Hivi mashabiki wa mpira huwa mnashabikia nini haswa?

Sababu kama zifuatazo
1:kukutana na marafiki baada ya kazi

2:kupumzisha akili baada ya kazi

3: kujifunza mawili matatu (hapa ina wahusu wacheza mpira
Usisahau swali langu
Nipe faida za Ubuyu kwa mwanaume
Hoja dhaifu kabisa

Unazungumziaje ile mipira inayooneshwa usiku wa manane ambapo kila mmoja anakuwa yupo kwake??
 
Usifikiri usingizi unawanyima Uhuru starehe ya muda
Mfano hiyo saa nane kunamechi Kali kama ya Liverpool na Barcelona ww unafikiri usingizi utakuwepo?
Starehe ya mpira haielezeki
Mfano mcheza mpira ameumia lakini hataki kutoka uwanjani
 
Mambo ya kiume ya kupoteza muda wakati wenzenu wanaingiza pesa?
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23].
Mwanaume kamili eti ukashangilie wanaume wenzako 22 wanaogombania ngozi ya ng'ombe iliyoshonwa!!!.
Wanaoshabikia mpira bila kunufaika nao, ni wajinga
Haya mambo ya kiume huwezi kuelewa hata kidogo we baki huko kwenye udàku
 
Ungekua mwanaume ungeelewa vizuri zaidi ya hapo itakua kupoteza muda tuu
 
HONGERA SANA Utakuwa ni mtu wa kipekee sana, lazima una akili kubwa pia
Ni watu wachache sana wanagundua hilo, ni kweli michezo kwa ujumla ina faida nyingi sana
hasa kwa wale wadau husika mmoja kwa moja , mchezaji, waajiriwa wa tasisi za michezo,
mapato ya kodi, kiuchumi kama advertisements, washabiki kama burudani na kutumika kisiasa kuwapumbaza vijana n.k

Lakini ebu tuangalie upande wa pili:
1. Ulevi mbaya sana unagharimu pesa na muda hasa muda wa kazi /uzalishaji watu wanabishana kuhusu mpira na hapati pato lolote.

2. Ukanda wa pwani tanga ,Dar, Moro n.k watoto wa kiume wanashindwa kabisa ku concentrate masomo madarasani kisa ushabiki na mpira kila mtoto ana ndoto ya kuwa mchezaji bora, hii ni moja ya sbb wasichna kuongoza madarasani kuliko wavulana mtoto anakariri wachezaji ulaya yote darasani ZERO, na ukiangalia ajira zitokanazo na mpira ni 0.0002%ya ajira zote kwa ujumla

3. Mpira -USHABIKI ni chanzo cha umaskini , uzembe , mjini mageneni wapo watu kazi yao ni mdomo tu ushabiki wa mpira tena kibaya zaidi timu za ulaya, wazee hata wamama na watoto wanachinda njaa magengeni lakini maneno hayakaki mdomoni KAZI ZERO

4. Ushabiki wa mpira usio na tija ni janga la JAMII hasa pwani ni ulevi sawa kabisa na VIROBA, BANGI , GONGO na kwa kuutumia kisiasa kwa kuwalewesha jamii hasa vijana

5. Kwa TZ ushabiki huu wa mpira umeshamiri sana kwenye jamii ambayo ipo nyuma kielimu.

MWISHO NAOMBA RADHI KWA WALE WOTE NITAKAOWAKWAZA SIJASEMA TUSISHABIKIE MPIRA KBS HAPANA "KUNYWA ILA USIWE MLEVI"
 
Washabiki wa barca utawajua tuu
 
Kifupi mkuu hua hatushabikii mpira bali tunashabikia timu (logo ya timu).
Hata wachezaji wote pamoja na kocha wao wakiondoka halafu tukasajili wachezaji wa timu pinzani pamoja na kocha wao bado tutaendelea kushabikia timu ileile, kiufupi ni starehe ambayo imechanganyika na ka uwehu fulani hivi ( yaani ni kama vile tumelishwa ndele) huku wajanja fulani wakiendelea kupiga pesa.
 
Bora wewe uliokuwa wazi ni hekima pia
 
Aisee.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Ha ha ha ,kweli kabisa mkuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…