Hivi mtu akiua mtu aliyemfumania na Mke/Mume sheria inasemje?

Hivi mtu akiua mtu aliyemfumania na Mke/Mume sheria inasemje?

Shamkware

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2013
Posts
1,750
Reaction score
2,283
Mimi nataka kuuliza leo, Haya matukio ya kuuana kwenye mahusiano hasa fumanizi yamekuwa mengi sana siku hizi. Hivi karibuni tu January 04 ya mwaka huu tulisikia jamaa mmoja Huko Chunya Mbeya amemua mtu aliyemfumania na mke wake ndani ya nyumba kwenye chumba anacholala akifanya mapenzi na mke wake.

Nadhani kila mtu anajua maumivu ya kusalitiwa kwa wote mume na mke ikiwa ni kwenye mahusiano au ndoa. Kitendo cha mtu kumkuta anafanya mapenzi na mke wako, ndani kwako, kwenye chumba chako, kwenye kitanda chako ebu imagine ni maumivu makali kiasi gani utakuwa nayo? Na ndipo sasa inatokea hapa mtu anaua bila kukusudia.

Naamini kabisa hapa wengi wanauwa bila kukusudia ni kutokana na stuation anayoipata mtu kwa wakati huo sehemu ya tukio. Ni wachache sana amkute mtu anafanya mapenzi na mkeo/Mumeo amwache tu aondoke bila kashi kashi wala kumgusa mtu huyo aisee.

Na je sheria ya ugoni ikoje hapa mtu ukimpeleka mahakamni ametembea na mkeo na akakana ushaidi huwa unapatikanje? na je ikidhibitika huwa kuna kifungo au faini kwa huyo mtu. Watu wengi wanachukua sheria mkononi pengine sheria ya ugoni haimwajibishi vizuri mtuhumiwa kiasi cha kupunguza maumivu ya mlalamikaji au tatizo nini?.

Pamoja na yote hayo inakuwaje mtu aliyeua katika stuation hiyo ahukumiwe kama muuaji wa kukusudia maana ankuwa amesababishiwa hisira za kuua.

Nawasilisha.

20210111_090840.jpg
 
Ukikutwa na hatia ya mauaji obviously kesi inakua ngumu kwako na uenda hukumu ikakukuta. hakuna Tz inayoamuru raia kuuana.
 
Ukikutwa na hatia ya mauaji obviously kesi inakua ngumu kwako na uenda hukumu ikakukuta. hakuna Tz inayoamuru raia kuuana.
Mbona kuna watu wanaua na wanaachiwa huru huwa wantumia kigezo gani
 
Mbona kuna watu wanaua na wanaachiwa huru huwa wantumia kigezo gani
Kila kitu kinatokea ndo sababu sio wanaohukumiwa wote basi wapo na hatia. kama ushahidi utawaridhisha walio na mamlaka ya kukuhukumu basi utahukumiwa tu. ila ukipesa kesi ya mauaji si kitu rahisi kukikabili
 
Tena ndani ya chumba changu,godoro,kitanda vyote kwa pesa yangu alafu unamkunja style ambazo hata duniani azipo.
Skuachi.
 
Utafungwa maisha, ukituacha sisi uraiani tukila bata la kufa mtu huku wewe ukinyea debe, msosi mbaya ukilala chini na kunywa maji machafu na kuwindwa kutolewa marinda kila siku! Shauri yako..
 
Back
Top Bottom