Hivi ndivyo tunavocheat, palipo na viatu vya muwewe kuna ndala zangu

Hivi ndivyo tunavocheat, palipo na viatu vya muwewe kuna ndala zangu

Salaam wadau,


Maisha yanatupa zoefu nyingi sana, zenye matokeo chanya na wakati mwingine zinaweza kukuachia alama ya uchungu isiyosahaulika. Mara nyingi sio kwa kupenda au kuridhia maisha automatically yanakupa darasa. Hiki ni kisa Cha ukweli.

Nitajaribu kuweka wazi mambo magumu ili upate picha japo kwa kusoma. Nikusihi tu soma na chukua machache kwajili ya kuboresha mahusiano Yako. Wala usinijaji kwa yaliotokea maana huko nilishatoka 6 years back na sijutii. Toba ilishamaliza kila kitu. Twende kazi.

Miezi miwili tu baada ya kumaliza elimu ya juu nipo home mark timing ndio nakutana na aliyefanya niandike huu Uzi. Tulikutana dukani mtaa Mmoja, wakati Mimi nafika yeye alikua akisubiri chenji/chenchi yake. Muuzaji alitoka kidogo ikabidi nimuulize yeye sasa. "Habari Yako, huyu yupo wapi ?". Akanijibu. " ametoka kidogo kufata chenchi anarudi sasahivi". Hili duka lilikua ndani ya mji wa mtu, unaelewa sikuhizi unajenga nyumba Yako na frame kadhaa mbele yake. Ndivo ilivokua.

Mimi sikuona Haya kuanzisha stori nae ili kubuy time. Mimi " sorry wewe ni mwenyeji huu mtaa ?" Huyu dada naomba tumuite Recho. Akanijibu "Ndio mi nikaa hapo tu jirani, na wewe ?". Mimi "Me pia nyumba ya tatu kutoka hapa". Recho " ooh! Kumbe tupo jirani... sasa mbona Mimi sijawahi kukuona na kwangu we ni mgeni kabisa". Nikamjibu Hilo swali kuwa na Mimi nilitaka nimuulize nivile tu kaniwai. Huku ukweli nikwamba ni kweli sio mkaaji sababu ya shule. Basi muuzaji alirudi na akampa chenchi yule dada akarudia nyuma kunipa nafasi nihudumiwe lakini hakuondoka nikama alikua akisoma sms kwenye simu yake.


Wadau mwanamke udhaifu wake upo masikioni. Maana yake ni unaweza athiri namna yake ya kufikiri kwa kupenyeza maneno matamu kwenye sikio lake. Lakini kwetu wanaume Macho ndio weakpoint. Kutaamani kunaanzia kwenye kuona. Binafsi nilimtamani yule dada. Why ? alikua amevaa tight ndefu ya grey, t-shirt ambayo kwake ni oversize chini kabisa kaua na kikuku Cha chain mguu mmoja. Shape na muonekano mzima of course alinivutia japo sijamuelezea kwa 100% maana sio dhima yangu ya msingi ingawa kama ungeiona picha yake insta naamini ungegusa kwenye kuview profile.

Bila kujua au kujali sikumpa tena attention kwani niliamini anaondoka lakini nilishangazwa na kitu. Nilisikia... " jirani me naondoka", nikama 30sec zilikatika toka anipishe nipate hudumu. Nikageuka chap naona ni kweli anashuka ngazi. Nikamwambia " sawa jirani tutaonana tena". Nilichonotice ni kama Recho alitarajia ninge endeleza maongezi sorts of maswali na hatimaye tubadilishane namba. Ukweli ni alikua sahihi lakini nilikaza tu maksudi maana niliamini kama ni jirani kweli na anakaa pale aliponionesha kwa kidole basi tungekutana mara nyingi zaidi maana nipo home sasa.

Kimsingi nilikua nimefunga zipu yangu kwa miezi kama mitatu hivi au ziaid hivyo nilikua hyper flani hivi. Hapa niweke kitu clear. Notion iliojengeka kichwani mwangu ni, mwanamke ambaye Anableach...anavaa vikuku...anatattoo. Iwe ni ana kimoja kati ya hivyo au vyote kwa pamoja ni Wanawake ambao wapo beyond the limits. Yaani kama kaolewa au anamtu kucheat sio issue na mambo ya bata hasa sex ndio issue zinawapa fantasy sana. Na hio Haina uhusiano na elimu yake . Super woman chukua hioo itakuaaidia. So niliamini tu hapa nitapiga hata iweje. Niliweka nia lazima nitamtafuta tu.

Kesho yake mida ya saa 5 asubuhi nilipita jirani kabisa na Ile nyumba na ilikuwa na fence. Kichwani nikawaza nigonge geti au nikaushe naona shetani akawini. Nikagonga geti, baada ya muda kidogo likafunguliwa. Aisee ni yeye Recho kafungua. " Jamani jirani umepajuaje hapa. Heeh! Karibu kumbe kweli wewe ni mwenyeji". Mimi " Jana baada ya kunionesha tayari nikajua ni nyumba gani haswaa" mara kidogo nyuma yake akafata mtoto mdogo wa kiume kama miake 4+. Sikuuliza lakini alinambia "Oh! Mwanangu huyu jirani, haya karibu basi ndani."

Kaka mkubwa niliingia Ndani, Moja kati ya very high risks nimewahi kufanya ni hii. Kuingia ndani ya mji wa mtu pasina kujua kaolewa au lah na kama kaolewa mwenye mke yupo ndani, katoka au utarudi muda gani... Leo tuishie hapa then kesho tujue yalionikuta, inshallah tunaendelea.
Kumbe ni siriz, naona upo field kwa shigongo
 
Watu wa aina hii ni kupiga hata Risasi ya matako yaaani umekula mke wa mtu alafu unakuja kujisifia humu hujui jamaa akijua hata kama miaka imepita mingi lazima akufanyie ubaya ubwela Shauri yako
Hili ni onyo usiendelee kuleta huu upuuzi hapa la sivyo usije jutia
 
Salaam wadau,

Tuendelee EPISODE 10C


Niliacha wiki ikate kisha nimtafute Recho kwa namna nyingine ingawa mara moja moja nilikua najaribu kupiga na majibu yalikua ni yaleyale 'blocked'. Hio haikuishia hapo tu nilipigwa tofali mpaka WhatsApp. Rasmi sioni tena status za Recho, meseji zipo 'single tick' na status zangu hazioni tena.


Baada ya wiki kukata niliona sina sababu tena ya kulazimisha mapenzi. Nilighaili kumtafuta tena Recho na kukubali maisha mapya. Hii haimaanishi sikuwa na mbinu mbadala, lah hasha. Kwa akili zangu nilikuwa na namna kibao za kumpata tena hewani lakini niliona haina maana kwani akishajua ni mimi haitabadilisha chochote.


Siku moja nikiwa nimepost status yangu WhatsApp ambayo sasa ni kila mtu anaona, miongoni mwa walio 'view' ni pamoja na Recho. Sikuamini hii kitu, ikabidi nimpigie. Simu kweli ikapokelewa, Mimi "Hello", akaitika " yes Z... mambo". Mimi " Dah! Siamini kama ni wewe umepokea simu yangu". Recho kwa sauti ya kawaida kabisa asiyo na shaka " Ni Mimi...kwani nimekuuliza we nani...najua naongea na Z". Mimi " Aisee, ok upo free tuongee". Recho we ongea tu nakusililiza".


Majibu ya Recho pamoja na 'tone' aliyokua akitumia ilinishangaza kidogo. Kwanini?. Kwasababu ni muda kidogo umepita zaidi ya mwezi mwezi na nusu toka ani 'block', ajabu ni alizungumza kama vile tunaongea kila siku.


Swali langu kwa Recho, " umeamua tuachane bila taarifa?". Recho " kwanini... mbona simu yako nimepokea!!". Mimi " nimeshangaa umeview status...ok kwanini ulinibock na ukapotea mazima". Recho "Nisikilize Z, Hapa katikati nimepitia mambo mambo... hivi tunavyoongea mume wangu kahamishwa kituo na sasa tupo tupo mkoa X".


Nikamdaka " Hivi kwa ukaribu tuliokuwa nao mbona hilo halizuii mawasiliano". Baada ya hilo swali kimya kidogo kikapita kisha, Recho " nisikilize Z, mume wangu alijua kuwa ninatoka nje na ndio kipindi hicho anapata uhamisho". Akaendelea " mambo mengi yalifata baada ya hapo mpaka tunaamia hapa ndio maana nikaamua nikuweke kando ili kurejesha amani ya ndoa yangu".


Mimi " Ni sawa Recho una hoja ila kwanini usingeniambia nijue kinachoendelea badala yake unaniblock". Recho "niliona ndio njia pekee ya kukaa mbali na wewe ili ni 'concentrate' na familia yangu".


Nikashusha pumzi. Kwa yale majibu yake Recho niliona kabisa kwake thamani yangu haipo tena, huyu ameshaamua lake. Nilitaka kufupisha mjadala nikate simu lakini Recho alikataa huku akiniregezea sauti. Ile niliyoizoea mwizi mimi.


Recho " Z nisikilize, ukiachilia mbali sasa nipo mkoa mwingine lakini ninajoina mbinafsi sana... sasa hivi unakazi, inatakiwa upate mwanamke mpambane mjenge maisha. Nikiendelea kukushikilia hutakuwa na familia". Hapa Recho aliongea kitu kikapenya flani hivi japo siku onesha kukubali Ile hoja


Mimi "Ooh! sasa ninakuelewa... kumbe tayari umeniacha ". Recho " hapana Z usichukulie hasira. Hujui nimemtumia nguvu kiasi gani kukubali nikuache uendelee na maisha yako. Hata Ile siku umepiga simu niliona nikublock tu maana nikiruhusu kukuwaza naumia".


Mimi "Recho ninayo mengi ya kusema juu ya jinsi nimeteseka na nateseka kwajili yako lakini haina maana tena kukwambia". Nikaendelea "Kumbe ulijiandaa kuniacha, poa". Palepale nikabadili mada kwani niliona nikama napata hasira na hisia za unyonge tena wa mapenzi.


Hatukuongea sana hata baada ya kubadili mada nikakata simu. Mpenzi msomaji, kwa sauti Ile ya mwanzo Recho alionekana ukurasa wa mapenzi na Z alishaufunga kilichobaki ilikua ni kunipa taarifa tu.


Mpaka wakati huo 'contact name' ya Recho katika simu yangu ilikua ni 'Amore' nikimaanisha mpenzi baada ya kunitoa ujinga kichwani nilibadili chap na kumsave kwa jina lake la NIDA.


Taarifa rasmi ya kuachwa maana kule sio kuachana haikuniumiza kwa level hio kwani nilisha iandaa saikolojia yangu toka awali. Sikuwahi kufuta ujumbe hata mmoja kutoka kwa Recho tangu nimeflash siku ya kwanza niliyoomba namba mpaka hio siku napewa rasmi taarifa.


Nilifuta Ile chat, kuhusu kufuta namba niliona haina maana kwani mbali na mapenzi huenda kuna siku atanifaa kwa ushauri wa kimaisha.


Recho yupo na familia yake mpaka leo. Z nipo na familia yangu mpaka leo. Hatuna mawasiliano sana lakini mara chache sana tunawasiliana na kushauri pale panauhitaji. Sina baya naye kabisa.


Katika simulizi hii nilijaribu kuongea na kila kundi katika jamii kwa kutoa vipande vya ushauri ndani ya kisa. Vijana na wanawake niliwapendelea zaidi lakini kwa heshima na upendo nitatoa bonus Episode kufungua code fulani kwa wanaume walio ndani na hata Nje ya Ndoa.

Nimewaona kina Recho kadhaa kwenye comments na Z kama wawili lakini huu Uzi utawafaa wote. Nashukuru sana, Ahsanteni.
 
Watu wa aina hii ni kupiga hata Risasi ya matako yaaani umekula mke wa mtu alafu unakuja kujisifia humu hujui jamaa akijua hata kama miaka imepita mingi lazima akufanyie ubaya ubwela Shauri yako
Hili ni onyo usiendelee kuleta huu upuuzi hapa la sivyo usije jutia
Karibu sana mkuu. wegero kwetu
Wapo moderators na content quality editors. Wape nafasi kaka.
 
Back
Top Bottom