Hivi mnaosoma kozi kama Bsc in Physics, Bsc in Chemistry, Bsc in Mathematics huwa mnapanga kuja kuwa kina nani hasa?🀣

Huu ni uongo uliotukuka, mtu amesoma bachelor ya Physics anakuwaje mwalimu wa physics na hajasoma education????

Mfano hai kaka yangu alisoma hii kozi pale UDOM na sasaivi akiomba hizi ajira ualimu wa Physics anachaguliwa lakini akifika kituo cha kazi wanamtoaa wanamwambia hana vigezo vya kuwa mwalimu sababu hajasomea ualimu labda akasome kozi flani hivi sijui ndo ualimu ila ni mwaka mmoja pale openi university
 
Yawezekana kwa kuwa mwalimu wa chuo kikuu maana wana taratibu zao tofauti za kupata walimu.
 
Siku hizi ikishaitwa "degree" inatosha.Bila kujali kasomea nini.
 
Wakatu mwingine usemacho kinaweka wazi ufinyu wako wa mawazo. Hizi kozi ni pana kwa mfano wa BSc in Physics wanasoma aviation pia wanaweza fanya kazi airport, wanaopiga x ray mahospitali pia wafizikia wapo. Kwa hiyo jambo usilolijua ni usiku wa giza.
 
Mwambie asihangaike na ualimu mwambie akapige post graf ya eng.. ashift to technology kuliko ualimu.
 
Wapo Tanzania au huko nje ya Nchi alfu mbona hata mimi Bachelor of Archaelogy naweza kuwa Computer progammer

Suala sio zinawasaidiaje Suala wanaajiriwa wapi kama nani TANZANIA
Ata accountant all is possible, so ilimradi hesabu tu haahaha
 
Excellent πŸ‘πŸ‘πŸΏpopote ulipo kunywa pepsi big nakuja kulipia🚢🏿
 
Kuwa na taaluma inayoeleweka at least inapunguza stress. Kuliko kusoma taaluma isioleweka.

Yaani hata ukiulizwa kitaaluma wewe ni nani unapata tabu sana kuelezea.

Sasa hawa watu wanaomba kazi za ualimu, kwanini hawakusoma tu ualimu wajue moja.
wanaotengeneza mabomu na simu na vingne vingi wengi wao wamesoma physics tu au mathematics tu au chemistry. kwa tanzania wengi wanaishia kuwa walimu lakini sio lengo la hzo course. tanzania ipo nyuma kiuchunguzi wa kisayansi ndio maana unawadharau hao wanaosoma hizo course. sehemu kama iran na marekani maprofesa wa physics wanaheshmika na wana ulinzi mkali mana akitekwa yule mjiandae kulipuliwa na mibomu mipya
 
Kwa anayesoma BSc in Chemistry, BSc Physics au BSc in Mathematics na akaimanya vizuri hawezi kufa njaa mtaani.
Mark my words
 
Hakuna shule isiyotaka mwalimi wa Physics, Chemistry au Mathemtics. Zina shavu balaa.

Dogo langu moja lilimaliza BSc Educstion kwa major ya Chemistry na Mathematics likapata shavu kubwa mjini Dsm shule moja hivi ya kitabe sana na mshahara juu.

Narudia tena, hizo degree za sayansi zinalipa sana
 
M
Hawa ni baadhi tu ya computer Scientists wenye degrees za mathematics na physics.Wewe kazi kubisha hata facts huna.Computer bila mathematics sio computer

Charles babbage
Von Neumann
Alan turing
Ada lovelace
Alonzo Church
Mitaala ni tofauti aisee wenzetu wanafundishwa kuapply sana knowledge yao hususani katika ku innovate na kudiscover technology mpya, tofauti na bongo ambapo hao watu wa BSC in maths wanaenda kujifunza wha is a computer chuoni kwa mara ya kwanza. Mtu katoka mwanza vijijini hata kuwasha computer hajui ndio anaenda kufundishwa chuo ,huyu hataweza kuinnovate wala kugundua chochote aisee tofauti na wenzetu ambapo mtoto wa primary tayari anagonga codes
 
Mm ni graduate wa BSC. chem. mwaka 2015, tuligraduate watu 24 mwaka wetu katka darasa wetu watu 7 wako ofisi ya mkemia mkuu, wa4 wako TBS,mmoja yupo tume ya madini TMC,waliobaki ni ma HOD kwny viwanda vya vinywaji,madawa na mafuta...na hakuna aliyebak mtaan
 

Mambo ya Physics hayo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…