Hivi, ni kipi Kenya inaweza ikapoteza tukifungiana mpaka na Tanzania

Hivi, ni kipi Kenya inaweza ikapoteza tukifungiana mpaka na Tanzania

Hayo yote uliyoyaandika ni kama mpuuzi asiye na akili anayejisifia Shule yetu imeongoza kitaifa matokeo ya level fulani ya elimu ilihali yeye binafsi katika matokeo ya mtihani huo amepata Division Zero. Kiukweli uchumi wa Kenya kuwa juu hakumnufaishi Mwananchi wa kawaida wa Kenya na wanaofaidi Keki ya Taifa la Kenya ni mabaki ya Settlers, nchi za Ulaya na Marekani na wakenya wachache ambao hawazidi hata 1%. Hii imepelekea purchasing power ya wakenya walio wengi kuwa chini na kuishi maisha ya hovyo ukilinganisha na nchi zingine za East Africa. Kwa ufupi uchumi wa Kenya haupo mikononi mwa raia wa nchi hiyo kitu ambacho ni tofauti na Tanzania ambapo uchumi wa nchi kwa asilimia kubwa unamilikiwa na wananchi wenyewe na kuwafanya kuwa na purchasing power kubwa kuliko wakenya.

Sent using Jamii Forums mobile app

Hii haijajibu swali langu maana ni yale yale mliaminishwa kwamba Kenya yote inamilikiwa na wazungu, hilo tulishalijadili tukajaribu kuwaelimisha lakini kwa mlivyo mabumbumbu hamkuelewa. Ni kama tusemavyo utajiri asilimia 70% wa Tanzania umemilikiwa na wahindi na waarabu ambao ndio kumi bora kwa wanaoimiliki Tanzania, maana humo Watanganyika weusi hawana lolote, labda mmoja tu yule Mchagga bwana Mengi, wengine wote kajamba wa Manzense.
 
Hizo bidhaa mnazo zalisha na kuuza tz 10℅ na 90% kuuza sehemu nyingine unajua malighafi asilimia ngapi zinatoka tz ? Tena unajua kwanini wawekezaji wa kigeni na mashirika mbalimbali ya kigeni yanawekeza Kenya badala ya tz Kwa kifupi madini na rasilimali za tz zinazo ibiwa zinafichwa Kenya hata madini yaliyo kamatwa majuzi yalikuwa yanaenda Kenya sikuzote mwizi uficha mali ya wizi nje ya alipo Fanya wizi wazungu na waasia wakishirikiana na serikali ya kenya wanao ibia tz wameifanya Kenya kuwa kituo cha wizi wao tz
Ndiyo maana unashangaa kwanini serikali ya Kenya hipo kimya ma bwanyenye wanao himiliki Kenya wanaogopa kama nini mpaka ukifungwa Kwa 100% wanajua vizuri hii kitu ila Kwa we we MK 254 inaonyesha itakuwa ni masikini wa kibera ndiyo maana ujui hadi unashangaa kwanini serikali yenu inanywea kuusu tz inaogopa kuvimbisha kifua

Sent using Jamii Forums mobile app

Leta takwimu za malighafi kiasi gani ambacho kinatoka Tanzania, na kama kweli kuna asilimia kubwa ya maliighafi inahuska kwenye mauzo ya bidhaa zetu, ina maana tukifungiana mipaka, na nyie pia mtaishia kujamba huko maana zitaozea huko huko.
Hayo ya madini hayana mashiko maana yanawanufaisha Wakenya na Watanzania wachache, hivyo sio kitu cha kupoteza muda kukijadili humu.
 
Unajua maana ya 10% au unaropoka Tu? Kama vipi Ondokeni tuuu na dharau zenuu..

Ndio nataka nijuzwe hiyo 10% ni kiasi gani cha kusababisha tuangamie tukiikosa.
 
Mshauri Mh. Kenyatta afunge tu huo mpaka hakuna jinsi.
 
mleta mada ombea hilo lisitokee maana kila mmoja atapata hasaha kwa kiasi chake na watakao umia ni raia wengi.Kikubwa ambacho kinatakiwa ni kuondoa tofauti zetu hasa kwa viongozi wetu ili kuendelea kudumisha urafiki ambao kwa sasa unaonekana upo kimya kimya uwe wa wasi ili kudumisha biashara zetu ktk ukanda wetu.
Hata kama faida ni ndogo au kubwa kwa kila upande kutegemeana lkn umoja ni muhimu kudumishwa na tusiombee utengano hata siku moja
 
Hii haijajibu swali langu maana ni yale yale mliaminishwa kwamba Kenya yote inamilikiwa na wazungu, hilo tulishalijadili tukajaribu kuwaelimisha lakini kwa mlivyo mabumbumbu hamkuelewa. Ni kama tusemavyo utajiri asilimia 70% wa Tanzania umemilikiwa na wahindi na waarabu ambao ndio kumi bora kwa wanaoimiliki Tanzania, maana humo Watanganyika weusi hawana lolote, labda mmoja tu yule Mchagga bwana Mengi, wengine wote kajamba wa Manzense.
Kwa ufupi kama kusipokuwa na tatizo la upungufu wa mvua Tanzania ina uwezo wa kutoa guarantee ya food security kwa population yote ya East Africa community kitu ambacho nchi ya Kenya haiwezi kufanya kufanya hivyo kujitosheleza kwa chakula yenyewe hata kwa mwaka mmoja rejea scenario ya mwaka jana baada ya Tanzania kukaza kutouza mahindi yake nje nchi ya Kenya walipata taabu sana mpaka kulazimika kufanya Importation ya mahindi kutoka nchi nyingine. Kwahiyo jeuri inayopata Tanzania kutokana na mauzo yake ya bidhaa za chakula kwa nchi jirani ndiyo inawapa nguvu ya manunuzi(purchasing power) watanzania walio wengi rejea wananchi wengi wa Tanzania wanajishughulisha na kilimo. Kitu ambacho ni tofauti na Kenya uchumi wa Kenya unategemea viwanda vya kati ambavyo soko lake kuu ni Tanzania kwa bidhaa kama Kiwi, Maziwa n.k. na profit inayopatikana kwa viwanda hvy hairudi kwa wananchi wa Kenya but owners wa hvy viwanda ambavyo asilimia kubwa ni Foreigners hali inayowapelekea wananchi wengi wa Kenya kuwa na Maisha duni na kuwa watumwa ndani ya nchi yao. Rejea hata hy KQ uliyoitaja fuatili share holders wa shirika hilo ni wakina nani tofauti na Air Tanzania.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa jinsi Al Shaabab wanavyowachapa, fungeni mipaka halafu muone! All ur access to SADC countries will evaporate also! Tourism package will also seize! Mlifunga 1977 mpaka Leo mnalilia Bolongoja gate!
 
Leta takwimu za malighafi kiasi gani ambacho kinatoka Tanzania, na kama kweli kuna asilimia kubwa ya maliighafi inahuska kwenye mauzo ya bidhaa zetu, ina maana tukifungiana mipaka, na nyie pia mtaishia kujamba huko maana zitaozea huko huko.
Hayo ya madini hayana mashiko maana yanawanufaisha Wakenya na Watanzania wachache, hivyo sio kitu cha kupoteza muda kukijadili humu.
Malighafi nyingi mnazopata kutoka tz ni za wizi na madini ya wizi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa ufupi kama kusipokuwa na tatizo la upungufu wa mvua Tanzania ina uwezo wa kutoa guarantee ya food security kwa population yote ya East Africa community kitu ambacho nchi ya Kenya haiwezi kufanya kufanya hivyo kujitosheleza kwa chakula yenyewe hata kwa mwaka mmoja rejea scenario ya mwaka jana baada ya Tanzania kukaza kutouza mahindi yake nje nchi ya Kenya walipata taabu sana mpaka kulazimika kufanya Importation ya mahindi kutoka nchi nyingine. Kwahiyo jeuri inayopata Tanzania kutokana na mauzo yake ya bidhaa za chakula kwa nchi jirani ndiyo inawapa nguvu ya manunuzi(purchasing power) watanzania walio wengi rejea wananchi wengi wa Tanzania wanajishughulisha na kilimo. Kitu ambacho ni tofauti na Kenya uchumi wa Kenya unategemea viwanda vya kati ambavyo soko lake kuu ni Tanzania kwa bidhaa kama Kiwi, Maziwa n.k. na profit inayopatikana kwa viwanda hvy hairudi kwa wananchi wa Kenya but owners wa hvy viwanda ambavyo asilimia kubwa ni Foreigners hali inayowapelekea wananchi wengi wa Kenya kuwa na Maisha duni na kuwa watumwa ndani ya nchi yao. Rejea hata hy KQ uliyoitaja fuatili share holders wa shirika hilo ni wakina nani tofauti na Air Tanzania.

Sent using Jamii Forums mobile app

Bado hili halijajibu swali langu maana mahindi ni yenu, ardhi ni yenu lakini hela za kununua ni zetu, hamtupi kama msaada, mwaka mlioshindwa kuzalisha mahindi ya kujitosheleza, kwa njaa zenu na chuki mkazuia kutuuzia, lakini kwa sababu tulikua na hela zetu, mataifa mengine yakapiga hodi na kutuuzia tena kwa kutubembeleza, hiyo inaitwa jeuri ya kuwa na hela.
Swali langu lilikua, ikitokea tumefungiana, ni kwa jinsi gani Kenya itaangamia, leo hii tumeona mkifungia vitu ambavyo huwa tunawategemea navyo, na bado hatukuangamia, hayo mahindi kuna mataifa mengi tu yanazalisha na mazao yanaozea kwenye maghala kwa kukosa wanunuzi, hivyo ukiwa na jeuri ya hela hutababaishwa.

Ni kweli tukifungiana mipaka kuna jinsi tutaumia, na sio mara ya kwanza kufungiana mpaka, lakini na nyie pia cha moto mtakiona huko huko na umaskini wenu, chochote mnachotuuzia kitaozea huko huko.
 
Malighafi nyingi mnazopata kutoka tz ni za wizi na madini ya wizi

Sent using Jamii Forums mobile app

Nimekuambia hayo ya wizi yanawanufaisha wachache, maana Wakenya hawaji na kuiba wenyewe, lazima kuna Watanzania wanashirikiana nao, hivyo ni wachache tu wataona cha moto kama ikitokea tumefungiana, biashara za magendo hunufaisha mabwenyenye wachache, haswa kwenye nchi yenu hiyo shamba la bibi inaliwa sana na Wasouth, Wachina, Wahindi na Waarabu.
Watanganyika wengi ni makajamba wa kukaa pembeni wakiona mkiliwa na mabeberu, kuna siku mliahidiwa noah kwa kila Mtanzania ila ikaishia stori.
 
mleta mada ombea hilo lisitokee maana kila mmoja atapata hasaha kwa kiasi chake na watakao umia ni raia wengi.Kikubwa ambacho kinatakiwa ni kuondoa tofauti zetu hasa kwa viongozi wetu ili kuendelea kudumisha urafiki ambao kwa sasa unaonekana upo kimya kimya uwe wa wasi ili kudumisha biashara zetu ktk ukanda wetu.
Hata kama faida ni ndogo au kubwa kwa kila upande kutegemeana lkn umoja ni muhimu kudumishwa na tusiombee utengano hata siku moja

Binafsi siombei, lakini kwa utawala wenu wa leo mumezidisha chuki sana dhidi ya Kenya hadi sioni nafuu gani ya muungano ambayo inafaa kuruhusu yanayotendeka leo. Ni kweli tukifungiana tutaumia sote, kuna asilimia kiasi fulani itaumia pande zote mbili, lakini Watanzania wengi wameminishwa na kudanganywa kwamba wao hawana lolote la kupoteza na ndio inawapa jeuri ya kuendekeza chuki.
 
Mara nyingi tumetishiwa nyau na Watanzania kwamba tukifungiana mipaka, Wakenya tutaishia kuangamia maana tunaambiwa tunaihitaji Tanzania kwa hali na mali. Hivyo sasa hii imewapa Watanzania uhuru wa kudhihirisha chuki zao na kutuwaza kila siku.
Imewapa jeuri Watanzania ya kuibuka na kila aina ya sera za chuki dhidi yetu, Watanzania wote wameamishwa hizi chuki na kuwekwa kwenye mazingira ya kuamini kwamba nchi yao ndio hewa tunayoipumua leo, ilhali serikali yetu dhaifu ipo kimya hawajibu kwa lolote. Sasa nawaomba wachumi nguli mtusaidie kudadavua na kubaini nini ambacho tunaweza kupoteza tukipeana talaka na Watanzania kama ilivyotendeka awali maana sio mara ya kwanza kufungiana mpaka.
Ni kweli kuna vitu tutapoteza, lakini pia katika biashara lazima ukubali hasara haswa kwa wadeni jeuri "doubtful debts", au pia huruhusiwa kuachia wateja ambao japo unanufaika na biashara yao lakini wanakukwamisha kwenye mengine mengi.

Binafsi kwa mahesabu ya haraka
- Katika mataifa ambayo tunauza bidhaa zetu, Tanzania imechukua tu nafasi ya asilimia 10% hivyo, asilimia zingine 90% tunauza bila kuwategemea. Kenya imetumia nguvu nyingi sana kupata masoko kwenye mataifa tofauti duniani, leo hii hata KQ inapaa moja kwa moja kwenda Marekani.
- Likija suala la uhusiano baina ya raia wetu, ukweli ni kwamba takwimu huonyesha kwamba Watanzania wengi ndio wanakuja Kenya zaidi ya Wakenya wanaokwenda Tanzania, haswa ukizingatia sera zao dhidi ya Wakenya, ina maana hao Wakenya wachache waliopo huko kwao hawanufaiki pakubwa sana kihivyo, ilhali wao wamejaza Watanzania wao kwa maelfu huku Kenya, na wengi hawana umuhimu wowote huku bali omba omba tu.
- Tofauti baina ya uchumi wa Kenya na Tanzania inazidi kuongezeka, yaani Kenya inazidi kuiacha Tanzania kwa mbali, kuna miaka ya awali tofauti yetu ilikua dola bilioni mbili za Kimarekani, leo hii tofauti imezidi dola bilioni 30, yaani ukiunganisha Uganda, Burundi, Tanzania bado hautakua umetufikia. Tofauti inaendelea kuongezeka.
- Tuna miradi mikubwa inaendelea Kenya kwa leo yaani kuitaja humu nitaishia kujaza server za watu bure.

So kwa kifupi, Kenya yetu kainchi kadogo na nusu yake kame tupu, hatuna madini lakini uwezo wetu upo kwenye nguvu kazi ya watu wetu na kujituma, hicho ni kitu hatuwezi kukipoteza na ndio kimetuwezesha kutawala ukanda wote huu kiuchumi, kijeshi, kielimu n.k.
Leta na takwimu kabisa kwa jinsi gani tunanunua hivi vitu kutoka kwenu na mkifunga mpaka tutaangamia, maana kwa mfano kuna vipindi kwenu mnakua na njaa kiasi cha kutoweza kuuza hayo mahindi nje, tunaagiza kutoka mataifa mengine na tunaendelea na maisha tu bila kuangamia.
Ikumbukwe pia hamtupi bure wala kama misaada, hivyo tukifungiana, mtaishia na bidhaa hizo zikiozea huko na kwamba sisi tutanunua kwengine kama ilivyo mazoea kila mkikurupuka kuvifungia.
Kitu muhimu ni kwamba hela tunazo za kuweza kununua chochote ambacho hatuzalishi, na kuna mataifa mengi tu ambayo yanakanyagana yakija kutafuta soko kwetu
Wewe ndiyo ulete takwimu from reliable sources, acha kutapika sukuma wiki.
 
Mshauri Mh. Kenyatta afunge tu huo mpaka hakuna jinsi.

Ningependa wanaomshauri rais Uhuru wapitie huku ili watuambie kipi tutapoteza na kuangamia iwapo tutafungiana.
 
Wewe ndiyo ulete takwimu from reliable sources, acha kutapika sukuma wiki.

Mimi nimeomba wataalam wa uchumi waniambie tutaangamia vipi ikitokea tumepeana talaka na Tanzania, sasa kama wewe mtaalam, tiririka na takwimu zako tuone jinsi gani tutakosa hewa na kufa.
 
Bado hili halijajibu swali langu maana mahindi ni yenu, ardhi ni yenu lakini hela za kununua ni zetu, hamtupi kama msaada, mwaka mlioshindwa kuzalisha mahindi ya kujitosheleza, kwa njaa zenu na chuki mkazuia kutuuzia, lakini kwa sababu tulikua na hela zetu, mataifa mengine yakapiga hodi na kutuuzia tena kwa kutubembeleza, hiyo inaitwa jeuri ya kuwa na hela.
Swali langu lilikua, ikitokea tumefungiana, ni kwa jinsi gani Kenya itaangamia, leo hii tumeona mkifungia vitu ambavyo huwa tunawategemea navyo, na bado hatukuangamia, hayo mahindi kuna mataifa mengi tu yanazalisha na mazao yanaozea kwenye maghala kwa kukosa wanunuzi, hivyo ukiwa na jeuri ya hela hutababaishwa.

Ni kweli tukifungiana mipaka kuna jinsi tutaumia, na sio mara ya kwanza kufungiana mpaka, lakini na nyie pia cha moto mtakiona huko huko na umaskini wenu, chochote mnachotuuzia kitaozea huko huko.
Samahani kwa kutoka nje ya mada, naomba kujua una asili ya kutoka mji gani wa Kenya?
Maana una dalili zote za kuwa mTz.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Keny, ndio taifa lenye deni kubwa kuliko yote EAC. Yaani deni la kenya ni sawa na robo y auchumi wa Tz, halafu deni lenyewe halilipiki, mchina anachukua Kenya yake. Bora tu tufunge mpaka
 
Mara nyingi tumetishiwa nyau na Watanzania kwamba tukifungiana mipaka, Wakenya tutaishia kuangamia maana tunaambiwa tunaihitaji Tanzania kwa hali na mali. Hivyo sasa hii imewapa Watanzania uhuru wa kudhihirisha chuki zao na kutuwaza kila siku.
Imewapa jeuri Watanzania ya kuibuka na kila aina ya sera za chuki dhidi yetu, Watanzania wote wameamishwa hizi chuki na kuwekwa kwenye mazingira ya kuamini kwamba nchi yao ndio hewa tunayoipumua leo, ilhali serikali yetu dhaifu ipo kimya hawajibu kwa lolote. Sasa nawaomba wachumi nguli mtusaidie kudadavua na kubaini nini ambacho tunaweza kupoteza tukipeana talaka na Watanzania kama ilivyotendeka awali maana sio mara ya kwanza kufungiana mpaka.
Ni kweli kuna vitu tutapoteza, lakini pia katika biashara lazima ukubali hasara haswa kwa wadeni jeuri "doubtful debts", au pia huruhusiwa kuachia wateja ambao japo unanufaika na biashara yao lakini wanakukwamisha kwenye mengine mengi.

Binafsi kwa mahesabu ya haraka
- Katika mataifa ambayo tunauza bidhaa zetu, Tanzania imechukua tu nafasi ya asilimia 10% hivyo, asilimia zingine 90% tunauza bila kuwategemea. Kenya imetumia nguvu nyingi sana kupata masoko kwenye mataifa tofauti duniani, leo hii hata KQ inapaa moja kwa moja kwenda Marekani.
- Likija suala la uhusiano baina ya raia wetu, ukweli ni kwamba takwimu huonyesha kwamba Watanzania wengi ndio wanakuja Kenya zaidi ya Wakenya wanaokwenda Tanzania, haswa ukizingatia sera zao dhidi ya Wakenya, ina maana hao Wakenya wachache waliopo huko kwao hawanufaiki pakubwa sana kihivyo, ilhali wao wamejaza Watanzania wao kwa maelfu huku Kenya, na wengi hawana umuhimu wowote huku bali omba omba tu.
- Tofauti baina ya uchumi wa Kenya na Tanzania inazidi kuongezeka, yaani Kenya inazidi kuiacha Tanzania kwa mbali, kuna miaka ya awali tofauti yetu ilikua dola bilioni mbili za Kimarekani, leo hii tofauti imezidi dola bilioni 30, yaani ukiunganisha Uganda, Burundi, Tanzania bado hautakua umetufikia. Tofauti inaendelea kuongezeka.
- Tuna miradi mikubwa inaendelea Kenya kwa leo yaani kuitaja humu nitaishia kujaza server za watu bure.

So kwa kifupi, Kenya yetu kainchi kadogo na nusu yake kame tupu, hatuna madini lakini uwezo wetu upo kwenye nguvu kazi ya watu wetu na kujituma, hicho ni kitu hatuwezi kukipoteza na ndio kimetuwezesha kutawala ukanda wote huu kiuchumi, kijeshi, kielimu n.k.
Kule kuanza kufikiria tu kufunga mpaka ni mawazo potofu. Hilo lije tu panapokuwepo na mgogoro halisi ambao umeshindikana kutatuliwa. Mbali na hayo, kama kunakuwepo na kutoelewana hapa na pale, hiyo ni kawaida ya maisha. Tutatue hilo tatizo na kuendelea mbele. Hata kwenye familia kunakuwepo kutofautiana kati ya mume na mke au mzazi na mtoto. Huwezi kuanza kufikiria talaka au kufukuza mtoto mpaka hapo kila kitu kingine kitakapokuwa kimeshindikana.
 
Binafsi kwa mahesabu ya haraka
- Katika mataifa ambayo tunauza bidhaa zetu, Tanzania imechukua tu nafasi ya asilimia 10% hivyo, asilimia zingine 90% tunauza bila kuwategemea. Kenya imetumia nguvu nyingi sana kupata masoko kwenye mataifa tofauti duniani, leo hii hata KQ inapaa moja kwa moja kwenda Marekani.
- Likija suala la uhusiano baina ya raia wetu, ukweli ni kwamba takwimu huonyesha kwamba Watanzania wengi ndio wanakuja Kenya zaidi ya Wakenya wanaokwenda Tanzania, haswa ukizingatia sera zao dhidi ya Wakenya, ina maana hao Wakenya wachache waliopo huko kwao hawanufaiki pakubwa sana kihivyo, ilhali wao wamejaza Watanzania wao kwa maelfu huku Kenya, na wengi hawana umuhimu wowote huku bali omba omba tu.
- Tofauti baina ya uchumi wa Kenya na Tanzania inazidi kuongezeka, yaani Kenya inazidi kuiacha Tanzania kwa mbali, kuna miaka ya awali tofauti yetu ilikua dola bilioni mbili za Kimarekani, leo hii tofauti imezidi dola bilioni 30, yaani ukiunganisha Uganda, Burundi, Tanzania bado hautakua umetufikia. Tofauti inaendelea kuongezeka.
- Tuna miradi mikubwa inaendelea Kenya kwa leo yaani kuitaja humu nitaishia kujaza server za watu bure.
Based on this, you are trying to tell us something. Not otherwise.
 
Back
Top Bottom