Hivi Ndivyo Unavyoweza Kutajirika Kwa Kuanza Na Shilingi Elfu Moja

Hivi Ndivyo Unavyoweza Kutajirika Kwa Kuanza Na Shilingi Elfu Moja

Mkuu wala huhitaji kujitetea sana. Kikubwa umeeleza vizuri sana. Bila shaka walionza kipindi unatoa huu uzi walishafika mbali sana. Nikiwemo mm.
 
Hio hesabu n kwa waajiriwa wasiokuwa na idea ya kibiashara...
 
Kwa maana nyingine haumshauri mtu kuhusu uwekezaji, mm kwa kuongezeka juu ya ushauri wako mzuri, hizo hela ulizopata kwa mwezi tafuta sehemu zifanye kazi nazo pia zikuingizie 1000 kila siku au hata 500 na sio kumshauri mtu akaiweke hela iwafaidishe hao Company. Huwezi kupata hela ukapeleka bank, ikafanye nini na kwanini kwanza, Eti unataka utajiri, utajiri ni uwekezaji na sio kuweka pesa kiasi hiko.

NB: ushauri wako wauchukue lakini wasikubali kupeleka hela wanayoipata kwenye taasisi hiyo au hata bank mimi siwashauri, hakuna tajiri au mtu atakaye pata utajiri kwa utaratibu huo, haya kwa mfano hiyo hela unayoiweka mda huo, baadae unafanyia nini kama sio kubweteka kama mwanzo tu. USHAURI WANGU WEKEZA USIWEKE HELA BANK, hapo utapata mala 100 ya hela hiyo

VUTA PICHA
Kama una mtaji ambao utakuingizia 1000 kila siku, kwa wastani itakuwa biashara ya mtaji wa 50,000, ambayo kwa mwezi unapata 30,000 baada ya miezi 2 ukiwa unaweka hiyo buku una 60,000 ambayo tayari imezidi mtaji uliozizalisha hizo 60,000, kwa hapo ukianzisha biashara nyingine kwa siku unaanza kuweka 2000 na sio 1000 kama mwanzo, na kwa mwezi unakuwa na 60,000 na yenyewe pia ukifanya hivo kwa mwezi ni 90,000. Ukiwa unafanya hivo ndio inaitwa kuwekeza, na sio kumpeleka taasisi wa nini kama sio kumtajilisha na uzembe wa mawazo #kumradhi
Hii ndo akili ya kumsaidia mtu.
 
Mkuu soma vizuri uzi wa mdau utamuelewa. Watanzia tupo makundi mengi sana. Kuna watu ambao wapo vibaruani hata huo muda wa kupambana na hizo mbiringe za biashara huenda wasiwe nao lkn kuliko kusema wewe ni mwendo wa kupata kisha unapukutisha kila kitu sio sawa unaweza anza kuweka kidogo kidogo huku ukiendelea kujifunza kitu cha kufanya chenye low risk(kumbuka kwenye risk appetite tunatofautiana pia) siku kamtaji kakikua unajiengua taratibu kwenye kibarua kinachokufanya uwe bize masaa yote ilhali kipato hakikidhi mahitaji. Au ukaacha huko na huo ndo ukawa ujasiliamali wako na ww . Lakini pia kuna watu wakifanikiwa kupata mtaji japo kiasi wanaweza kufanya manipulation kwenye businesses na ndani ya mwaka mmoja ukamkuta mbali kweli(japo ni wachache) ila walio wengi kwenye ujasiliamali unaohusisha day to day activities wanaishia kwenye hand to mouth na wakati mwingine kudorora kabisa. Hata kwenye kilimo vivyo hivyo, hapo kwenye demand and supply ndo mziki ulipo. Unapata mazao mengi mara bei mbovu, unapata mazao kidogo mara bei juu mawinguni unaenda unajipanga kwa nguvu zaidi utoboe mara mvua chache. Yaaani taabu tupu. Kwahiyo ukichunguza sana unakuta mleta maada japo ni muda umepita alikuwa na lengo zuri tuu la kutufanya tufikirie hata fursa zingine ikibidi. Kimsingi hakuna njia moja ambayo ipo very perfect yenye kukufikisha kwenye uhuru wa kiuchumi. Zipo nyingi angalia ipi inaunafuu kwa upande wako
 
Hii kitu haiwezi kuaminika na watu wengi kwa sababu duniani maskini Ni wengi, umaskini unaanzia kichwan
 
Wanao beza nadhani hawajaelewa content ya uzi ,kiini ya uzi ni kuweka akiba inaweza isiwe buku hata 2k,3k,5k inshu kwmba ujiwekee akiba daily
 
Kwa hali halisi ya maisha yetu wabongo inahitaj moyo kwakel kumshawishi mtu kufata njia zako coz mda haukusubili ww
 
Hivi unajua kitu kinaitwa "time value of money?" Hiyo TZS 1,000 yako ya sasa baada ya miaka 2 tu hata pipi huwezi kununua. Hivyo unaweza kuweka hizo 1,000 moja zako na baada ya miaka 30 zikawa na nguvu ya sawa na 50,000 ya sasa.
Ulisema miaka miwili ila ni miaka mitano Sasa elfu moja still inanunua pipi na inalipa nauli.
Uchumi hauendeshwi kwa dhahania na story zenu za vijiweni
 
Makirita Amani nakuomba uandike uzi mwingine kurejerea uzi huu jumatatu nilijaza form ya kuuza vipande vyangu pesa yangu nimeshaingiziwa kwenye akaunti yangu vipande hivi nlianza kununua baada ya kusoma uzi huu 2014 jumatatu nakwenda kulipia kiwanja mlandizi na nadhani ntabakiwa na Kama milioni tatu hivi hapa napiga mahesabu nizungushie fensi au ninunue pikipiki kisha mapato yake niendelee kuwekeza wakati huo kiwanja pia kikipanda thamani.
Moderator JamiiForums au Makirita Amani unaweza kuuatach hii comment hapo juu kwenye uzi ulipokua ukishauri na watu wengi humu wakabeza.
Ahsante sana
 
Makirita Amani nakuomba uandike uzi mwingine kurejerea uzi huu jumatatu nilijaza form ya kuuza vipande vyangu pesa yangu nimeshaingiziwa kwenye akaunti yangu vipande hivi nlianza kununua baada ya kusoma uzi huu 2014 jumatatu nakwenda kulipia kiwanja mlandizi na nadhani ntabakiwa na Kama milioni tatu hivi hapa napiga mahesabu nizungushie fensi au ninunue pikipiki kisha mapato yake niendelee kuwekeza wakati huo kiwanja pia kikipanda thamani.
Moderator JamiiForums au Makirita Amani unaweza kuuatach hii comment hapo juu kwenye uzi ulipokua ukishauri na watu wengi humu wakabeza.
Ahsante sana
Hongera sana mkuu kwa kuchukua hatua kwenye andiko hili la karibu miaka 10 iliyopita na kuona manufaa yake.
Ni vile watu humu wamezoea kupinga kila kitu lakini ukweli hakuna daraja rahisi la uwekezaji hapa Tanzania kama UTT.
Siku hizi nimeacha kupiga kelele na kila mtu kwenye hili, lakini watu wote waliopo kwenye huduma zangu nyingine kuwekeza UTT ni sharti la lazima.
Na hakuna ambaye amewahi kufuata ushauri huo akajutia, zaidi ya kila mmoja kufurahia kwa manufaa makubwa anayoyapata.
Kwa mtu yeyote makini na anayetaka kujenga kesho yake ya kifedha bora, basi sina kingine cha kumshauri zaidi ya kumwambia soma huu uzi kama ulivyo na anza kuwekeza mara moja.
Kiwango weka chochote unachoweza, lakini kadiri unavyoweka kiwango kikubwa, ndivyo manufaa yanavyokuwa makubwa pia.
 
jumatatu nilijaza form ya kuuza vipande vyangu pesa yangu nimeshaingiziwa kwenye akaunti yangu vipande hivi nlianza kununua baada ya kusoma uzi huu 2014 jumatatu nakwenda kulipia kiwanja mlandizi na nadhani ntabakiwa na Kama milioni tatu hivi hapa napiga mahesabu nizungushie fensi au ninunue pikipiki kisha mapato yake niendelee kuwekeza wakati huo kiwanja pia kikipanda thamani.
Mkuu, baada ya kukupa maua yako hapo juu, nikuchane kidogo.
Misingi mikuu ya uwekezaji ni mitatu;
1. Anza mapema
2. Wekeza mara kwa mara
3. Usitoe uwekezaji wako, uache ukue.
Unadhani wewe umevunja sheria ipi kati ya hizo?
 
Moja ya sababu kubwa ambayo watu wengi husema kwamba inawazuia kufanya biashara ni mtaji. Mimi huwa nakataa sana sababu hii kwa sababu haiwezekani leo huna mtaji, mwaka kesho huna mtaji na hata miaka mitano ijayo huna mtaji.
Mtaji ni nini ?
 
Hongera sana mkuu kwa kuchukua hatua kwenye andiko hili la karibu miaka 10 iliyopita na kuona manufaa yake.
Ni vile watu humu wamezoea kupinga kila kitu lakini ukweli hakuna daraja rahisi la uwekezaji hapa Tanzania kama UTT.
Siku hizi nimeacha kupiga kelele na kila mtu kwenye hili, lakini watu wote waliopo kwenye huduma zangu nyingine kuwekeza UTT ni sharti la lazima.
Na hakuna ambaye amewahi kufuata ushauri huo akajutia, zaidi ya kila mmoja kufurahia kwa manufaa makubwa anayoyapata.
Kwa mtu yeyote makini na anayetaka kujenga kesho yake ya kifedha bora, basi sina kingine cha kumshauri zaidi ya kumwambia soma huu uzi kama ulivyo na anza kuwekeza mara moja.
Kiwango weka chochote unachoweza, lakini kadiri unavyoweka kiwango kikubwa, ndivyo manufaa yanavyokuwa makubwa pia.
Upo kwenye huduma gani nyingine ningependa kufahamu zaidi Kama hutojali unipe mawasiliano
 
Sio nature ya watu weusi kuwa na prolonged saving plan tatizo linaanzia hapo. Tunajiangalia wenyewe tunasahau familia tajiri zipo zilipofikia kutokana na mipango ya miongo. Wenzetu mkakati unaanza kizazi cha 1 kinakuja kunufaika kizazi cha 3 huko.
 
Isije ikawa kama pesa zetu za NSSF ambazo baadae unaanza kupangiwa uzitumiaje na wakupe kiasi gani
 
Isije ikawa kama pesa zetu za NSSF ambazo baadae unaanza kupangiwa uzitumiaje na wakupe kiasi gani
Basi tujiwekezee hata bank ili tuwe tunaziona kaka. Nimeona hili andiko leo ila ni kama naiona 2014 na harakati zangu. Hadi najisikia aibu.

Mimi nimeamua kujiwekezea mwenyewe kwa maana serikali yetu haieleweki.
 
Back
Top Bottom