Hivi Ndivyo Unavyoweza Kutajirika Kwa Kuanza Na Shilingi Elfu Moja


Mimi nimewekeza kwenye mfuko mmoja wapo pale UTT unaitwa mfuko wa jikimu ambao napata gawio kila robo mwaka lakini gawio hilo silichukui linaendelea kununua vipande.

sasa ninachouliza hii UMOJA FUND na JIKIMU FUND ipi nzuri kuwekeza?

maana nilimsikia mfanyakazi mmoja wa UTT akielezea kuhusu UMOJA FUND unawanufaisha watu kwa 75% kwa fedha uliyo iwekeza tangu ianzishwe mpaka sasa. Lkn mimi nikiangalia fedha yangu niliyoiwekeza kwenye JIKIMU FUND haija panda thamani kiasi hicho.

Sasa je ni bora nianzishe nguvu nyingine kwenye umoja fund ndo unalipa au niendelee kuongeza kwenye Jikimu Fund?

ushauri wako mkuu.
 

Hayo masaa mbona ujaweka na kuwa kwenye foleni na kusubiria usafiri hasa kwa walio mijini.
 

Sina hakika sana kuhusu JIKIMU FUND ila najua hiyo unaweka kiasi fulani halafu unakuwa unapewa gawio.
UMOJA FUND hakuna gawio bali vipande ndio vinakua thamani na mara nyingine vinakua sana hivyo watu kufaidiaka sana.
Nenda kwenye ofisi zao wakuelezee, ila kwa upande wangu naona UMOJA is the best.
 
Hayo masaa mbona ujaweka na kuwa kwenye foleni na kusubiria usafiri hasa kwa walio mijini.

Sasa huo ndio wakati mzuri sana wa kusoma au kusikiliza vitabu vilivyosomwa(audio books).
Kama upo kwenye foleni ndani ya gari lako unaweka audio cd na kusikiliza.
Kama upo kwenye daladala hata kama umesimama unaweka earphone zako na kusikiliza audio books ambazo unakuwa umeweka kwenye simu yako.
Ukiwa umekaa kwenye foleni nyingine na kusubiri huduma, kama kwenye ofisi au bank unatoa kitabu chako iunaendelea kusoma.
Mimi muda mwingi ninaopata wa kusoma ni wa aina hii popote nilipo nakuwa na audio books na pia nakuwa na kitabu. Nikipata dakika kumi nasoma.
Kujua zaidi jinsi unavyoweza kuitumia foleni kwa manufaa fungua link hii http://www.amkamtanzania.com/2013/11/hivi-ndivyo-ninavyoifurahia-foleni.html
 

Mkuu kuweka elfu moja siyo tatizo, ila kusoma vitabu mia 3, kwa miaka mitatu hii kwangu ni tatizo na ninakuona kama muongo labda kama vitabu vyenyewe vina page 10-20,

Je member anaweza kukopa kwa dhamana ya mchango wake anaojiwekea?au itabidi asubiri miaka 5 ndio aonje utamu wa mfuko?
 

Hakuna kisichowezekana, na tafadhali usiniite muongo. Kama hujawahi kuona ikifanyika haimaanishi haiwezi kufanyika.
Ndio unaweza kutumia vipande vyako kama dhamana ya kupata mkopo. Nenda ofisi zao watakupa maelezo mazuri.
Narudia tena watanzania wenzangu tuwe TUNAJIONGEZA, nilichoandika mimi sio sheria, kwa mfano hiyo miaka nimeandika kama ushauri wangu. Unaweza kuwekeza miaka miwili ukaona umepata kiasi cha kutosha ukafanya mengine. Unaweza kuwekeza miezi sita, ukaona imekutosha ukafanya mengine, maamuzi ni yako. Mimi nilikuwa nakuonesha faida ya kuweka kwa muda mrefu.
 

Mkuu nimekuita muongo kwa sababu mimi ni msomaji mzuri sana wa vitabu na pia kulingana na kazi yangu ya masaa 8 kwa Siku, muda wa kukaa na familia, muda wa kujipumzisha akili na shughuli za kijamii nasema ni vigumu kusoma vitabu 2 ndani ya wiki na kufanya discussions hata ukiwa jobless na hata ukiwa na uwezo huo hiyo hali haiwezi kuwa consistent na utakuwa huwezi kupata chochote kutoka kwenue hivyo vitabu labda kama unasoma majarida.

Na hata kukumbuka vitabu ulivyosoma na ulichokipata kutoka kwenye hicho kitabu itakuwa ngumu sana. Ila kama umeweza kusoma vitabu 300 ndani ya miaka 3, inamaana ndani ya wiki umesoma vitabu 2 nakuita wewe nI EXCEPTIONAL
 

Ndio maana nasema kama wewe huwezi usiseme haiwezekani. Mimi nimeshasoma vitabu vingi sana na kwa muda mfupi sana.
Ukijipanga vizuri unapata masaa mawili kwa siku, na wikiend unaweza kupata hata masaa matatubau manne. Kwa hiyo minimum unaweza kupata masaa 16 kwa wiki, je vitabu viwili haviishi?
Anza hivi, wahi kuamka saa moja kabla ya muda wako wa kawaida wa kuamka na tumia muda huo kusoma(hii inamaanisha uwahi kulala pia). Tembea na kitabu popote ulipo, ukiwa kwenye foleni soma, ukiwa umasubiri mtu au kitu soma.
Acha kuangalia tamthilia au movie, ni kupoteza muda, acha kupoteza muda mwingi kwenye mitandao ya kijamii. Na pia punguza muda unaokaa kupiga story zisizo na msaada kwako.
Fanya hivyo uone kama vitabu viwili havitaisha.
Tatizo letu watanzania tunataka mabadiliko yatokee bila ya sisi wenyewe kubadilika. Unahitaji kubadilika kwanza na kiubadili maisha yako ndio uweze kufanya mambo hayo.
 
Hapana miaka 30 ni mingi mno. Ungetuambia maswala ya kuweka akiba tu na kuwekeza kwenye mambo mengine kama ufugaji, ukulima na biashara ndogo ndogo..

hiki ndyo watanzania mnachotaka mnapenda sana kazi za kutoka jasho,na kuumia sana mkipewa option ya kutengeneza kipato kwa njia rahisi mnaona mnatapeliwa.....
 
Biashara matangazo.... Labda iwe kwa dola ila syo sh. Ya Tz.. Tuheshimiane. Hapo watakaonufaika ni UTT... wao wanawiri mimi niendelee kuwa maskin kusubiri miaka 60,
 


Nimeanza kusoma, nilipofika hapo kwenye red nikaacha. Umejifunza wapi Math?
 
Nimeanza kusoma, nilipofika hapo kwenye red nikaacha. Umejifunza wapi Math?

Haihitaji kujua hesabu, tumia fomula niliyoweka hapo kwenye link. Halafu kuna vingi vya kujifunza hapa zaidi ya hiyo hesabu moja.
 
........ .. kipato chako chenyewe ni 1000 kwa siku, then ukaiweke 1000 hiyo hiyo katika mfuko wa akiba .. pia kila siku utahitaji si chini ya 1500 kama gharama za usafiri kupeleka hiyo pesa kwenye huo mfuko, pia utahitaji zaidi ya masaa matatu hadi manne kwa siku ili kuifikisha hiyo 1000 panapohusika.. inamaana katika masaa 10 ambayo ulikuwa unaitafuta 1000 utabakiwa na masaa 6 tu ya kutafuta 2500.. teh tehh... okay hesabu rahisi katika miaka mitano utakuwa na mil 1,800,000 safi sana hapo panafurahisha na kuona mafanikio.. haya sasa twende katika garama za kuifikisha hiyo 1000 pale panapo husika ni sh 2,700,000.. maajabu ya musa hayo sasa unatumia 2,700,000 ili kutunza 1,800,000. huu ni uchizi aisee
 

Mkuu unaweza kuyapanga mawazo yako vizuri ili tuweze kukuelewa na kukusaidia inapobidi?
Maana nimejitahidi kukuelewa nimeshindwa.
Ila kidogo ninachoweza kukuambia kwa maelezo hayo no hivi; kama unapata hiyo elfu moja kwa siku utaendelea kupata hiyo mpaka lini? Na je unafikiri kuna maajabu gani yatatokea kukutoa hapo ulipo?
Hii ndio inatakiwa iwe changamoto ya wewe kukuza kipato chako na sio kutumia kama sababu ya kiuendelea kuwa makini.
Karibu sana.
 
nadhani hapo wazo liwe kuweka hiyo 1000 kwa ajili ya malengo ya baadae kwa familia... ila sio wewe kujikwamua kwa umasikini. nilichokuelewa hapo ni kwamba niweke akiba kwa miaka 60 wakati hata life span ya mtanzania haifiki miaka 50
 
Wazo zuri lakn watanzania wengi wanaishi chini ya dola moja yaani namaanisha pato langu ni 1500 hii natakiwa nitumie matumizi yangu yote unafikir mtu wa aina yangu atasave chochote
 
nadhani hapo wazo liwe kuweka hiyo 1000 kwa ajili ya malengo ya baadae kwa familia... ila sio wewe kujikwamua kwa umasikini. nilichokuelewa hapo ni kwamba niweke akiba kwa miaka 60 wakati hata life span ya mtanzania haifiki miaka 50

Nani kakuambia miaka 60! Nimeweka miaka mitano hapo ina maana hukuiona?
Ondoa mtizamo hasi ulionao mkuu, weka elfu moja kwa miaka mitano ijayo ufanye kitu cha kukukomboa.
Ukiendelea kutafuta sababu za kwa nini usiweke hiyo buku utazipata nyingi sana. Na hakuna mtu atakuja kukutoa hapo ulipo.
Chukua hatua sasa.
 
Hiyo buku kuiweka au kuizungusha upate faida lipi jema?
 
Hiyo buku kuiweka au kuizungusha upate faida lipi jema?

Mkuu unaweza kuisoma vizuri hii makala na kuielewa ndio uweke post? Maana hakuna sehemu niliyosema uweke buku akiba nimekuambia uiwekeze hiyo buku sehemu inayokua.
Halafu hebu niambie unawezaje kuizungusha buku ukapata faida?
 
Nduhu uliyeanzisha hii tread umeongea vitu vya kweli kabisa na nina kuunga mkono asilimia 100.

Tatizo la watanzania ni la muda mrefu sana, tangia utoto hatijapata elimu za muhimu kwa mfano kuhusu mambo ya pesa au kujisomea.

Mimi binafsi nimejifunza mambo mengi yaliyonibadilisha kutokana na kusoma, Bill Gates mwenyewe anasoma kitabu kimoja kila wiki, jiulize mpaka leo amesoma vitabu vingapi?

Naamini kabisa kuwa kipato chako kinaweza kulingana na mambo uliyojifunza kwenye maisha. Yaani kichwani una nini? Ndio maana yake hiyo. Wanaojua vitu vingi wanapata hela nyingi. Period.

Watanzania wengi wameshakubaliana na hali walizonazo, wana taka slope tu. Kujitaabisha wala!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…