Hivi ni kwanini siku hizi watu hawapigani mitaani kama miaka ya 1980s?

Hivi ni kwanini siku hizi watu hawapigani mitaani kama miaka ya 1980s?

Siku hizi unakuta kijana kavaa Suruali chini ya Makalio,sasa hapa atapigana vipi? Si itaanguka! Watoto wa siku hizi ni ubishoo na vimatusi kwenye social media tu,Kijana kapaka poda,cream ya kulainisha ngozi na hereni sikioni,saa ngapi atawaza kupigana? Afya zenyewe siku hizi ni mchoko tu,unaweza kukuta mtu anatembea kumbe kisha jifia zamani! Ukigusa tu unakua umenunua kesi ya mauwaji!

Halafu zamani eti ukipigana lazima uvue shati ili lisije kuchanika na Mama akajua home kua umepigana,

Where are those gold days aiseee?!

 
Mleta mada unanikumbusha mbali sana 1981 ama 1982 kama sijakosea kuna dogo flan aliingia anga zangu kijijin huko mbarali kwa kumtongoza mchepuko wangu. Nilitembeza vitasa kijiji kizima kwa madogo wote wenye umri kama wake. Maumiv makal sana niliwakabiz kwa kosa la mtu mmoja. Yan nilikuwa na bwaka nikiibuka 10 ardhin nikizama nikichomoza 20 wengine chali. Nikamchukua dogo mwengine mwembamba hiv nikamtumia kama fimbo kwa kuwacharaza. Ila kwasasa nimejikita zaid kusaka hela uzee nao ndio huo. Ila miaka iyo ya themanini nilikuwa mtemi sana
Hatari sana....
 
Ha ha haaa umeanza mkwara wa keyboard?

Hahaha! Nilimsikia Mitemba anamwambia mzee Jongo kwenye mchezo wa radio. Jongo bwana alimwambia Mitemba kwamba kama sio uchovu wa safari aliokuwa nao wangeshikana mashati (Kosema kama sio kuchoka safari, nakwambia hapa ngumi zingewaka moto ndii). Mitemba akamwambia Jongo nakupa wiki moja kapumzike uchovu wa safari yako, ule na mayai kabisa, halafu njoo hapa nikuonyeshe kazi! Nilicheka sikuwa na mbavu!
 
Siku izi ukirusha ngumi. Wanakupiga chupa ya kichwa. Ndio maana watu wamekuwa wastaarabu. Au unapigwa spana ya mdomoni lazima meno yatoke. Na ndio maana mtaani ukipata mdaa ukapita unakutana na vijana wengi awana meno iyo ni spana ya mdomo. Maeneo mengi vijana wamepoteza meno
 
The world is driven by brains. We piga pushup komaza ngumi, bonge mimi na Beretta mkononi can squash your brains 50 feet away. Without moving an inch.

Hata vita sikuhizi zinapigwa through presses of buttons.
 
kupigana zamani ilikuwa order of the day .....sasa hao machoko wangetoka wapi??? hata wale waliokuwa na nguvu waliunda UMOJA wa kusaidiana kama watoto wa mbwa mwitu ....ukimpiga mmoja wanakuja wote kuchangia ....hadi na viwembe
 
siku hz mbabe ni mwenye PESA ndo maana watu wapo bize kusaka PESA....
 
Enzi hizo mbabe wa kijiji/mtaa anajulikana kabisa, na watu walikuwa na maeneo ya kupogia matizi ya ngumi, ukipigwa sio rahisi kwenda kushitaki mambo yanaisha kibabe tu, ni mkono kwa kwenda mbele
 
Dah zama hizo nipo Dar, mgulani primary, kuna akina Wamensa (Shimo la udogo), Juma (Keko machungwa), Selemani (Keko mwanga) acha wale wa Temeke na Kurasini! hapo enzi za matumizi ya CHENI ile ya Bruce Lee!Zama hizi watu hawashibi, huko kupigana utaanzaje kufikiria?
 
Nilikua nikikupiga ngumi utahisi ni ndoo ya zege imekudondokea.........acha kabisa

Hahahaha. Kumbe wewe mtu hatari sana......hata Muhamad Ali hakuwa na ngumi nzito kiasi hicho!
Nilikuwa nakuona mpoleee, ila sasa nikikuona nabadili njia...!
 
Nakumbuka miaka ya 80-90 ilikuwa jambo la kawaida kukuta jamaa wanapigana mitaani halafu watu wanashangilia sana.

Yaani ukiwa mtemi au gangwe basi unaonekana wa maana sana. Hata baadhi ya disco ilikuwa lazima ziishe kwa ngumi.

Kwa wale wa Iringa mtawakumbuka kina cool 9, shedadi, Ray nk
Kumbuka ukiwa mdogo rika yako ni ya wale vijana wagomvi hata hivyo bado kupigana kupo ila wewe tu ndio umekuwa mkubwa na unapigana na maisha ambapo wadogo zako wanapigana bado
 
Siku izi ukirusha ngumi. Wanakupiga chupa ya kichwa. Ndio maana watu wamekuwa wastaarabu. Au unapigwa spana ya mdomoni lazima meno yatoke. Na ndio maana mtaani ukipata mdaa ukapita unakutana na vijana wengi awana meno iyo ni spana ya mdomo. Maeneo mengi vijana wamepoteza meno
Hahahahaha umenifanya nicheke,
Ahsante.
 
Mleta mada unanikumbusha mbali sana 1981 ama 1982 kama sijakosea kuna dogo flan aliingia anga zangu kijijin huko mbarali kwa kumtongoza mchepuko wangu. Nilitembeza vitasa kijiji kizima kwa madogo wote wenye umri kama wake. Maumiv makal sana niliwakabiz kwa kosa la mtu mmoja. Yan nilikuwa na bwaka nikiibuka 10 ardhin nikizama nikichomoza 20 wengine chali. Nikamchukua dogo mwengine mwembamba hiv nikamtumia kama fimbo kwa kuwacharaza. Ila kwasasa nimejikita zaid kusaka hela uzee nao ndio huo. Ila miaka iyo ya themanini nilikuwa mtemi sana
Heeeeh!
Vituko, mtu kawa fimbo,
Hahahaha itakua unasema movies za bruce lee.
 
Nakumbuka miaka ya 80-90 ilikuwa jambo la kawaida kukuta jamaa wanapigana mitaani halafu watu wanashangilia sana.

Yaani ukiwa mtemi au gangwe basi unaonekana wa maana sana. Hata baadhi ya disco ilikuwa lazima ziishe kwa ngumi.

Kwa wale wa Iringa mtawakumbuka kina cool 9, shedadi, Ray nk
Dah umenikumbusha Mfike Mapugilo (Fike kwa sasa) alikuwa mtemi wa soko matola Mbeya, sijui yupo wapi huyu jamaa. Ilikuwa burudani tosha
 
Hahahaha. Kumbe wewe mtu hatari sana......hata Muhamad Ali hakuwa na ngumi nzito kiasi hicho!
Nilikuwa nakuona mpoleee, ila sasa nikikuona nabadili njia...!

Napiga jamani........shetani anaogopa.........
 
Back
Top Bottom