Hivi mtu akishateuliwa kiongozi huwa akili zake zinaongezeka mara dufu?

Hivi mtu akishateuliwa kiongozi huwa akili zake zinaongezeka mara dufu?

Raia Fulani

JF-Expert Member
Joined
Mar 12, 2009
Posts
11,478
Reaction score
3,659
Huwa sielewe kwa kweli. Hasa nikiangazia teuzi za mawaziri. Unakuta leo waziri yupo wizara hii, kesho kateuliwa kule na keshokutwa kaletwa huku. Na kila unapomwona kwenye wizara mpya anaongea kama alikuwa hapo miaka kumi iliyopita.

Kuna wakati Bashungwa alikuwa waziri wa viwanda. Siku alialikwa pale Sheraton kukutana na wadau. Akaweka mikakati yake wee na kuunda timu ya ufuatiliaji na kuahidi kuona matokeo. Baada ya muda kama wiki 4 hivi akatolewa wizara hiyo, sikumbuki alienda wizara gani. Nilitamani sana kujua ni upi mwendelezo wa alichokianzisha. Najua kiliishia njiani tu japo lilikuwa wazo jema sana.

Tatizo ni hilo kila wizara. Yani mawaziri wamefanywa wanasesere. Aliyebaki na heshima wizarani ni Katibu Mkuu tu.

Sasa kilichonifanya kuandika haya ni kwamba natazama tbc hapa namwona Kijaji akitiririka na masuala ya maxingira utadhani alikuwa wizarrani hapo miaka mitano iliyopita. Wiki moja tu nyuma alikuwa waziri wa viwanda na alikuwa akitiririka kama alianzisha wizara. Wiki hiyohiyo Jery Silaa alikuwa wizara ya ardhi na ghafla akapelekwa Mawasiliano. Yani pale alipokuwa anaanza kuchanganya akatolewa. Hadi wananchi wakachukia. Kesho ukimsikiliza Silaa utadhani alikuwa mawasiliano miaka 7 iliyopita.

Tatizo hapa ni mteuzi kutuona wananchi ni maboya sana. Kwamba anaamka tu na pengine kwa maslahi binafsi anatengua uwaziri wa waziri fulani na kuhamisha huku na kule. Ni kama vile Raisi huwa na akilli za watanzania wote. Sasa nimefikiri nikaona yafuatayo;

1. Mteuzi awe na limit ya kuteua na kutengua. Mara mbili tu!

2. Waziri akae wizara husika angalau miaka mitatu bila kusumbuliwa na hamahama

3. Waziri akishindwa kudeliva hakuna haja ya kumhamisha. Ni kutengua tu

4. Waziri akideliva hakuna sababu ya kumhamisha. Ni kuvuruga malengo na kumharibia utendaji

5. Katibu mkuu wizara asitokane na uteuzi bali ushindani na ajira yake itokane na hekima za bodi
 
Kuanzia Rais, Mawaziri hadi wakuu wa mikoa huandaliwa kitu cha kuongea na huandikiwa hutuba.

Kama ni ziara ya kutembelea miji kadhaa au vijiji kadhaa huandaliwa talking notes ambazo zinaendana na sehemu atakapokuwa. Baada ya kuwa na talking notes anaweza kuongeza mbwembwe zake kama ana uzoefu.
 
Kuanzia Rais, Mawaziri hadi wakuu wa mikoa huandaliwa kitu cha kuongea na huandikiwa hutuba.

Kama ni ziara ya kutembelea miji kadhaa au vijiji kadhaa huandaliwa talking notes ambazo zinaendana na sehemu atakapokuwa. Baada ya kuwa na talking notes anaweza kuongeza mbwembwe zake kama ana uzoefu.
Narudi palepale kwamba hawa nawaziri hufanywa vikaragosi wasiokuwa na misimamo yao
 
Nyuma yake anakua na jopo la wataalam kwanini asionekane na akili
Mfano tuchukulie aliyekuwa waziri wa ardhi, kwa hiyo baada ya kuwasikiliza wananchi hurudi nyuma kupokea nondo toka kwa watendaji kisha anaanza kutoa maamuzi?
Mchukulie Nape. Kwa kauli zile ilimaanisha kuwa jopo lake la washauri hawakufanya kazi yao? Kwa nini ape hakung'oka na watu wake?
 
Kumbuka possibility ya kuwa rais 95% ni lazima atokee kwenye baraza la mawaziri. Ili uweze kuwa rais mzuri ni lazima uwe unaijuwa vzr serikali. Kwahyo kuwa badilisha nikuwafanya wa we na uwelewa mpana katika wizara mbalimbali. Au nyie ofisini kwenu hakuna job rotation?
 
Huwa sielewe kwa kweli. Hasa nikiangazia teuzi za mawaziri. Unakuta leo waziri yupo wizara hii, kesho kateuliwa kule na keshokutwa kaletwa huku. Na kila unapomwona kwenye wizara mpya anaongea kama alikuwa hapo miaka kumi iliyopita.

Kuna wakati Bashungwa alikuwa waziri wa viwanda. Siku alialikwa pale Sheraton kukutana na wadau. Akaweka mikakati yake wee na kuunda timu ya ufuatiliaji na kuahidi kuona matokeo. Baada ya muda kama wiki 4 hivi akatolewa wizara hiyo, sikumbuki alienda wizara gani. Nilitamani sana kujua ni upi mwendelezo wa alichokianzisha. Najua kiliishia njiani tu japo lilikuwa wazo jema sana.

Tatizo ni hilo kila wizara. Yani mawaziri wamefanywa wanasesere. Aliyebaki na heshima wizarani ni Katibu Mkuu tu.

Sasa kilichonifanya kuandika haya ni kwamba natazama tbc hapa namwona Kijaji akitiririka na masuala ya maxingira utadhani alikuwa wizarrani hapo miaka mitano iliyopita. Wiki moja tu nyuma alikuwa waziri wa viwanda na alikuwa akitiririka kama alianzisha wizara. Wiki hiyohiyo Jery Silaa alikuwa wizara ya ardhi na ghafla akapelekwa Mawasiliano. Yani pale alipokuwa anaanza kuchanganya akatolewa. Hadi wananchi wakachukia. Kesho ukimsikiliza Silaa utadhani alikuwa mawasiliano miaka 7 iliyopita.

Tatizo hapa ni mteuzi kutuona wananchi ni maboya sana. Kwamba anaamka tu na pengine kwa maslahi binafsi anatengua uwaziri wa waziri fulani na kuhamisha huku na kule. Ni kama vile Raisi huwa na akilli za watanzania wote. Sasa nimefikiri nikaona yafuatayo;

1. Mteuzi awe na limit ya kuteua na kutengua. Mara mbili tu!

2. Waziri akae wizara husika angalau miaka mitatu bila kusumbuliwa na hamahama

3. Waziri akishindwa kudeliva hakuna haja ya kumhamisha. Ni kutengua tu

4. Waziri akideliva hakuna sababu ya kumhamisha. Ni kuvuruga malengo na kumharibia utendaji

5. Katibu mkuu wizara asitokane na uteuzi bali ushindani na ajira yake itokane na hekima za bodi
Ndiyo zinaongezeka kwani anakuwa anaważa namna ya kujiongeza kwa kuiba hela za Serikali na kujitajirisha yeye na machangudoa wake.
 
Kumbuka possibility ya kuwa rais 95% ni lazima atokee kwenye baraza la mawaziri. Ili uweze kuwa rais mzuri ni lazima uwe unaijuwa vzr serikali. Kwahyo kuwa badilisha nikuwafanya wa we na uwelewa mpana katika wizara mbalimbali. Au nyie ofisini kwenu hakuna job rotation?
Hii ya kina Samia sio rotation ni reshuffle aisee. Rotation ndio hivyo isingepungua miaka mitatu kabla ya kubadilishwa
 
Back
Top Bottom