pita kwa Bwana Yesu aliniponya kabisa
Mungu mkubwa tokea 2008 hadi sasa nimekunywa dawa mara 2 nikipo kuwa jkt na mdudu aliingia kwenye mkono nikapewa dawa yakutuliza maumivu cos nilikuwa naingia kwenye paper
 
Back
Top Bottom