komasalonde
JF-Expert Member
- Sep 9, 2024
- 1,783
- 2,479
Aliyetengeneza hiyo picha/sanamu hakuakisi au kukariri sura halisi ya JKNB.Ndugu zangu Watanzania,
Mheshimiwa David Kafulila Chuma cha Reli ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa PPP, ametua mbele ya Sanamu ya Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere Katika ubalozi wetu wa Tanzania Nchini India . Ambapo Mzalendo huyu mwenye maadili na aliyenyooka kama rula.
Na ambaye amekuwa akisifiwa sana kwa uchapakazi wake, misimamo ya kizalendo,Maono,Ubunifu katika kazi na upeo wake mkubwa ameweza kufika eneo hilo palipo na sanamu ya Mwalimu Nyerere.
Hii maana yake nini? Hii inamaanisha kutambua mchango mkubwa wa Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Nyerere Mzalendo wa kweli wa Taifa letu katika kulijenga kuwa Nchi na Taifa lenye heshima siyo tu Afrika bali Duniani Kwote. Ni katika kiu ya kutaka kuyaishi maono ya Baba wa Taifa aliyeichukia rushwa, ufisadi, unyonyaji,ubaguzi na vitendo vyote vya maonezi kwa watu hususani wanyonge.
Hii inaonyesha Chuma David Kafulila bado anaisikia Sauti ya Hayati Mwalimu Nyerere ndani yake ikimkumbusha wajibu wake kwa Taifa .na anaona bado ana wajibu na jukumu kubwa sana la kufanya kwa Taifa letu. Hii inaonyesha Chuma David Kafulila akiona Kizazi cha kesho kikimhitaji atimize vyema wajibu wake kwa Tanzania bora.
Ndio sababu mzalendo huyu wa kweli anayekumbukwa na kuacha alama kila alipofanya kazi tangia akiwa Mbunge,RAS Songwe,RC Simiyu na sasa Mkurugenzi PPP amekuwa akifanya kazi kubwa sana na kwa nguvu zake zote kuwatumikia watu,kuleta matokeo Chanya na yenye kuacha alama kama alivyofanya kule Simiyu kwenye zao la Pamba.
Kwake Mheshimiwa Kafulila uongozi ni utumishi kwa watu,kuwapa watu matumaini,kuwatatulia kero,kuwapa majibu,kuwawashia taa,kuwatoa gizani,kuwaonyesha njia,kuwawezesha na kuwasadia.ndio maana amekuwa mtu msikivu na mnyenyekevu sana na asiye na makuu wala kujikweza kwa mtu.View attachment 3109171
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Mwalimu, hayati, Rais Julius Kambarage Nyerere Burrito.