Kama bwana mdogo amechemka basi wewe utakuwa kuni zinazoungua kumfanya mtoa hoja achemke.
Nadhani ulitakiwa kama unania ya kumkosoa mtoa hoja uwe na strong points za kutetea hoja yako kwa maana uwe CRITIC.Sasa hicho ulichoandika hapo kwenye RED ni vague statements.Inaonyesha jinsi gani unatetea hoja kwa mapenzi binafsi pasipo kudadisi nini kiini cha hoja.
Mtoa hoja ametoa uchambuzi wake usio na evidence na wala chanzo cha utafiti ,pia majibu yake ni Biased.Ila sio ticket ya kupinga 100% alicho ainisha.
Kwa takwimu za Ranking Web of World Universities ambazo zimetolewa 31/7/2011 UDS ni chuo cha 3,438 duniani wakati Mzumbe ni chuo cha 10,107.Tena haitoshi kwa Tanzania Mzumbe katika Rank hiyo Kipo Nyuma ya SUA,Hubert Kariuki,Open University of Tanania.
Ubora wa chuo unapimwa kwa vitu vingi sana ,Machapisho ya Chuo-kutokana na tafiti mbalimbali,Wahitimu wanaomaliza (Competence yao Global),links mbalimbali za chuo,Uwezo wa walimu wa chuo(qualification zao) na staff wengine nk..
Katika vigezo hivyo-sitapenda kukuchosha sana ila hakuna hata kimoja ambacho Mzumbe inaweza ikaizidi UDSM.Ukitetea kuhusu competence ya wahitimu utakuwa unajidanganya kwa kuwa kwa % UDSM itakuwa juu sana kutokana na kuwa inawanahitimu wengi wengi zaidi ya Mzumbe Kuanzia Undergraduate mpaka Postgraduate (Master & PhD) ,hivyo kigezo hicho ukilinganisha kwa % Mzumbe itakuwa imeachwa mbali sana,Pia Mzumbe ni chuo kichanga ukilinganisha na UDSM kwa kigezo hicho.Na hata kwa uhalisia Global wahitimu wa UDSM bado wapo compitance zaidi ya Mzumbe-(Mifano hai ipo ,Dr.Asha Rose Migiro,Prof. Baregu,Prof Lipumba,Prof Pius Yanda,Dr Azaveli Rwaitama n.k-hawa ni baadhi ya watu wanao compete global na ni mazao ya UDSM)
Nimekupa angalizo kuhusu Competence makusudi kwa sababu ndio hoja ambayo wengi wanaitetea wakati si kweli.
Angalau ungekuja na hoja kuwa wanafunzi wanaomaliza MZUMBE-BAF wakienda kufanya mitihani ya ACCA wanahitimu kwa % kubwa kulinganisha na wanafunzi wa B-COM UDSM hapo ungekuwa umejenga hoja kuliko hizo Vegue statement kwenye Red