Hivi ni kwanini siku hizi watu hawapigani mitaani kama miaka ya 1980s?

Hivi ni kwanini siku hizi watu hawapigani mitaani kama miaka ya 1980s?

zile zilikua zinanaitwa enzi za ujinga,leo mtu anasifiwa pesa sio mabavu tena.nakumbuka hata mitaani kwetu walikua wanavuma zana wenye kupiga kumi na mabavu sana ila sasa watu tumeelimika maendeleo kwanza ndoo heshima hata kama mtoto utaitwa mzee,kitu mpungaaa.
 
Mleta mada unanikumbusha mbali sana 1981 ama 1982 kama sijakosea kuna dogo flan aliingia anga zangu kijijin huko mbarali kwa kumtongoza mchepuko wangu. Nilitembeza vitasa kijiji kizima kwa madogo wote wenye umri kama wake. Maumiv makal sana niliwakabiz kwa kosa la mtu mmoja. Yan nilikuwa na bwaka nikiibuka 10 ardhin nikizama nikichomoza 20 wengine chali. Nikamchukua dogo mwengine mwembamba hiv nikamtumia kama fimbo kwa kuwacharaza. Ila kwasasa nimejikita zaid kusaka hela uzee nao ndio huo. Ila miaka iyo ya themanini nilikuwa mtemi sana
heeeeee, boss hapo kuanguka na 10 kuzimama na 20 umekaanga mbuyu,,,,,hahahahaaaaa
 
Zamani Elimu haikua ya kutosha....wapumbavu walikua wengi kuliko wastaarabu...
Kadri siku zinavyokwenda wapumbavu wanakufa, wanapungua au wana badilika na kuwa werevu...ndio maana hamna kupigana pigana

Elimu muhimu Sana.
 
Nakumbuka miaka ya 80-90 ilikuwa jambo la kawaida kukuta jamaa wanapigana mitaani halafu watu wanashangilia sana.

Yaani ukiwa mtemi au gangwe basi unaonekana wa maana sana. Hata baadhi ya disco ilikuwa lazima ziishe kwa ngumi.

Kwa wale wa Iringa mtawakumbuka kina cool 9, shedadi, Ray nk
zamani watu walikuwa hawapelekani kwenye vyombo vya sheria kama sasa hv. Mambo yalikuwa yanaishia uwanja wa mapambano. Kwasasa utamtajirisha mtu bure. Halafu ustaarabu umeongezeka kwa watu wengi.
 
utahira tu kupigana hadharai watu wanapambana kutafuta maisha yao yakae sawa....af eti kupigana haijalishi una nguvu unaweza viziwa tu naukaumizwa ukapa hasara ya maisha....au ukuawa au ukafa manamtu anajua hawezi kukupiga so anakausha anakuvizia..upuuzi huo tu piganana shetani u kwa sasa
This is childhood thing hapo sio watu wazima wanaozungumziwa
 
Nakumbuka miaka ya 80-90 ilikuwa jambo la kawaida kukuta jamaa wanapigana mitaani halafu watu wanashangilia sana.

Yaani ukiwa mtemi au gangwe basi unaonekana wa maana sana. Hata baadhi ya disco ilikuwa lazima ziishe kwa ngumi.

Kwa wale wa Iringa mtawakumbuka kina cool 9, shedadi, Ray nk
Kipindi hicho walikua wanakula ugali wanashiba,sasa kizazi hiki cha chips yai na andazi nguvu za kupigana wanapata wapi.

Pia bangi za zamani zilikua og yani wahuni walikua wahuni kweli kweli.

Hiphop ngumu,sio sikuhizi mtoto wakiume anaimba nyimbo zote za zuchu.

What a loss generation
 
Ngumi nimepigana Sana Ila mapambano Kati ya sabini niliohudhuria mtaani kwetu hasa ukizingatia nilikuwa mwingi wa hasira na mwepesi kuzikunja ,kiukweli nakumbuka ni mawili tu ndiyo nilishinda Ila mengine nilichezea kipigo haswa uzuri Sina alama ya kuikumbuka kuwa nilikung'utwa
 
Vijana wengi wa 2000 afya hawana wapo wembamba kama askilimu au mnyoo nguvu za kupigana zitoke wapi kutembea tupu kijana kama zombi sijui kumetokea Nini Kwa vijana wa sasa
 
Back
Top Bottom