Hivi Marekani haioni haya wala kujua hatari ya wanachokifanya Israel

Hivi Marekani haioni haya wala kujua hatari ya wanachokifanya Israel

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Kujiamini kwa kupitiliza kwa Marekani na Israel ndiko kunakokaribisha chuki kutoka kila upande duniani.Huwa wanafanya kile kisichopendeza kwa wenzao na wakifanyiwa wao inakuwa ni nongwa kubwa.

Raisi Biden tangu siku ya mwanzo bila kupata picha kamili ya vita vilipoanza akasema Israel inastahiki kujilinda full stop.

Baada ya hapo wamepeleka meli za kubeba ndege za kivita kwenye bahari ya Mediterranean.Ndege za mizigo tangu siku ya mwanzo zimekuwa zikipeleka shehena za silaha Israel.

Leo tena Antony Blinken ameizuru Israel na kufanya mazungumzo na Netanyahu na baadae kutoka kwenye press conference kutoa matamko.

Katika tamko lake Blinken ameeleza masikitiko yake makubwa na kutoa hisroria ya wazazi wake aliosema wametokea eneo hilo na katikati ya hotuba yake akatokwa na machozi.

Waislamu watatafsiri vipi machozi yake hayo wakati wapalestina wameshauliwa kwa malaki huko nyuma na hayo hayakumuuma.Wakati akitoa hotuba yake mauwaji yalikuwa yakiendelea Gaza ya hao hao wanawake na watoto wasio na silaha.

Kwa upande mwengine watu wenye kuwaonea huruma Hamas na wapalestina kwa ujumla wamekuwa ni watu wengi maarufu mmoja momoja na viongozi wachache nchi.Hakuna miongoni mwa majirani za Palestina na ndugu zao waislamu walioonekana kuwa na moyo wa huruma kama ule wa Marekani.Wanaacha waluliwe bila kuhoji na bila matamko.

Kwa ujumla naona kujiamini kwao na kibri cha kumiliki silaha kunawasahaulisha kwamba wanacheza na binadamu wenzao.Kilichompata kule Afghanistan na kule Ukraine inaonekana hawajapata fundisho la kutosha.
 
Kwa upande mwingine kuna Asilimia kubwa sana ya watu wanaikubali Israel na hawa Ni Silent Majority hawaongei wala kupiga Kelele....kwa hiyo usione vi video viwili vitatu twitter ukafikiri kwamba kila mtu ana chuki na Israel ....

Kama unachunguza utakuta wanaoonesha kufurahishwa na kitendo cha hamas na kutuma hashtag ya #Happy October na Ku-retweet video za mauaji wengi wao ni watu wenye asili ya Asia..

Wazungu ni mara chache ukakuta wana kiherehere cha kukimbilia mitandaoni kuonyesha hisia zao...

Ni Kweli kuna baadhi ya Mambo Israel wanavuka mipaka na kukosa ubinadamu, na haya yako wazi kabisa..

Lakini hata Hamas nao wamejivua nguo mchana kweupe kwa kudhihirisha kwamba ni wakatili zaidi ya wanyama.

Haswa baada ya video kusambaa wakionekana wakiwa wamepakia mwanamke kwenye Bodi ya Jeep akiwa uchi wa mnyama amekufa na ana majeraha halafu wanashangilia Allah Akbar...huku wakimtemea mate kichwani na walivyo na akili ndogo wakarecord wenyewe na kurusha mtandaoni.

Kitendo hiki kimeibua hasira na Chuki pia ndiyo maana hata baadhi ya wanaharakati waliokuwa mstari wa mbele kuwatetea wapalestina baadhi wamenyamaza na kurudi hatua moja nyuma...

Katika kitu ambacho ukitaka Watu wa Mataifa ya magharibi na mashirika ya misaada wakupige kisogo ni linapokuja suala la Kumjali na kumlinda mwanamke.

Na mamlaka ya Palestina ikatangaza kukubaliana na kilichofanywa na hamas....

Hamas baada ya kujua walichokifanya kimewaaibisha jana kwa unafiki wanajifanya kurecord video wakionekana wanamwachilia huru mwanamke mmoja wa kiyahudi waliyekuwa wamemshikilia mateka.....

Shame....
 
Hilo suala la palestina, mnakosea mnapolielezea katika mtazamo wa dini ya uislama, sote ni binadamu, mwislamu anamhitaji mkiristo na mkiristo anamhitaji mwislam, shida imeanza baada ya Hamas kushambuliwa Turkey ndo alijaribu kuongea Kwa kubalance, ila aliluhusu maandamano ya kupongeza mashambulizi, Iran maandamano ya kuwapongeza hamasi yalifanyika, katika mazingira kama hayo unatarajia marekani afanye nini? Ukumbuke mateka Bado wameshikiliwa.

Hapo nyumba waasi wa PKK walishambulia Turkey na kuua watu, Kwa kigezo Cha kutaka ardhi ya Turkey ili wapewe nchi Yao ya wakrudi, hatukuona Turkey anawaacha na kusema wanada haki Yao, amewatandika mpaka basi, Palestine na Israel inatakiwa iwe nchi Moja na waishi pamoja Kwa amani.
 
Kujiamini kwa kupitiliza kwa Marekani na Israel ndiko kunakokaribisha chuki kutoka kila upande duniani.Huwa wanafanya kile kisichopendeza kwa wenzao na wakifanyiwa wao inakuwa ni nongwa kubwa...
Hammas walipoanza kuwaua,kuwateka,kubaka na kuchinja mamia ya waisrael ulikuwa huoni ila majibu ya Israel kuwashambulia hammas ndio unayaona acha unafiki

Sent from my Infinix X663 using JamiiForums mobile app
 
Kujiamini kwa kupitiliza kwa Marekani na Israel ndiko kunakokaribisha chuki kutoka kila upande duniani.Huwa wanafanya kile kisichopendeza kwa wenzao na wakifanyiwa wao inakuwa ni nongwa kubwa...
Tulia, hiki kipigo ni mpaka waseme.Umeambiea usifanye fujo wewe ukafanya fujo basi upigwe tu kwani hakuna namna nyingine, na mimi nasema wapigwe tu. Israeli anataka ahakikishe kuwa ndani ya miaka zaidi ya 20 ijayo Ukanda wa Gaza uko na adabu zote.

Sent from my SM-A6050 using JamiiForums mobile app
 
Kujiamini kwa kupitiliza kwa Marekani na Israel ndiko kunakokaribisha chuki kutoka kila upande duniani.Huwa wanafanya kile kisichopendeza kwa wenzao na wakifanyiwa wao inakuwa ni nongwa kubwa...
Si mlikuwa mnashangilia juzi tu hapo, mmeanza kulialia tena?

Tuliwaambia hii issue itawatokea puani.
 
Kujiamini kwa kupitiliza kwa Marekani na Israel ndiko kunakokaribisha chuki kutoka kila upande duniani.Huwa wanafanya kile kisichopendeza kwa wenzao na wakifanyiwa wao inakuwa ni nongwa kubwa...
Kiufupi kipindi hichi hammas wamezingua wameonyesha ukatili wa hali ya juu umeona taifa hata moja wakiwatetea wapalestine zaidi ya Iran ndio imewapongeza

Sent from my Infinix X663 using JamiiForums mobile app
 
Kujiamini kwa kupitiliza kwa Marekani na Israel ndiko kunakokaribisha chuki kutoka kila upande duniani.Huwa wanafanya kile kisichopendeza kwa wenzao na wakifanyiwa wao inakuwa ni nongwa kubwa...

IMG_9999.jpg
 
Kujiamini kwa kupitiliza kwa Marekani na Israel ndiko kunakokaribisha chuki kutoka kila upande duniani.Huwa wanafanya kile kisichopendeza kwa wenzao na wakifanyiwa wao inakuwa ni nongwa kubwa...
walichofanya ulikiona?
 
Kiufupi kipindi hichi hammas wamezingua wameonyesha ukatili wa hali ya juu umeona taifa hata moja wakiwatetea wapalestine zaidi ya Iran ndio imewapongeza

Sent from my Infinix X663 using JamiiForums mobile app
Ni tabia ya watu kusahau historia ya mambo mapema na vile vile binadamu wako wenye unafiki nyoyoni mwao.Huwa wanamshangilia mtu kuokana na alichonacho na wala si kwa haki ya anachokitenda.

Maana yangu hapo watu wanaweza kuwa upande wa Israel kwa vile tu inaungwa mkono na Marekani na wote wana silaha na uchumi mkubwa na si kutokana na uzuri wa matendo yao.Hamas wanaweza wakapuuzwa kwa vile tu ni wanyonge wasiokuwa na chochote.

Matendo yaliyofanywa na Israel kwa wapalestina ni karibu robo tatu ya karne na mfanyaji huyo anafanya kwa jeuri katikati ya maazimio ya umoja wa mataifa.Karibuni hivi amepanda wazimu akawa anaingia masjidul aqsa.

Hamas wamefanya kidogo tu kujitetea imekuwa wao ndio wakosa bila kuzingatia historia.Kilichotakiwa baada ya tukio la wiki iliyopita ni kukubali makosa na kutoa haki za wapalestina na sio kuonesha kibri zaidi au kuiunga mkono kulipiza kisasi.
 
Ni tabia ya watu kusahau historia ya mambo mapema na vile vile binadamu wako wenye unafiki nyoyoni mwao.Huwa wanamshangilia mtu kuokana na alichonacho na wala si kwa haki ya anachokitenda...
kwamba walichofanya Hamas ni sahihi?
 
Ni tabia ya watu kusahau historia ya mambo mapema na vile vile binadamu wako wenye unafiki nyoyoni mwao.Huwa wanamshangilia mtu kuokana na alichonacho na wala si kwa haki ya anachokitenda...
Hivi unajitetea kwa Kubaka na kuchinja watoto wadogo? Na Kuwavua nguo wanawake na kuwaburuta huku ukiwatemea mate ukilitaja jina la Allah?

Huko ndiyo Kujitetea? Ndiyo maana mataifa kama Saudi Arabia, Quatar, Misri nk wamekaa kimya kwa maana hata wao wanastaajabu kwa kuona jina La allah linanajisiwa na watu wajinga wasio na uelewa ni ni wakati gani wa Kulitumia jina hilo.
 
Ni tabia ya watu kusahau historia ya mambo mapema na vile vile binadamu wako wenye unafiki nyoyoni mwao.Huwa wanamshangilia mtu kuokana na alichonacho na wala si kwa haki ya anachokitenda...
Wapewe haki kwa kuua raia wa Israel wasio na hatia? Acha ushabiki wa ovyo.
 
Kujiamini kwa kupitiliza kwa Marekani na Israel ndiko kunakokaribisha chuki kutoka kila upande duniani.Huwa wanafanya kile kisichopendeza kwa wenzao na wakifanyiwa wao inakuwa ni nongwa kubwa.

Raisi Biden tangu siku ya mwanzo bila kupata picha kamili ya vita vilipoanza akasema Israel inastahiki kujilinda full stop.

Baada ya hapo wamepeleka meli za kubeba ndege za kivita kwenye bahari ya Mediterranean.Ndege za mizigo tangu siku ya mwanzo zimekuwa zikipeleka shehena za silaha Israel.

Leo tena Antony Blinken ameizuru Israel na kufanya mazungumzo na Netanyahu na baadae kutoka kwenye press conference kutoa matamko.

Katika tamko lake Blinken ameeleza masikitiko yake makubwa na kutoa hisroria ya wazazi wake aliosema wametokea eneo hilo na katikati ya hotuba yake akatokwa na machozi.

Waislamu watatafsiri vipi machozi yake hayo wakati wapalestina wameshauliwa kwa malaki huko nyuma na hayo hayakumuuma.Wakati akitoa hotuba yake mauwaji yalikuwa yakiendelea Gaza ya hao hao wanawake na watoto wasio na silaha.

Kwa upande mwengine watu wenye kuwaonea huruma Hamas na wapalestina kwa ujumla wamekuwa ni watu wengi maarufu mmoja momoja na viongozi wachache nchi.Hakuna miongoni mwa majirani za Palestina na ndugu zao waislamu walioonekana kuwa na moyo wa huruma kama ule wa Marekani.Wanaacha waluliwe bila kuhoji na bila matamko.

Kwa ujumla naona kujiamini kwao na kibri cha kumiliki silaha kunawasahaulisha kwamba wanacheza na binadamu wenzao.Kilichompata kule Afghanistan na kule Ukraine inaonekana hawajapata fundisho la kutosha.
Mmeanzisha vita msivyovimudu, malizeni vita mlivyovianzisha
 
Back
Top Bottom