MK254
JF-Expert Member
- May 11, 2013
- 32,408
- 50,809
Mara nyingi tumetishiwa nyau na Watanzania kwamba tukifungiana mipaka, Wakenya tutaishia kuangamia maana tunaambiwa tunaihitaji Tanzania kwa hali na mali. Hivyo sasa hii imewapa Watanzania uhuru wa kudhihirisha chuki zao na kutuwaza kila siku.
Imewapa jeuri Watanzania ya kuibuka na kila aina ya sera za chuki dhidi yetu, Watanzania wote wameamishwa hizi chuki na kuwekwa kwenye mazingira ya kuamini kwamba nchi yao ndio hewa tunayoipumua leo, ilhali serikali yetu dhaifu ipo kimya hawajibu kwa lolote. Sasa nawaomba wachumi nguli mtusaidie kudadavua na kubaini nini ambacho tunaweza kupoteza tukipeana talaka na Watanzania kama ilivyotendeka awali maana sio mara ya kwanza kufungiana mpaka.
Ni kweli kuna vitu tutapoteza, lakini pia katika biashara lazima ukubali hasara haswa kwa wadeni jeuri "doubtful debts", au pia huruhusiwa kuachia wateja ambao japo unanufaika na biashara yao lakini wanakukwamisha kwenye mengine mengi.
Binafsi kwa mahesabu ya haraka
- Katika mataifa ambayo tunauza bidhaa zetu, Tanzania imechukua tu nafasi ya asilimia 10% hivyo, asilimia zingine 90% tunauza bila kuwategemea. Kenya imetumia nguvu nyingi sana kupata masoko kwenye mataifa tofauti duniani, leo hii hata KQ inapaa moja kwa moja kwenda Marekani.
- Likija suala la uhusiano baina ya raia wetu, ukweli ni kwamba takwimu huonyesha kwamba Watanzania wengi ndio wanakuja Kenya zaidi ya Wakenya wanaokwenda Tanzania, haswa ukizingatia sera zao dhidi ya Wakenya, ina maana hao Wakenya wachache waliopo huko kwao hawanufaiki pakubwa sana kihivyo, ilhali wao wamejaza Watanzania wao kwa maelfu huku Kenya, na wengi hawana umuhimu wowote huku bali omba omba tu.
- Tofauti baina ya uchumi wa Kenya na Tanzania inazidi kuongezeka, yaani Kenya inazidi kuiacha Tanzania kwa mbali, kuna miaka ya awali tofauti yetu ilikua dola bilioni mbili za Kimarekani, leo hii tofauti imezidi dola bilioni 30, yaani ukiunganisha Uganda, Burundi, Tanzania bado hautakua umetufikia. Tofauti inaendelea kuongezeka.
- Tuna miradi mikubwa inaendelea Kenya kwa leo yaani kuitaja humu nitaishia kujaza server za watu bure.
So kwa kifupi, Kenya yetu kainchi kadogo na nusu yake kame tupu, hatuna madini lakini uwezo wetu upo kwenye nguvu kazi ya watu wetu na kujituma, hicho ni kitu hatuwezi kukipoteza na ndio kimetuwezesha kutawala ukanda wote huu kiuchumi, kijeshi, kielimu n.k.
Imewapa jeuri Watanzania ya kuibuka na kila aina ya sera za chuki dhidi yetu, Watanzania wote wameamishwa hizi chuki na kuwekwa kwenye mazingira ya kuamini kwamba nchi yao ndio hewa tunayoipumua leo, ilhali serikali yetu dhaifu ipo kimya hawajibu kwa lolote. Sasa nawaomba wachumi nguli mtusaidie kudadavua na kubaini nini ambacho tunaweza kupoteza tukipeana talaka na Watanzania kama ilivyotendeka awali maana sio mara ya kwanza kufungiana mpaka.
Ni kweli kuna vitu tutapoteza, lakini pia katika biashara lazima ukubali hasara haswa kwa wadeni jeuri "doubtful debts", au pia huruhusiwa kuachia wateja ambao japo unanufaika na biashara yao lakini wanakukwamisha kwenye mengine mengi.
Binafsi kwa mahesabu ya haraka
- Katika mataifa ambayo tunauza bidhaa zetu, Tanzania imechukua tu nafasi ya asilimia 10% hivyo, asilimia zingine 90% tunauza bila kuwategemea. Kenya imetumia nguvu nyingi sana kupata masoko kwenye mataifa tofauti duniani, leo hii hata KQ inapaa moja kwa moja kwenda Marekani.
- Likija suala la uhusiano baina ya raia wetu, ukweli ni kwamba takwimu huonyesha kwamba Watanzania wengi ndio wanakuja Kenya zaidi ya Wakenya wanaokwenda Tanzania, haswa ukizingatia sera zao dhidi ya Wakenya, ina maana hao Wakenya wachache waliopo huko kwao hawanufaiki pakubwa sana kihivyo, ilhali wao wamejaza Watanzania wao kwa maelfu huku Kenya, na wengi hawana umuhimu wowote huku bali omba omba tu.
- Tofauti baina ya uchumi wa Kenya na Tanzania inazidi kuongezeka, yaani Kenya inazidi kuiacha Tanzania kwa mbali, kuna miaka ya awali tofauti yetu ilikua dola bilioni mbili za Kimarekani, leo hii tofauti imezidi dola bilioni 30, yaani ukiunganisha Uganda, Burundi, Tanzania bado hautakua umetufikia. Tofauti inaendelea kuongezeka.
- Tuna miradi mikubwa inaendelea Kenya kwa leo yaani kuitaja humu nitaishia kujaza server za watu bure.
So kwa kifupi, Kenya yetu kainchi kadogo na nusu yake kame tupu, hatuna madini lakini uwezo wetu upo kwenye nguvu kazi ya watu wetu na kujituma, hicho ni kitu hatuwezi kukipoteza na ndio kimetuwezesha kutawala ukanda wote huu kiuchumi, kijeshi, kielimu n.k.