Hivi ni busara kupigana na vibaka kama watatu au zaidi kama wanataka kukuibia simu, hela n.k?

Hivi ni busara kupigana na vibaka kama watatu au zaidi kama wanataka kukuibia simu, hela n.k?

Ivi ni busara kupigana na vibaka Km watatu au zaidi Km wanataka kukuibia cm, hela n.k au bora uwaachie Km unajua umezidiwa? Hili kwa wanaume hata Km unajua kupigana unafanyaje?
Mkuu kama ni usiku, wameshika silaha na wamekuwahi kwenye suala la timing, ni kheri kutulia tu kuliko kusababisha madhara makubwa.
 
Kama hawajakugusa makalio na hapo pengine katikati wala huna haja kupigana nao. Waachie wachukue kama ni simu, hela au chochote (material wise). Wajinga wanaweza kukuchoma bisibisi ukaoza utumbo sababu ya itel.

Kama wana mawazo ya kijinga na makalio yako basi pigana hadi jasho na damu vya mwisho kabisa vitoke
 
Hamna kuachia simu wala kupigana...
Tumia miguu yako vizuriii.

Kwenye hio secta sijawahi kujiangusha,

Mmoja au wawili wepesi wasio na siraha, Pambana kiume wasikuzoee.
Wakabaji lazima wana visu au bisibisi kiunoni. Huwa hawategemei kupigana ngumi, wanachojali wao ni kumaliza tukio haraka iwezekanavyo na kuondoka salama. Na hpo sasa ndio hutumia silaha bila kujali madhara yake sababu anajua wananchi wakimdaka kaisha!
 
Kuna mwamba mmoja soweto Moshi aliamua kama baridi baridi kama moto moto ila sio vuguvugu, alizichapa ngumi mpaka wakasimama kuangaliana, wakaanza kuongea mwisho wa tukio wakaomba pesa ya bangi na jamaa akawapa 10,000 wakaondoka.
Baadae wakawa marafiki.
 
Hivi ni busara kupigana na vibaka kama watatu au zaidi kama wanataka kukuibia simu, hela n.k au bora uwaachie kama unajua umezidiwa?

Hili kwa wanaume hata kama unajua kupigana unafanyaje?
Kwa yeyote anayejua kupigana anakwepa maeneo yote hatarishi . Ila vibaka wakikujaza kwenye 18 unaangalia upepo mfano panya road uwape usiwape lazima ule panga tumia mbinu zote za self defence ikibidi mbio au uzichape kisha mbio ila vibaka wa kawaida hawa wanaowania pesa ruhusu tu wachukue uwe salama.

Onyo acha ubahiri mazingira hatarishi chukua ubber au Boda au piga njia ya mzunguko wa mbali ambayo ni salama achana na short cut ni hatari kwako.
 
Mkuu kama ni usiku, wameshika silaha na wamekuwahi kwenye suala la timing, ni kheri kutulia tu kuliko kusababisha madhara makubwa.
Zali kama hizi natamani zinitokee lakini zinawatokea wengine. Kila siku usiku natembea maksudi keko magurmbasi, temeke mikoroshini, buza, mbagala yani napishana nao tu tunakodoleana macho yananipita kimoyomoyo nasema tu si walianzishe waniv.amia yani huo mkono ntakavoutembeza
 
Back
Top Bottom