Hivi ndivyo tulivyotapeliwa na Ontario wa TMT kwenye Forex

Hivi ndivyo tulivyotapeliwa na Ontario wa TMT kwenye Forex

Fid Q aliwahi kusema neno lenye utamu siku zote halina ukweli na neno lisilo na utamu ndio lenye ukweli ndani yake. Tuwe makini sana na maneno matamu ya watu wa kariba ya Ontario.

Kwenye ile thread yake ya Namna alivyopiga milion 19 alipata kusema hivi "shika akili zao waachie mioyo yao" ndio kauli mbiu yake guys tuwe makini dogo asishike akili zetu kirahisi.

Kama Juma Nature vile alivyosisitiza kwenye ngoma yake ya mshikemshike ndege tunduni..sisi wajanja tumekimbia...! Ahahaha!
 
Mbona huyu dogo alikuwa pale na watu wazito sana yani kwaiyo max ruge mtahaba na ujanja wake kala za uso Ay kwa kweli Ontario ni mtu hatari
Sifa ya tapeli ni kukupofusha na maneno sukari ili uingie kingi akukamue!

Ila ndio maana hata sijutii kupigwa kama hadi watoto wa mjini akina Ruge, AY wamepigwa Mimi ninaetoka Ikungu lya mbeshi nina ujanja gani zaidi wa kuruka kiunzi cha Ontario?

Thus, shit happen bru!
 
Ulitaka awe anatumia nini mkuu??? Ninavyojua mimi true forex trader ni yule atumiae candlestick,resistance and support, kuchambua soko.....Yaani kuwa pure price action trader.


Nijibu kwanza nilichokuuliza kabla sijaongea ninachotaka kuongea


Ngoja nimsaidie kujibu mkuu wangu...uko sahihi kabisa kusema kuwa true forex trader ni yula anayetumia candlestics, resistance and support kuchambua soko....labda niongeze na chart patterns pamoja na trend..Kama unavojua cardinal rule number 1 ya forex is Trend is your friend Never go against the trend. Sasa mzee baba Cre mara nyingi sana huwa anaenda against the trend na ukimstua ukamwambia mbona labda trend ni down ila yeye anatoa call ya buy huwa anakuwa tu mbishi na kang'ang'ania kuwa endelea kuhold buy trades wakati trend inaruhusu sell.

Kingine sio mzuri sana kwenye kusoma candlesticks na chart patterns kuna vitu huwa analazimisha...kwa mfano anaweza sema kuna double top au double bottom kwenye tf FULANI wakati kimsingi haipo'

Kingine huwa haheshimu support and resistance...kwa mfano mnaweza kuwa mnatrade pair fulani e.g GBPJPY sell labda na mnakuwa mnamake profit kabla haijafika kwenye support anasema tp halafu atamake call nyingine baadaye,,,,hyo baadaye akimake calll anasema buy kwa hyo hyo pair ambayo bado haijafika kwenye support...sasa mkuu hapo ndo kilio kinaanza. Kwa kifupi jamaa bado hajaiva kuwa mentor analazimisha tu.
 
Sifa ya tapeli ni kukupofusha na maneno sukari ili uingie kingi akukamue!

Ila ndio maana hata sijutii kupigwa kama hadi watoto wa mjini akina Ruge, AY wamepigwa Mimi ninaetoka Ikungu lya mbeshi nina ujanja gani zaidi wa kuruka kiunzi cha Ontario?

Thus, shit happen bru!


Mkuu wangu simtetei Ontario ila najua kabisa nafsi yake inaumia sana kwa hiki kilichotokea..Ujanja ujanja kwenye biashara ni kitu cha kawaida sana na hata mm nafanya biashara na natumia ujanja ujanja sana..Sema tu ujanja wenyewe unaotumia usije siku moja wateja wako wakaung'amua maana ndo itakuwa mwisho wa hyo biashara. Alichobugi sana ontario ni kufanya biashara na watu ambao sio sahihi..Kusingekuwa na huku kupoteza hela consintently wala haya malalamiko unayosikia sasa usingeyasikia..Hata wewe usingeleta huu uzi hapa endapo tangia uanze kutrade ungekuwa umepata labda loss mbili tatu. Kilichosababisha haya yote yanaibuka ni loss za kila siku zilizosababishwa na call za Cre ambaye kimsingi hajaiva kuwa Mentor bali analazimisha tu. Kimsingi Ontario kwenye kutafuta mentor hapo ndo alibugi big time.
 
Dahh ila Ontario anajua kuandika bana acha kabisa, anajua kushawishi yaani kipaji chake cha kushawishi akikitumia vizuri kitamfikisha mbali ila sio kwa hapa JF manake pameshachafuka. Nilihamasika kabisa na mimi ningekuwa mmoja wenu sasa hivi. Mungu amenisaidia, nikajisemea moyoni ngoja nisubiri awamu ijayo kumbe Mungu ananiongoza. Asante Mungu [emoji120][emoji120][emoji120][emoji120]
 
Zile call alikuwa anafanya makusudi,BB broker hawezi fanya uhuni wake bila msaada wa mtu wake ataepotosha newbies. Mission accomplished


Mzee baba Singo upooooo...nakumbuka kwenye uzi wa mwanzo wa forex tulikuwa tunaelimishana sana kuhusu hii mambo na kupeana maujuzi kibao kibao...Kwa kifupi sio kuwa Cre alikuwa anafanya makusudi kwa zile call zake ni kwamba jamaa bado ni mchanga sana kwenye forex sema tu analazimisha mambo. Na kwa mwanzoni tulimake hela maana alikuwa naiba analysis za watu anatuletea..alipogundulika akajitoa kwenye hilo group alilokuwa anaiba analysis na kubaki yeye kama yeye....baada ya hapo ndo dhahama la loss likaanza...Cre bado sana mkuu wangu...bado sana yaani.
 
Nimesoma uzi kwa utulivu kabisa na baadhi ya comments za wadau.. naomba nikazie tena kwenye hoja ya mleta Uzi kuwa FOREX SIO UTAPELI ILA BAADHI YA WATU NDO WANAFANYA FOREX IONEKANE NI UTAPELI.

Kimsingi mimi nafanya forex na nilipata training pale pale kwa ONTARIO ila kabla ya training nilishasoma vitabu kibao na hakuna kitu ambacho nilikisikia kwa Rea ambacho kilikuwa kigeni kwangu.

Naomba nimuongelee ontario kidogo..kwa kifupi tu mtu unayejua kusoma mtu ukikutana na ontario kwa mara ya kwanza tu huna hata haja ya mpaka ukae naye uongee nayo utajua tu kuwa ni mtu mwenye dharau. Dharau za ontario kwa mtazamo wangu zinaweza kuchangiwa na vitu kadhaa,,

  • kwanza kabisa kabila lake ni watu wa kujisikia sana (nina mfano wa professor mmoja hv pale chuo kikuu hata chai ya ofisi alikuwa hanywi anakuja na chai yake. na ni mtu wa kujisikia kweli kweli yaani yeye ndo yeye hakuna mwingine)
  • background yake na mafanikio yake kwenye umri mdogo,,,kama mnavojua ontario alishakiri hapa si mara moja wala mbili kuwa katokea kwenye familia maskini kabisa na kapambana sana kufika hapo alipo. Sasa basi kama wengi tujuavyo ukiwa umetokea kwenye familia maskini halafu ukaja kuzishika tena kwenye umri mdogo basi tutakukoma kama we ni limbukeni wa hela. Kwa hyo kinachomsumbua ontario ni background yake na ana ulimbukeni wa hela kiasi kwamba anaona wasio nazo kama mabwege fulani hivi.
  • Ontario amejitahidi kujua mambo mengi sana akiwa bado mdogo kwa jinsi hyo anawaona wale ambao hawajui kama wanaijaza tu dunia bure. Najua amefanya bidiii sana kuyajua ayajuayo ila kisiwe kigezo cha kuwaona wasiojua kuwa hawafai.

Nirudi kwa TMT na biashara ya forex...Kwa kifupi ONTARIO hakujipanga kuanzisha TMT...kimuonekano alijitahidi sana ila je wale aliowalete kutoa training na mentorship ni watu sahihi??? Nikianza na Rea sikuon tatizo lake maana alitahidi sana kumwaga material kadri ajuavyo yeye na kwa kikubwa alitoa basics za forex ilibaki tu mtu mwenyewe kujiongeza kwa kusoma vitabu na kufanya backtesting kwenye demo ila awe nondo zaidi.

Nije kwa Mentor Cre...Mungu wangu yule jamaa ni bure kabisa...yaani kwa kifupi nilianza kumwekea walakini week ya pili tu baada ya kumaliza training na kuanza kutrade live. Kwa kifupi Cre ni mchanga sana kwenye forex yaani jicho lake kwenye charts ni changa mno na kimsingi hajaiva kuwa mentor bado anatakiwa kuwa chini ya mentor na sio yeye kuwa mentor maana bado ni mchanga sana sana sana kwenye kuanalyze charts. Kuna baadhi ya jamaa zangu niliwaleza mwanzo kabisa kuwa Cre bado hajaiva ila wakaona kama najifanya najua sana ila kwa sasa wamekubaliana na mm kuwa kuna vitu niliona kwa Cre ambavyo walikuwa hawajaona. Kwa kifupi Cre sio mentor na asipokubaliana na hali na kukubali kuwa chini ya mentor ili apate ujuzi atawaumiza wengi.

Kuna ishu fulani ilijitokezaga mwezi wa 12 mwaka jana kuwa Cre alikuwa anaiba analysis za BFG wa south na kushare ana Mentees wake ila ile ishu Cre alikana na kusema alishajotoa kwenye group la BFG ila nashawishika 10000000000% kuwa Cre alikuwa anaiba analysis za BFG kwani baada tu ya kusema ameshajitoa kwenye group la BFG ndo alianza kumake call za ajabu ajabu (yaani loss tupu).

Ishu ya Cre kusema kuwa JPmarkets walikuwa wanawa B Book clients wake huo ni uongo wa kiwango cha lami maana mm mara ya mwisho kutrade call za Cre sikuwa na Jpmarkets ila nilipata loss kubwa tu kwa kuitika call yake. Sasa endpo call yake ilikuwa sahihi kwa vile mm nilikuwa na broker mwingine nilitakiwa kupata faidi na wale waliokuwa na JPmarkets ndo wangepata loss maana jpmarkets wanatrade against client wake kama alivosema Cre. Kwa kifupi Cre ni mweupe jamani......Khaaaaaaa....mpaka nakereka.

Nina mengi ya kuandika kuhusu huyu bwana Cre ila ngoja tu mengine niache maana huyu jamaa alishanikera sana sana maana loss nyingi nilizopata nilikuwa nawasiliana naye na kumweleza kabisa kuwa call aliyomake sio ila anakuwa mbishi. Na mm kwa kutojiamini inabidi nikubaliane naye halafu baadae inakuwa maumivu tu.

Ushauri kwa ONTARIO

  • Mkuu najua sana wewe ni mpambanaji sana sana ila kama alivyosema mleta mada tamaa imekuponza sana sana...sitaki kwenda ndani zaidi maana mleta mada ameshasema mengi...Ila ontario acha tamaa mdogo wangu.
  • Umejishushia sana heshima yako ambayo umeijenga kwa muda sana kwa kwanza kuweka tamaa mbele ila kibaya zaidi watu ulioshirikiana nao kwenye kuleta forex tanzania sio watu sahihi maana ungeleta watu sahihi hata huu ujanja ujanja tuliogundua wala tusingegundua endapo mentor angekuwa sahihi na watu wanaona faida kwa kutrade forex. Sisemi kuwa hakuna loss kwenye forex trading ila hizi loss za Cre zimezidi mkuu wangu. Kwa kifupi jamaa ni mweupe sana sana sana.
  • Kama una mpango wa kuendelea kutoa training ya forex trading na mentorship..Nakushauri achana na Cre tafuta mentors wengine...South kuna mentro kibao ambao wanaweza kurudisha hesima yako kwa mwezi mmoja tu. Watanzania sisi ni watu wa kusahau mapema ukituletea mentor mzuri tukapiga hela mwezi mmoja tu mbona haya yote tuliyopitia tunayasahau faster tu.

Namalizia kwa kuseme Ontario Cre sio professional trader na hatakaa awe. yule anatakiwa tu awe chini ya mentor baaasi na sio yeye kuwa mentor.
Umeandika kwa uchungu sana toka moyoni..... huyu Ontario kipaji chake n kuandika tu story.. ila sio professional trader... hata zile story humu JF za yeye kupiga PESA nying through FOREX n za kutunga tu.
 
Mkuu wangu simtetei Ontario ila najua kabisa nafsi yake inaumia sana kwa hiki kilichotokea..Ujanja ujanja kwenye biashara ni kitu cha kawaida sana na hata mm nafanya biashara na natumia ujanja ujanja sana..Sema tu ujanja wenyewe unaotumia usije siku moja wateja wako wakaung'amua maana ndo itakuwa mwisho wa hyo biashara. Alichobugi sana ontario ni kufanya biashara na watu ambao sio sahihi..Kusingekuwa na huku kupoteza hela consintently wala haya malalamiko unayosikia sasa usingeyasikia..Hata wewe usingeleta huu uzi hapa endapo tangia uanze kutrade ungekuwa umepata labda loss mbili tatu. Kilichosababisha haya yote yanaibuka ni loss za kila siku zilizosababishwa na call za Cre ambaye kimsingi hajaiva kuwa Mentor bali analazimisha tu. Kimsingi Ontario kwenye kutafuta mentor hapo ndo alibugi big time.
Chief wewe unadhan Ontario alikuwa hajui janja janja ya cre... alikuwa najua kila kitu... anajua cre n mweupe hajui kitu.. kimsingi Ontario alidhamiria kbsaaa kupiga watu PESA... ujanja ujanja mwingi kumbe mpigaji tu....
 
Chief wewe unadhan Ontario alikuwa hajui janja janja ya cre... alikuwa najua kila kitu... anajua cre n mweupe hajui kitu.. kimsingi Ontario alidhamiria kbsaaa kupiga watu PESA... ujanja ujanja mwingi kumbe mpigaji tu....
Yeye mwenyewe Ontario alikuwa hatumii call za Cre iweje sisi hatuache tutumie call za cre kwa zaidi ya miezi 6?

Scammer murfaka!
 
Chief wewe unadhan Ontario alikuwa hajui janja janja ya cre... alikuwa najua kila kitu... anajua cre n mweupe hajui kitu.. kimsingi Ontario alidhamiria kbsaaa kupiga watu PESA... ujanja ujanja mwingi kumbe mpigaji tu....


Sina uhakika sana na hilo ila huwa najua kumsoma sana mtu na kimsingi simuoni ontario kama tapeli ila namuona kama kijana ambaye ni very ambitious yaani anataka kuwa mtu fulani hapa tanzania. Na kama lengo lake ni kuwa mtu fulani sidhani kama anaweza kukubali kuonekana tapeli waziwazi maana ndoto yake ya kuwa mtu fulani itayeyuka. Kimsingi namuona kama mtu anayetaka kuachieve a lot ila sio tapeli wala mpigaji. Namuona kama mtafutaji na katika utafutaji ujanja ujanja ni sehemu yake. Ile ishu ya kuongeza spread na kulazimisha watu watrade na jpmarkets ili wawe IB hyo ndo sehemu ya ujanja ujanja kwenye biashara ila ili la kusema kuwa call za Cre za loss zilikuwa za makusudi ili wakagawane pesa na broker traders wanapopoteza hela hilo sidhani kama ni kweli (Siwezi kuapa ila intuition yangu hainitumi hvyo).

Ishu hapa ni kwamba Cre ni mweupe na ndo maana baada ya kuona maji yamefika shingoni anaanza kutaka kuwashawishi watu kuwa broker ndo anawa B book ila kimsingi tatizo ni Cre...Hzo allegations za B Booking amezileta tu ila kujinasua kwenye lawama ila tatizo ni yeye na weupe wake.
 
Nikipata time ntaanzisha uzi...... huyu Dogo Ontario arudishe PESA za watu..... FOREX is real sema ni kama sports betting tu... utofauti wake FOREX n kusoma soma ma vitabu.... but n same na betting.. huwez tajirika through FOREX....

Ukiachana na utapel watu kama akina Ontario.. behind FOREX kuna kitu kikubwa sana ambacho watu hawakijui thus why wanapoteza.... FOREX ingekuwa kama Ontario na watu wengine wanavyoaminisha hakuna mtu angekuwa masikini.. watu wote tungekuwa matajiri.....

Kuliko mtu afanye FOREX bora afanye sports betting TU....
Frankly speaking kama ulisoma vitabu na ukatrade hata kwa demo na bado unaona forex ni kama sport betting basi hakika hukuelewa wakati unasoma
 
Pole sana kiongozi take time jifunze mwenyewe taratibu utaweza kutrade very successful Tafuta kitabu kinaitwa intelligence investor I think nikizuri kuliko maelekezo ya hao wapigaji
 
Frankly speaking kama ulisoma vitabu na ukatrade hata kwa demo na bado unaona forex ni kama sport betting basi hakika hukuelewa wakati unasoma
Subir uzi utakuja.... "kilicho jificha nyuma ya FOREX" .. kila kitu ntaweka hapa... narudia tena usitegemee retailer kama wewe FOREX itakutoa never never........
 
Frankly speaking kama ulisoma vitabu na ukatrade hata kwa demo na bado unaona forex ni kama sport betting basi hakika hukuelewa wakati unasoma


Forex ni kama sport betting????....huyu le professeri vipii...hv kwenye spot betting unaweza tumia stop loss....hv kwenye sport betting unaweza take partial profit???yaani kwa mfano labda umebet match kati ya ManU Vs Mancity kuwa ManU watashinda na akishida labda utapata 100,000 ikafika half time ManU akawa kashampiga Mancity 1:0...hv unaweza kwenda kwa muhindi ukamwambia kuwa akupe 50,000 yako kuwa hutaki kuendelea mpaka mwisho wa match???

Kwenye forex unaweza take partial profit yaani kama lengo lako labda kwenye hyo trade ulikuwa unataka utengeneze pips 50 zinaweza fika pips 20 na ukaona kama kuna kitu kinataka kwenda kinyume na wewe ukaamua kuchukua profit ya zile pips 20 na kukaa pembeni. Sasa hapa sijui mtu analinganishaje forex na sport betting.
 
Sina uhakika sana na hilo ila huwa najua kumsoma sana mtu na kimsingi simuoni ontario kama tapeli ila namuona kama kijana ambaye ni very ambitious yaani anataka kuwa mtu fulani hapa tanzania. Na kama lengo lake ni kuwa mtu fulani sidhani kama anaweza kukubali kuonekana tapeli waziwazi maana ndoto yake ya kuwa mtu fulani itayeyuka. Kimsingi namuona kama mtu anayetaka kuachieve a lot ila sio tapeli wala mpigaji. Namuona kama mtafutaji na katika utafutaji ujanja ujanja ni sehemu yake. Ile ishu ya kuongeza spread na kulazimisha watu watrade na jpmarkets ili wawe IB hyo ndo sehemu ya ujanja ujanja kwenye biashara ila ili la kusema kuwa call za Cre za loss zilikuwa za makusudi ili wakagawane pesa na broker traders wanapopoteza hela hilo sidhani kama ni kweli (Siwezi kuapa ila intuition yangu hainitumi hvyo).

Ishu hapa ni kwamba Cre ni mweupe na ndo maana baada ya kuona maji yamefika shingoni anaanza kutaka kuwashawishi watu kuwa broker ndo anawa B book ila kimsingi tatizo ni Cre...Hzo allegations za B Booking amezileta tu ila kujinasua kwenye lawama ila tatizo ni yeye na weupe wake.
Sema chief unakosea one thing kumtetea Ontario.. na kumponda cre while wote wapo kwenye boat moja ya kuwapiga PESA watanzania masikin wenye kutegemea mlo mmoja kuishi.. imagine nasikia kuna mtu aliweka kiiinua mgongo chake kwa call za cre na kimekwenda wengine waliuza mpk viwanja, mashamba wapate mtaji.. vyote wahuni.. matapel hawa wamebebaa
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] uwiii nimecheka aisee poleni kwa kupigwa hakuna utajiri wa hivyo, mjifunze siku nyingine.
Labda tu niwaambie kitu. Huyo jamaa kaharibu brand name yake kwa kujifanya IB but kafungua sana watu. kwa sasa watu wanatrade forex like no other, na watu wamejiunga mafunzo ya online kutoka south africa, USA, etc. Wanazidi kuingia kila siku, and amini usiamini miaka 2, 3 ijayo college dropout zitakuwa nyingi na zitakuwa zinaongezeka.
Unasema hakuna utajiri wa hivyo, kwa fikra zako upo sahihi, lakini kwangu mimi kama watu walioanza December sasa wameanza kutengeneza atleast dollar 300 kwa siku consistently things are not bad.
 
Sema chief unakosea one thing kumtetea Ontario.. na kumponda cre while wote wapo kwenye boat moja ya kuwapiga PESA watanzania masikin wenye kutegemea mlo mmoja kuishi.. imagine nasikia kuna mtu aliweka kiiinua mgongo chake kwa call za cre na kimekwenda wengine waliuza mpk viwanja, mashamba wapate mtaji.. vyote wahuni.. matapel hawa wamebebaa


Sijamtetea mkuu wangu ila nina taarifa za ndani kuwa Ontario waliwakiana sana na Cre kuhusu call zake zinazofanya watu wapoteze hela....ila nimesema siwezi kumwapia Ontario kuwa si sehemu ya watu kupoteza hela (yeye ndo anajua na Mungu wake na kama alileta hii kitu ili akawatapeli watu basi itamrudi big time maana kweli watu wamepoteza hela walizozipata kwa jasho sana sana sana na hilo haliwezi kwenda hv hv). Na kimsingi hzo allegations za jpmarkerts kuwa B book client wake sidhani kama zina ukweli maana endapo client watagundua kuwa broker anawa B book watamkimbia huyo broker na ndo utakuwa mwisho wake maana broker faida yake ipo kwenye spread, Swap na commission kama anacharge maana kuna broker wengine hawacharge commission.
 
Back
Top Bottom