Hivi Lissu atafanya vipi kazi na viongozi wenzake aliowatangaza ni watoa rushwa?

music mimi

JF-Expert Member
Joined
Jun 16, 2013
Posts
485
Reaction score
876
Okay, Lissu ameshinda furaha ni kubwa kwa supporters wake lakini kwa wapinzani wake ni msiba mzito. Ni msiba sio kwa kuwa tu wamepoteza nguvu kwenye chama na Mbowe kashindwa, ila msiba mzito ni wao kusemwa vibaya wakati wa kampeni.

Lissu alisema wazi chaguzi za kanda na mikoa zilijaa rushwa na viongozi wa kanda na mikoa wamepatikana kwa rushwa.

Nimemsikia akisema hayo wakati wa kampeni na hata baada ya kampeni nimemskia interview yake na Salim Kikeke akirudia ilo suala.

Soma Pia: Yanayojiri Uchaguzi Mkuu CHADEMA 2025: Tundu Lissu ashinda nafasi ya Mwenyekiti CHADEMA Taifa kwa Kura 513 sawa na 51.5%


Sijui muundo wao wa ufanyaji kazi ila naona kuna ugumu sana kwenye kufanya kazi pamoja au labda atatumia strategy gani sijui au atatumia makao makuu kwenye kila shughuli yani sioni mtu kama Wenje akimpa ushirikiano Lissu kwa awa watu awamuheshimu hata kidogo. Kazi ipo kwa kweli
 
First 90 days

Kapewa Kikombe cha moto na Kiazi cha moto πŸ˜‚
 
Rahisi sana hiyo, kuridhiana tu.
 
Wote mtawajibika kwa chair kama hamuwezi mtupishe wengine wafanye kazi habembelezwi mtu hapa.
Sio rahisi kiivyo watu kuwa loyal kwa Lissu kwa kuwa tu yeye ni Chairperson. Ni lazima kuwe na bond ya kuweza kufanya kazi pamoja. Kufukuza watu ni kuzidisha majeraha wapo wengi sana wasiomkubali karibu nusu hawakumpigia kura.
 
Kama wana akili waachie ngazi hasa Wenje
 
First 90 days

Kapewa Kikombe cha moto na Kiazi cha moto πŸ˜‚
Kwa kweli ana kazi nzito sana kukiweka chama sawa. Bila hivyo atakuwa vitani kila siku akipanga wengine wanavuruga.
 
Sio rahisi kiivyo watu kuwa loyal kwa Lissu kwa kuwa tu yeye ni Chairperson. Ni lazima kuwe na bond ya kuweza kufanya kazi pamoja. Kufukuza watu ni kuzidisha majeraha wapo wengi sana wasiomkubali karibu nusu hawakumpigia kura.
Ndio wanatakiwa wawajibike kwake uchaguzi ulishaisha kama hawana furaha ndani ys chadema waende ccm kwa mzee wasira anayezurula barabarani
 
Alyepokea rushwa, alifanyaje kazi na anayepinga na kukemea rushwa Lissu???πŸ€£πŸ€£πŸ€£πŸ€”πŸ€”πŸ€”
 
1-Wameshindwa na hawapo kwenye uongozi/ofisini.
2-Waliopo wengi walimuunga mkono Lissu wapo naye ofisini.
3-Hawajajitoa uanachama.
4-Wataletaje shida wakati hawatakuwa ofisini pamoja?
 
Wanaweza kuwa wamoja kwa maslahi ya mapana ya chama.

Kenya walitifuana sana mwisho wa siku hadi vyama pinzani vinafanya kazi pamoja. Odinga, Ruto, Uhuru wameamua kuweka maslahi ya nchi mbele.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…