Hivi ni kwanini jua linapochomoza na linapokaribia kuzama sio kali sana kama linavyokuwa muda wa mchana?

Mfano ni toch inavyokumilka, chukua mpo watu wawili umbali wa mita 100 then toch imlenge mmoja, obviously mtu wa pili ambaye hajalengwa (pembeni) ataona mwanga hafifu (joto) tofauti na aliyemulikwa centre.
Mtu aliye pembeni na nyuma yake. Usisahau umbo la duania siyo bapa.
 
Let's say I'm marking your answer:

2/5 marks
 
Umbali unaohusika hapa siyo kati ya dunia na jua kwa ujumla, bali ni kati ya eneo mahususi la dunia alipo mtazamaji na jua.

Umbali huo huathiriwa na umbo la dunia.
 
Hivi ni kwanini jua linapochomoza na linapokaribia kuzama sio Kali sana kama linavyokuwa muda wa mchana?

Wajuzi karibuni.

Asante sana.
Tofauti ya umbali kati ya jua na dunia ,pia umbo la mduara la dunia lakini sababu zote mbili zinakua na maana kutokana na mzunguko wa dunia kulizunguka jua
 
Uchawi upo kwenye the angle upon which solar rays hit the atmosphere....hapo ndipo husababisha
  • Hali joto kupungua or kuongezeka
  • Muonekano wa umbo la jua
  • Aurora lights
Unachanganya mambo mawili kwa wakati mmoja.

Swali ni mahususi kuhusu jua kali mchana kuliko magharibi na asubuhi.

Aidha, pembe ya miale ya jua inapaswa iwe kumridhi (with respect to) eneo mahususi la dunia na wala siyo angahewa tu.

Rejea jibu #28
 
Unachanganya mambo mawili kwa wakati mmoja.

Swali ni mahususi kuhusu jua kali mchana kuliko magharibi na asubuhi.

Aidha, pembe ya miale ya jua inapaswa iwe kumridhi (with respect to) eneo mahususi la dunia na wala siyo angahewa tu.

Rejea jibu #28
Uchawi wote ni upon angle ya solar rays hitting the atmosphere....

 
Jibu hili ni ushahidi mkubwa kwamba watu wengi wanakiriri mambo na kunakili tu bila kujua wanachoandika.

1/10 marks.
 
The reason is that earth rotates on its axis and its takes 24 hours to make one revolution.
When we are on the side of Earth that is facing the Sun, we have daylight. As Earth continues its spin, we are moved to the side facing away from our Sun, and we have nighttime.
So pale dunia inapoanza kulitazama jua lazima ukali wa jua utakuwa mdogo na dunia inavyozidi kulitazama jua upande wetu linakuwa kali zaidi.
 
Hivi ni kwanini jua linapochomoza na linapokaribia kuzama sio Kali sana kama linavyokuwa muda wa mchana?

Wajuzi karibuni.

Asante sana.
Njia rahisi kumuelewesha kuhusu hili ni katika matumizi ya tochi kumulika. Mwanga wa tochi unavyomulika mbali utawanyika zaidi lakini mwangaza na ukali wa mwanga wake hupungua. Lakini ukiweka mkono karibu natochi mwanga utamulika sehemu moja kwamaana ya mwanga utakusanywa na intensity yake itakuwa kali (mwangaza mkali).
Vivyo hivyo, katika jua na dunia. Dunia inapozunguka inafika wakati AFRIKA inakuwa perpendicular 90degree na jua. Hivyo jua linakuwa kali. Lakini inavyozidi dunia kujizungusha sehemu hyo ya Afrika huwa mbali zaidi mpaka nyuzi 180 hivyo hupata mwanga usio mkali. Intensity inapungua hiyo wakati wa jioni na asubuhi. Mahali ambapo wewe upo hiwa mbali na jua miale hutawanywa zaidi na hivyo intensity huwa low.
Bila shaka sio slow Lerner utakuwa umeelewa babu mkongwe.
 
Hujajibu swali.
0.5/10
 
So pale dunia inapoanza kulitazama jua lazima ukali wa jua utakuwa mdogo na dunia inavyozidi kulitazama jua upande wetu linakuwa kali zaidi.
Swali la msingi: Kwa nini jua liwe kali mchana kuliko asubuhi ^pale dunia inapoanza kulitazama jua,^ au jioni ^pale dunia [inapoacha] kulitazama jua^?
 
Swali la msingi: Kwa nini jua liwe kali mchana kuliko asubuhi ^pale dunia inapoanza kulitazama jua,^ au jioni ^pale dunia [inapoacha] kulitazama jua^?
Nimeelezea hapo, mchana jua linakuwa over the head.

Asubuhi jua liko kwenye horizon kwahiyo sun rays zinatravel umbali mrefu kwenye atmosphere kutufikia hence it seems no so hot, while in mid day sun is over the head hence too hot kwasababu sehemu tulipo inakuwa inatazamana na jua moja kwa moja.
 
Umbali unaohusika hapa siyo kati ya dunia na jua kwa ujumla, bali ni kati ya eneo mahususi la dunia alipo mtazamaji na jua.

Umbali huo huathiriwa na umbo la dunia.
Hayo ni maneno mengi tu ambayo kimsingi ni sawa na kusema uso wa dunia.
Generally ni uso wa dunia na angle of incidence.
Ndiyo maana nimetumia neno "uso wa dunia". Asante kwa ufafanuzi, ila sorry ni kama umezidisha maneno.
 
Ikiwa miale ya point a,hufika duniani ikiwa dhaifu zaidi kutokana na umbali zaidi mpaka kusababisha barafu wakati mwingi eneo hilo,basi hata point C niliyoweka alama inaathirika kwa mtindo ule ule wakati jua litakapokuwa limesogea kuzunguka upande wa nyuma.
Tofauti ya C na A ni kwamba c inakuwa na vipindi vyote kwa masaa 24 tu,ila a haifikiwa na miale jua sawa sawa zaidi ya mwanga hafifu tu.

Labda swali gumu ni kujiuliza kwanini huwa linaonekana ni kubwa zaidi.
 
Uzi huu ningeleta mimi watu wangeupotezea na kuona nawazingua, sababu sina umaarufu. Kwavile kauleta Bujibuji wadau wanaumiza vichwa kwanini jua ni kali mchana! Anyways hii dunia haiko fair kabisa.
 
Hili swali hata Mimi niliwahi kujiuluza nikakosa majibu

Ni mda upi Jua linakuwa lipo mbli nasi?

Kama ni asubuhi ndio lipo mbali kwanini tunaliona kuwa ni kubwa kuliko mchana linapokuwa karibu?

Kama asubuhi ndio lipo karibu Kwa Nini miale yake Haina nguvu kuliko mchana ambapo lipo mbali?

Hata mwezi pia unapochomoza unaonekana mkubwa kuliko unapokuwa usawa wa utosi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…