Una ushabiki wa kitoto sana,gharama za maisha huku pesa ikionekana kwenye circulation. I see things with my naked eyes, si maelezo ya kwenye makaratasi yasiyoendana na uhalisia.
Hauni haya kuzungumzia ukabila wakati mkulu wa kaya anautengeneza kwa bidii zote.
Kwenye ukosefu mkubwa wa ajira kweli nyani haoni kundule,ni aibu kwa Mtanzania kuisimanga nchi yoyote kuhusu ukosefu wa ajira. Toa kwanza boriti kwenye jicho lako ndiyo utaona kibanzi kwenye jicho la mwenzako.
GDP ni indicator muhimu, wewe ni ile timu ambayo inalazimisha data za hali ya uchumi zitoke tu kwenye mamlaka za serikali ili ziwe za kupikwa zilizojaa giliba na ambazo haziendani na uhalisia. Mkipewa data za World Bank mnazikataa na kusema ni mabeberu wanataka kuwakatisha tamaa lakini hao hao World Bank wakitoa msaada mnawasifia japo sifa zaidi mnampa mkuu wa kaya kuwa anakubalika kwa wadau wa maendeleo. Hypocrisy at it's highest level.
Failing projects, za Kibongo hauzioni? Simple example is ATCL, ni failure huku ikitumika nguvu kubwa kuificha aibu kwani ni mradi wa nyapara mkuu.
Unasema Kenya kuna suicides nyingi, vipi kuhusu torture, liquidations, executions, kidnappings na false cases wanazobambikwa wakosoaji wa serikali kwa upande wa Tanzania.
We una akili timamu kweli ?????
Mauaji na kujiua kisa ugumu wa maisha vinafanana???
Nilidhan nazungumza na mtu alo hai!!!!!!!!
Asa kwan mm naona na closed eyes???
I also see things with my naked eyes.
Nitajie mauaji yaliyotekelezwa na rais ya kiukabila.
Ila Kenya Kikuyu wanaua jaluo.
We sijui unazungumzia nn???
Kuhusu ATCL hilo jambo kuwa shirika linaingiza hasara bado halijathibitika maana route mpya kila msimu zinafunguliwa.
Na twaisubiri route ya kwenda Uingereza na China.Ila itizame KQ inafanya flight cancellation daily.
Sasa hv wamekimbiwa na mapilots wana shortage ya mapilots.
Tz ajira zinatolewa japo kwa uchache nadhani unasikiaga kuwa kuna walimu kiasi flan wamepata ajira ama madaktari kiasi flan wamepata ajira.
Nenda kenya wanachuo wanajiua kwa kuhofia ukosefu wa ajira na ugumu wa maisha.
Wananchi wanajiua baadhi pia kwa ugumu wa maisha.
Ajira zimefungwa MIAKA MITATU KENYA NIKAKUULIZA JE UMESHAWAHI KUSIKIA TZ AJIRA ZIMEFUNGWA TAKRIBAN HATA MWAKA????
Yani mauaji ya siasa unafananisha na ukabila.
Hivi unajielewa ww????
Umeenda mbali mpk mauaji unafananisha na kujiua.
Nimekuletea hadi video uone wananchi wa Kenya wanavyolalama je ushawahi ona Tz watu wanalalama hovyo kama hivyo???
Ebu acha hizo ww hata kama haumkubali Magufuli ila ondoa chuki na Tz usifananishe ugumu wa maisha wa Tz na Kenya.
Nikakupa mfano kuwa Tz unaweza ukawa na 100 ksh zibadilishe kwa hela za Tz hazifiki ht 6k tsh nadhan.Lakin mtz anaitumia na anafurahia maisha.
Ichukue hela hiyo hiyo kampe mkenya.
Huna hata fact naona umeongea uhemko mwingi sana basi mm nahitaji majibu ya maswali yafuatayo;
1)Nitajie mwaka ambao Tz imesitisha ajira kwa muda km Kenya ilivyofanya hata kwa miaka miwili.
2)Nitajie mauaji ya kikabila yaliyofanywa na serikali yetu km yanavyofanywa na kikuyu kwa jaluo.
3)Nitajie idadi ya wanachuo Tz waliojiua kisa kuhofia ugumu wa maisha na ukosefu wa ajira km Kenya.
-Kenya kuna mradi wa BRT umefeli wamepaka lipstick kwa barabara only brt wametulia.
-KQ inaleta hasara mpaka wanafanya flight cancellation mpk marubani wamewakimbia.
-Kuna mradi waliupanga wa kilimo cha umwagiliaji Kenya kushinei haupo na haujafanyika.
-Sgr ya kenya ishaanza kuleta matatzo uendeshaji mkubwa kuliko faida.
4)Nitajie miradi yetu inayosumbua ama iliyofeli kabbisa kama ya kenya.
NB:sina rais nayemkubali Tz toka inaumbwa lakini usifananishe maisha ya Kenya na Tanzania unakosea.