Hivi Mkuu wa Wilaya Ubungo atathibitishaje ukahaba wa hawa watu?

Hivi Mkuu wa Wilaya Ubungo atathibitishaje ukahaba wa hawa watu?

Bashir Yakub, WAKILI.
+255 714 047 241.

1. Pengine utasema ni kahaba kwasababu kavaa nguo fupi sana dizaini ya chupi au nyinginezo.

Lakini hii sio ushahidi wa mtu kuwa kahaba. Tanzania hatuna Sheria inayoelekeza(regulate) mavazi. Mtu anaweza kuvaa vyovyote vile. Na pia hakuna mavazi mtu akivaa anahesabika kahaba kwa mujibu wa sheria.

2. Pengine utasema nimemkuta amesimama sehemu fulani usiku wa manane.

Kusimama nje usiku wa manane sio ushahidi wa ukahaba/ biashara ya ngono. Wengi wetu husimama na hatufanyi hizo biashara.

Pia Tanzania hakuna kosa mtu kusimama sehemu yoyote usiku wa manane labda sehemu hiyo pawe panazuiwa kusimama na mmiliki wa pale.

Na kama mmiliki wa pale ndio hapendi mtu asimame basi hiyo sio kesi ya mkuu wa wilaya bali ya mmiliki dhidi ya aliyesimama pale. Na so far sio kesi ya ukahaba bali uvamizi wa eneo(trespass).

Kusimama nje ya Baa, nje klabu, nje ya kituo cha mabasi kama Riverside, au kurandaranda nje tu, au kuwa popote nje usiku sio kosa na sio ushahidi wa kufanya biashara ya ngono. Watu kada zote husimama maeneo hayo.

3. Pengine utasema nimemkuta lodge, guest nk. Tena akiwa na mwanaume au wanaume.

Kuwa lodge,guest na mwanaume, wanaume, au peke yako sio ushahidi wa ukahaba.

Hope hata huyo mkamataji amewahi mara kadhaa kuwa maeneo kama hayo na hakukamatwa kwa kushiriki ukahaba.

Na zaidi, mwanamke kuwa ndani ya lodge au guest peke yake au na mwanaume au wanaume(3 au 4s..me) nalo sio kosa Tanzania, na hata iwe usiku wa manane ama mchana kweupe.

4. Pengine utasema nimemkuta kwenye vile vijumba wanavyopanga vya uwanja wa fisi na mwananyamala.

Si atasema mi naishi hapo. Na hata kama umemkuta na mwanaume au wanaume atasema ndio nilikuwa nao sasa kosa liko wapi. Kuwa na mwanaume au wanaume nyumbani kwangu linakuwaje kosa nchi hii. Hata ukiwakuta wanafanya kosa liko wapi, si nchi nzima ingeishia jela kama ni hivyo.

5. Ushahidi wa Ukahaba/biashara ya ngono.

Kitu pekee kinachoweza kuthibitisha kuwa mtu fulani anafanya biashara ya ngono na mtuhumiwa akapatikana na hatia bila wasiwasi ni kimoja tu. Ni mtuhumiwa mwenyewe kukubali kuwa ni kweli anafanya biashara hiyo.

Anyway, tusiseme sana lakini hili jambo ni gumu .

Namuona Mkuu wa Wilaya akiwalipa fidia ya udhalilishaji hawa viumbe.

Tunaongelea SHERIA hatutetei wala kumkandamiza yeyote.

PIA SOMA
- Vita ya DC Ubungo na Makahaba: Mgongano wa sheria, haki na maadili

- Mkuu wa Wilaya ya Ubungo adhamiria kutokomeza biashara ya ukahaba
Bilioni 36 zitatokea wapi. ???
Tusubiri muda utaongea !
 
madada poa (makahaba) walikuwepo toka enzi za kwenye biblia. Tafuta habari ya Kahaba Rahabu kwenye biblia, au habari ya mwanamke aliyetaka kuuliwa kwa kupigwa mawe sababu ya uzinzi lakini akaokolewa na Yesu.
Wengine wakaambiwa yule anayejiona hana dhambi aanze kurusha jiwe kumpiga yule mwanamke mzinzi 😳
 
Bashir Yakub, WAKILI.
+255 714 047 241.

1. Pengine utasema ni kahaba kwasababu kavaa nguo fupi sana dizaini ya chupi au nyinginezo.

Lakini hii sio ushahidi wa mtu kuwa kahaba. Tanzania hatuna Sheria inayoelekeza(regulate) mavazi. Mtu anaweza kuvaa vyovyote vile. Na pia hakuna mavazi mtu akivaa anahesabika kahaba kwa mujibu wa sheria.

2. Pengine utasema nimemkuta amesimama sehemu fulani usiku wa manane.

Kusimama nje usiku wa manane sio ushahidi wa ukahaba/ biashara ya ngono. Wengi wetu husimama na hatufanyi hizo biashara.

Pia Tanzania hakuna kosa mtu kusimama sehemu yoyote usiku wa manane labda sehemu hiyo pawe panazuiwa kusimama na mmiliki wa pale.

Na kama mmiliki wa pale ndio hapendi mtu asimame basi hiyo sio kesi ya mkuu wa wilaya bali ya mmiliki dhidi ya aliyesimama pale. Na so far sio kesi ya ukahaba bali uvamizi wa eneo(trespass).

Kusimama nje ya Baa, nje klabu, nje ya kituo cha mabasi kama Riverside, au kurandaranda nje tu, au kuwa popote nje usiku sio kosa na sio ushahidi wa kufanya biashara ya ngono. Watu kada zote husimama maeneo hayo.

3. Pengine utasema nimemkuta lodge, guest nk. Tena akiwa na mwanaume au wanaume.

Kuwa lodge,guest na mwanaume, wanaume, au peke yako sio ushahidi wa ukahaba.

Hope hata huyo mkamataji amewahi mara kadhaa kuwa maeneo kama hayo na hakukamatwa kwa kushiriki ukahaba.

Na zaidi, mwanamke kuwa ndani ya lodge au guest peke yake au na mwanaume au wanaume(3 au 4s..me) nalo sio kosa Tanzania, na hata iwe usiku wa manane ama mchana kweupe.

4. Pengine utasema nimemkuta kwenye vile vijumba wanavyopanga vya uwanja wa fisi na mwananyamala.

Si atasema mi naishi hapo. Na hata kama umemkuta na mwanaume au wanaume atasema ndio nilikuwa nao sasa kosa liko wapi. Kuwa na mwanaume au wanaume nyumbani kwangu linakuwaje kosa nchi hii. Hata ukiwakuta wanafanya kosa liko wapi, si nchi nzima ingeishia jela kama ni hivyo.

5. Ushahidi wa Ukahaba/biashara ya ngono.

Kitu pekee kinachoweza kuthibitisha kuwa mtu fulani anafanya biashara ya ngono na mtuhumiwa akapatikana na hatia bila wasiwasi ni kimoja tu. Ni mtuhumiwa mwenyewe kukubali kuwa ni kweli anafanya biashara hiyo.

Anyway, tusiseme sana lakini hili jambo ni gumu .

Namuona Mkuu wa Wilaya akiwalipa fidia ya udhalilishaji hawa viumbe.

Tunaongelea SHERIA hatutetei wala kumkandamiza yeyote.

PIA SOMA
- Vita ya DC Ubungo na Makahaba: Mgongano wa sheria, haki na maadili

- Mkuu wa Wilaya ya Ubungo adhamiria kutokomeza biashara ya ukahaba
Muache akafie mbele kwa stroke mbele ya wasomi wakali! Ameshaanza kudaiwa 36b/-
Halafu anashitakiwa binafsi! hakuna state attorneys
 
Utakuta hata yeye kapitia wengi tu au katemwa
Haki za binadamu zina mambo mengi sana, uhuru wa mtu huwezi kuuingilia kwa kukamata

Kama ni street crawlers sawa wakamatwe kwa sababu za kiusalama na maadili
Lakini kama wanajistiri huko ni kumnyima mtu haki zake za msingi
Sitetei bali ni haki ya mtu kufanya anachotaka ili mradi havunji sheria
 
Tatizo lilinzia pale alipoita na Waandishi wa habari wakiwa na makamera yao huku Polisi wakitumia nguvu kuwatoa watu vyumban hapa ndipo alipokosea sana kavamia faragha za watu
Cross Examination Day;

Wakili:
Mhe. Mkuu wa Wilaya ijuze mahakama kiwango chako cha elimu.

Mkuu wa Wilaya:
Shahada

Wakili:
Ieleze mahakama majukumu yako kwa kifupi

Mkuu wa Wilaya:
Mwakilishi wa Mhe. Rais Wilaya ya Ubungo na Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama Wilaya

Wakili:
Je! Unawafahamu madada 36 walioko hapa mahakamani

Mkuu wa Wilaya:
Siwafahamu

Wakili:
Ilikuwaje ukaamuru Polisi wawakamate na kuwashikilia mahabusu?

Mkuu wa Wilaya:
Ni 'madada Poa'

Wakili:
Mhe. Mkuu wa Wilaya ieleze mahakama unamaanisha nini unaposema hawa ni 'Madada Poa?'

Mkuu wa Wilaya:
'Madada Poa' ni wanawake wanaojishughulisha na biashara haramu ya kuuza miili yao.

Wakili:
Je! Ulijuaje madada hawa wanafanya hiyo biashara uliyoisema?

Mkuu wa Wilaya:
Niliwakuta wamesimama usiku Sinza

Wakili:
Je! Ulipowakuta walikuuzia wewe miili yao

Mkuu wa Wilaya:
Hapana

Wakili:
Je! Unaweza ukataja majina ya wateja (wanaume) waliokuwa wananunua miili ya hawa madada?

Mkuu wa Wilaya:
Sikuwaona.

Wakili:
Unafahamu maana ya biashara

Mkuu wa Wilaya:
Biashara ni shughuli ya kuuza na kununua bidhaa au huduma

Wakili:
Je! kusimama Sinza usiku ni kufanya biashara

Mkuu wa Wilaya:
Hapana

Wakili:
Je! Kusimama Sinza usiku ni kosa la Jinai?

Mkuu wa Wilaya:
Hapana

Wakili:
Je! Unafahamu kuwaita madada hawa jina ulilowaita na kuwaweka kwenye Vyombo vya Habari ni kuwadhalilisha na kutweza utu wao mbele ya waume zao, familia zao na umma kwa ujumla (Defamation)?

Mkuu wa Wilaya:
Ndio

Wakili:
Je! Unafahamu kuwakamata watu na kuwashikilia rumande Polisi kwa muda wa ziadi ya siku tano pasipo kuwapeleka mahakamani ni kinyume cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai, Sura 20?

Mkuu wa Wilaya:
Najua

Wakili:
Kwa hiyo umefanya makusudi kuvunja Sheria za nchi?

Mkuu wa Wilaya:
Hapana. Nilikuwa nasafisha Wilaya yangu ya Ubungo

Wakili:
Je! Unamaanisha hawa madada ni takataka?

Mkuu wa Wilaya:
Hapana

Wakili:
Mhe. Hakimu sina maswali zaidi.
 
Bashir Yakub, WAKILI.
+255 714 047 241.

1. Pengine utasema ni kahaba kwasababu kavaa nguo fupi sana dizaini ya chupi au nyinginezo.

Lakini hii sio ushahidi wa mtu kuwa kahaba. Tanzania hatuna Sheria inayoelekeza(regulate) mavazi. Mtu anaweza kuvaa vyovyote vile. Na pia hakuna mavazi mtu akivaa anahesabika kahaba kwa mujibu wa sheria.

2. Pengine utasema nimemkuta amesimama sehemu fulani usiku wa manane.

Kusimama nje usiku wa manane sio ushahidi wa ukahaba/ biashara ya ngono. Wengi wetu husimama na hatufanyi hizo biashara.

Pia Tanzania hakuna kosa mtu kusimama sehemu yoyote usiku wa manane labda sehemu hiyo pawe panazuiwa kusimama na mmiliki wa pale.

Na kama mmiliki wa pale ndio hapendi mtu asimame basi hiyo sio kesi ya mkuu wa wilaya bali ya mmiliki dhidi ya aliyesimama pale. Na so far sio kesi ya ukahaba bali uvamizi wa eneo(trespass).

Kusimama nje ya Baa, nje klabu, nje ya kituo cha mabasi kama Riverside, au kurandaranda nje tu, au kuwa popote nje usiku sio kosa na sio ushahidi wa kufanya biashara ya ngono. Watu kada zote husimama maeneo hayo.

3. Pengine utasema nimemkuta lodge, guest nk. Tena akiwa na mwanaume au wanaume.

Kuwa lodge,guest na mwanaume, wanaume, au peke yako sio ushahidi wa ukahaba.

Hope hata huyo mkamataji amewahi mara kadhaa kuwa maeneo kama hayo na hakukamatwa kwa kushiriki ukahaba.

Na zaidi, mwanamke kuwa ndani ya lodge au guest peke yake au na mwanaume au wanaume(3 au 4s..me) nalo sio kosa Tanzania, na hata iwe usiku wa manane ama mchana kweupe.

4. Pengine utasema nimemkuta kwenye vile vijumba wanavyopanga vya uwanja wa fisi na mwananyamala.

Si atasema mi naishi hapo. Na hata kama umemkuta na mwanaume au wanaume atasema ndio nilikuwa nao sasa kosa liko wapi. Kuwa na mwanaume au wanaume nyumbani kwangu linakuwaje kosa nchi hii. Hata ukiwakuta wanafanya kosa liko wapi, si nchi nzima ingeishia jela kama ni hivyo.

5. Ushahidi wa Ukahaba/biashara ya ngono.

Kitu pekee kinachoweza kuthibitisha kuwa mtu fulani anafanya biashara ya ngono na mtuhumiwa akapatikana na hatia bila wasiwasi ni kimoja tu. Ni mtuhumiwa mwenyewe kukubali kuwa ni kweli anafanya biashara hiyo.

Anyway, tusiseme sana lakini hili jambo ni gumu .

Namuona Mkuu wa Wilaya akiwalipa fidia ya udhalilishaji hawa viumbe.

Tunaongelea SHERIA hatutetei wala kumkandamiza yeyote.

PIA SOMA
- Vita ya DC Ubungo na Makahaba: Mgongano wa sheria, haki na maadili

- Mkuu wa Wilaya ya Ubungo adhamiria kutokomeza biashara ya ukahaba
Labda wakikubali kupata mikopo Kwa maana watakuwa wamekubali kufanya ukahaba pia inaweza Ikawa njia rahisi ya kukwepa mtego wa maswali yako, japo hakuna asiyependa pesa, Swali fikirishi je hiyo mikopo Wana biashara za kuwezesha kulipa marejesho, (kulipa mkopo)
 
Huyo DC hakupaswa kuendelea kuwa katika ofisi ya umma mpaka sasa hivi, ni kwa vile tu nchi hii individual freedom rights sio kitu cha kutiliwa maanani sana.
 
Vijana kwa wazee, wote wanasimama na dada poa, hadi raha.....

#freedadapoa #freezeutamu
Wakimaliza kuwadhalilisha wanaodaiwa dada poa watahamia kwa michepuko, madanga na watu wanaoishi kama mume na mke bila ndo mwisho mnashangaa mmegeuka kama Iran au Afghanistan hakuna hata kuingia chumbani wawili kama hamna cheti cha ndoa.
 
Wilaya ya ubungo inaongoza kwa baraka mbovu DSM angeshughulikia hilo kwanza tungemshukuru sana.
 
Back
Top Bottom