Hivi ni kweli kuna maisha baada ya kifo?

Hivi ni kweli kuna maisha baada ya kifo?

Sasa utakua upande upi endapo dini itakinzana na sayansi, kwa mfano ishu ya flat earth na jua kuzunguka dunia
Mimi sio Astronaute. Mambo ya flat earth ama jua kulizunguka jua huwa sifuatilii kabisa. Hapa nimefuatilia kwa sababu mimi ni mwanasayansi ya mwili wa mwanadamu. Tukiwa chumba cha upasuaji tukiwabadilishia watu figo,Ini na after unaona mgonjwa karecover. Unasema Asante sayansi. Ukiwa na mgonjwa wa Covid ambae alikuwa tubed. Siku mnaondoa tube na mgonjwa anaweza kupumua mwenyewe mnasema Yes. Kuna wakati mwingine mnafail mgonjwa anafariki dunia. Lakini mnakuwa mmejaribu kila njia kuokoa maisha.
 
Nikwasababu kuna neno "vimejitosheleza" lililotangulia kabla ya hilo neno nililoandika mimi

Nikuulize wewe, neno "vimejitosheleza" unalifafanua vipi?
Jibu maswali niliyo kuuliza.
 
hapo ninachoona mimi ni ngumu mtu kuamini imani ya mtu mwengine mifano hai ipo mpaka leo wakristu na waislam kila mmoja anambeza mwenzake kwa kile anachoamini au hata kwa wakristu wenyewe kila mmoja ana iman yake na kila mmoja anaona imani yake ni bora kuliko ya mwenzake cha ajabu sasa wote hawa wanapingana lakin mwisho wa siku wote wanaamini katika kitu kimoja Mungu
Wasomi kama nyie mnaoamini miujiza ndio mnaifanya afrika igande.. mungu unayemtaja anayejua yote ndio huyu alikua anahamasisha utumwa na biashara ya utumwa?
 
Kwa Mimi naamini kila binadamu ni kwa kiasi Fulani anaamini kuwepo kwa Mungu hata kama atakataa(kitendo Cha kukubali au kukataa ni ishara tosha za uwepo wa super natural power) ila..
Tofauti ipo katika hizo Sheria zinazoitwa ni za Mungu hapa naamini kwa kiasi kikubwa ni binadamu wachache walizitunga alafu kuwaaminisha watu wote wazifuate ati ni amri za Mungu. Ukizichunguza kwa undani utaona Kuna baadhi ya Sheria zina madhaifu makubwa kama Sheria hizi ambazo sisi wanaadamu tumezitunga.
Ki msingi sisi wenyewe ndio tunaojiamulia maisha, hakuna Sheria iitwayo ya Mungu isipokuwa tunayo mamlaka sisi binadamu ya kutunga Sheria zetu Ili kulinda hadhi ya binadamu na mazingira yake.
mimi naamini in law of physics, evolution and natural selection
 
Mimi sio Astronaute. Mambo ya flat earth ama jua kulizunguka jua huwa sifuatilii kabisa. Hapa nimefuatilia kwa sababu mimi ni mwanasayansi ya mwili wa mwanadamu. Tukiwa chumba cha upasuaji tukiwabadilishia watu figo,Ini na after unaona mgonjwa karecover. Unasema Asante sayansi. Ukiwa na mgonjwa wa Covid ambae alikuwa tubed. Siku mnaondoa tube na mgonjwa anaweza kupumua mwenyewe mnasema Yes. Kuna wakati mwingine mnafail mgonjwa anafariki dunia. Lakini mnakuwa mmejaribu kila njia kuokoa maisha.
Madr kama nyinyi hakawii kushawishi watu waende kwa mganga[emoji2357][emoji2357][emoji2357][emoji2357] we unajua mwili wa binadamu unavyofanya kazi halafu unatupia neno msaada wa mungu
 
Mimi sio Astronaute. Mambo ya flat earth ama jua kulizunguka jua huwa sifuatilii kabisa. Hapa nimefuatilia kwa sababu mimi ni mwanasayansi ya mwili wa mwanadamu. Tukiwa chumba cha upasuaji tukiwabadilishia watu figo,Ini na after unaona mgonjwa karecover. Unasema Asante sayansi. Ukiwa na mgonjwa wa Covid ambae alikuwa tubed. Siku mnaondoa tube na mgonjwa anaweza kupumua mwenyewe mnasema Yes. Kuna wakati mwingine mnafail mgonjwa anafariki dunia. Lakini mnakuwa mmejaribu kila njia kuokoa maisha.
Umeandika kwamba wanasayansi "Kuna wakati mwingine mnafail mgonjwa anafariki dunia. Lakini mnakuwa mmejaribu kila njia kuokoa maisha".
Sasa je, hayo maisha mlioshindwa kuokoa baada ya mgonjwa kufariki dunia yalitoka wapi na yanaenda wapi?
 
Tunapigana kamba tu mkuu!.. wenye akili wanacheza na bongo zetu wanatufanyia vurugu ili tusile raha hapa duniani!. Just imagine unaenda eti kutubu kwa padri ukiamini yeye ni mtakatifu wakati hujui matendo yake!, serious kama unaakili huwezi fanya hivi am telling you.

Hakuna Cha pepo hakuna cha moto isipokuwa ukienda kinyume na nature laws mazingira yatakuadhibu hapahapa hakuna kusubiri.
Unashindwa kwenda kutubu kwani padre msimamia kitubio ndio mliegombania demu jana yake.
 
Ukifa hujui Kama unekufa una-transform na kuingia katika ulimwengu mwingine.

Uhakika ni kuwa Maisha baada ya kifo yapo Ila yapoje hakuna ajuaye.

Ni ishu ya ku-transformation
Total contradiction! yapo lakini hakuna ajuaye yapoje! Taarifa ya uwepo unao uthibitisho zaidi ya simulizi za bible? Unaweza thibitisha kisayansi?
 
Umeandika kwamba wanasayansi "Kuna wakati mwingine mnafail mgonjwa anafariki dunia. Lakini mnakuwa mmejaribu kila njia kuokoa maisha".
Sasa je, hayo maisha mlioshindwa kuokoa baada ya mgonjwa kufariki dunia yalitoka wapi na yanaenda wapi?
Hiyo ndiyo inaonyesha kuwa uwezo kwa mwanadamu una limit. Ila tena jiulize Yes tumekubali kuna limit. Na ndiyo maisha ya mwanadamu ya mwisho na mwisho ni kufa. Mtu akifa ndo kafa baada ya hapo ni decomposition.
 
Nilifanya surgery miezi miwili iliyopita, niliwekewa general anesthesia (ganzi ya kulala kabisa).

Niseme tu, mimi sikuwa na Imani na mambo ya nafsi, roho, dimensions zingine n.k ingawa nilikuwa open to proof and understanding, Lakini toka nimeamka kutoka kwenye ile surgery, ni kama nimeamka hivi, ni kama nimezinduka, nahisi Kuna ukweli fulani ambao siujui/hatuujui juu ya haya maisha, a certain reality beyond what we see. Probably waliotuletea hizi dini walikuwa wamejaribu Kwa uwezo wao kuelezea ukweli huo.

Ilikuwa kidogo nianzishe thread niulizie experiences za watu waliowahi kuwekewa ganzi na kulala kabisa. Nikasema sitaki negativity, nitatafuta ukweli taratibu.

Nimejaribu ku google experiences za watu, sijaona yeyote aliyeandika ku experience nilicho experience. Apparently wote walilala tu na hawana kumbukumbu yeyote.

Nikawaza labda nilikuwa naota nikawa nakumbuka ndoto. Lakini ndoto ni tofauti, ukiamka unajua kabisa ulikuwa unaota. Nomatter how real the dream felt you'll still know that it was just a dream!

What I experienced was different! I was somewhere else! Very aware! The real me was there, not an imaginary me! Na kwanza sijawahi kuota chochote Cha namna ile. Nikawa nawaza kabisa nikiwa kule Is this real life? Yani hata ile wakati naanza kuzinduka na kurudi kulala, ilikuwa ni kama I'm jumping into this world then jumping right back into the other. And I was very aware of both. Like yes niko hapa nimelala nafanyiwa surgery, lakini huku kwingine ni wapi!! Mbona mauzauza!

Tangu nimeamka all I could think of was that experience. Where was I?? Nikawa na shauku kweli nije nimwambie daktari, sema alinitoa confidence maana nilimuanzia mbali, nilimwambia Kuna scenario fulani ikitokea kwenye theater akakataa haikutokea wakati yeye mwenyewe hakuwepo wakati inatokea.

Nikaona nikimwambia na hayo mengine ataniabia nilikuwa naota, and sitaki kabisa mtu adismiss nilicho experience kirejareja...

Yani mpaka nikawa na hamu nifanyiwe surgery nyingine niwekewe ile anaesthesia nione kama nitarudi kule. Nikawaza au ile ganzi ilinilevya kama madawa ya kulevya? Labda wanaovuta madawa ndo huwa Wana experience nilicho experience!! Manake niliwahi kusikia wanaovuta wanakuwa wanaona mauzauza.

Sema huwa sipati muda kukaa mwenyewe most of the times, lakini siku nilikaa kimya peke yangu nikawa nimekodolea macho mmea fulani and honestly zile pattern za majani ni kama pattern za kule nilikokuwa, the awkward patterns and the motions were coming back to me.

Coz where I was was just a world of awkward patterns and very very fast motions and awkward distant shadowy figures and awkward sounds (I could describe the sounds as the sounds you hear ukiwa ndani ya maji). Jumlisha na feeling of helplessness like I want to move but I can't, but I'm just sliding!!!

Inshort, nimeanza kuamini there's more to the human consciousness than just "ukifa haupo tena!" Manake kama wanategemea ukiwekewa ganzi uwe "umekufa Kwa muda", me nilikuwa sijafa bwana I was very aware.

* Bila kusahau surgery yenyewe ilimchukua kama lisaa hivi, lakini ile nimedumbukia kwenye ulimwengu huo Hadi nimeanza kuzinduka ilikuwa kama sekunde chache tu!! Like 30 seconds!!

Someone tag a doctor for me.
 
Hiyo ndiyo inaonyesha kuwa uwezo kwa mwanadamu una limit. Ila tena jiulize Yes tumekubali kuna limit. Na ndiyo maisha ya mwanadamu ya mwisho na mwisho ni kufa. Mtu akifa ndo kafa baada ya hapo ni decomposition.
Kaka neno Mungu ni nadharia pana sana unajua watu wengi wanaamini Mungu kama mtu flani hivi mwenye macho n.k as(as the bible refers) lakini si lazima Mungu awe mfano wa binadamu ila yaweza kuwa Mungu ni jambo jingine kabisa. Wapo wanaoamini Mungu ni Sub Atomic particles etc etc.
Turejee kwenye mada, ushahidi si lazima uwe wa physical bali hata nathari na athari ya mazingira unaweza kuwa ushahidi tosha. Kukosekana kwa ushahidi physical haifanyi kuwa jambo flani ati kuwa ni batili au halipo. Katika kutathmini hii dhana ya maisha baada ya kifo inaweza kujadiliwa katika misingi mikuu miwili Ili kubashiri maisha baada ya kifo yaani probability. Misingi hii ni uwepo wa maisha kabla ya kiumbe kutokea (hapa tutamzungumzia zaidi binadamu), na maisha baada ya kiumbe kutokea.
Unajua kabla ya kuwepo kwa binadamu zipo processes flani zilitokea na kusababisha uwepo wa hii Dunia ambayo ni favourable kwa kutokea kwa uhai (refer to the Big Bang theory).
Jambo hili la kuzuka kwa Dunia mpya si jambo la muhali wala ukiwa yani kwamba limetokea tu kwa bahati mbaya bali ni hatua kadha wa kadha zimefanyika ili kuyaumba maisha. Dunia ndio sehemu rasmi iliyochaguliwa kwa viumbe kuishi na wala sio Mars wala Jupiter (japo elimu yetu inaweza kutufanya tukaishi huko)
Hii ni ishara ya mwanzo kabisa. Msingi wa pili ni ule wa nadharia ya Darwin aka Darwinism theory ya kuwa binadamu hajatokea from nowhere rather ni stages mbalimbali ambazo viumbe vimezipitia mpaka kuwepo kwa hivi viumbe vya leo.
Natamani kuandika kwa urefu zaidi ila nimalizie tu kwa Conclusion ya kuwa hizi ni nadharia na kama ni hivyo suala la kuwepo au kutokuwepo kwa maisha baada ya kifo ni bahati nasibu. Sote twaweza kuwa sahihi na ndio maana tukaita Imani. Yani kuipa uhakika na uyakini wa jambo flani lipo hata kama hulioni kwa macho. Tunaweza kubishana sana na kupingana ila niamini kila mtu yupo sahihi, ila nikushauri tu mkuu usikubali kuamini au kukataa jambo ati kwa kuwa hulioni au hujalithibitisha kwa macho. Yapo mambo flani flani ambayo tunakubali kuwa yapo bila ya ushahidi wowote ule wa kisayansi kwa kuwa Bado Bado elimu yetu haijafanikiwa kuyajadili au kuyatolea hoja.
 
Hiyo ndiyo inaonyesha kuwa uwezo kwa mwanadamu una limit. Ila tena jiulize Yes tumekubali kuna limit. Na ndiyo maisha ya mwanadamu ya mwisho na mwisho ni kufa. Mtu akifa ndo kafa baada ya hapo ni decomposition.
Nakubaliana na wewe kwamba mwanadamu ana ukomo (limit) wake wa kufahamu mambo fulani. Hata hivyo, ukomo wetu usihalalishe kuwa hakuna maisha baada ya kifo.

Mimi naamini kuna maisha baada ya kifo kwa sabababu hatujashudia yakioza (decompose) kabirini kama uozavyo mwili wa mfu.

Kumbuka; mtu akifa tunasema amepoteza maisha yake. Maisha yake yamepotea, yameutoroka mwili wa marehemu.
Kitu kinapotea haimabishi hakiwezi kupatikana sehemu nyingine.
 
Nakubaliana na wewe kwamba mwanadamu ana ukomo (limit) wake wa kufahamu mambo fulani. Hata hivyo, ukomo wetu usihalalishe kuwa hakuna maisha baada ya kifo.

Mimi naamini kuna maisha baada ya kifo kwa sabababu hatujashudia yakioza (decompose) kabirini kama uozavyo mwili wa mfu.

Kumbuka; mtu akifa tunasema amepoteza maisha yake. Maisha yake yamepotea, yameutoroka mwili wa marehemu.
Kitu kinapotea haimabishi hakiwezi kupatikana sehemu nyingine.
Mwili unaoza bwana. Kwanza maiti ikikaa muda mrefu bila treatement inaoza na kunuka mpaka funza wanatoka. Watu waliozikwa makaburi yakifukiliwa itakutwa mifupa tu na baadae mifupa huoza na kujimix kwenye udongo.
 
Maisha baada ya kifo yapona yataendelea kuwepo. Ndiyo, ukifa utazaliwa chura au nyoka au kiumbe chochote na hata mmea. Napo utakufa na kuzaliwa kiumbe mingine tena ndio maana wakasema maisha ni mzunguko!
Habari wanazengo,

Leo ningependa kufahamu au kujua kile unachoamini wewe kama wewe tulivyoumbwa kila mmoja amepewa utashi ukiwa na lengo la kupambanua mambo, tuachane kwanza na hizi imani ambazo tunazoamini au kuaminishwa.

Hivi ulishawahi kujiuliza baada ya kufa nini kinaendelea, kuna maisha baada ya kufa au ndiyo ukifa umekufa mazima!
 
Maisha baada ya kifo yapona yataendelea kuwepo. Ndiyo, ukifa utazaliwa chura au nyoka au kiumbe chochote na hata mmea. Napo utakufa na kuzaliwa kiumbe mingine tena ndio maana wakasema maisha ni mzunguko!
[emoji848][emoji848]
 
Ndo unavyojiliwaza hivyo au siyo....Lakini unasahau kabisa kwamba kabla ya hapo wewe HUKUWEPO na HUKUJULIKANA KABISA KAMA UTAKUWEPO ghafla ulishtukia tu UPO na UKAWEPO BILA RIDHAA YAKO,hivi huyo aliyekufanya UWEPO akakutengenezea hizo system za kustaajabisha na zinazoshangaza kama hzo na tena kama ulivyosema zinafanya kazi kwa kushirikiana bila kukosea,na baadhi huwa zinafanya kazi bila ridhaa yako ikiwemo MOYO au MFUMO WA MMENG'ENYO WA CHAKULA MWILINI,yan kazi yote hiyo kubwa aliyoifanya awe basi tu amekuleta tu duniani hapa kuja kucheza cheza tu kupoteza muda kisha ufe akuzime tu kama taa usiwake tena? Kwa thamani yote hiyo ya hzo syatems ulizozitaja ipitee kizembe zembe tu ufe tu kama mzoga iwe imeisha eti asikurudishe tena? Kirahisi rahisi tu....Umeishi muda flan hv kisha huyo Mtengenezaji hizo SYSTEMS akaamua kuzi SHOOT DOWN(kufa) bila wewe kupenda,Hivi HUYO kwa ujuzi mkubwa wa kushangaza kama hivyo ashindwe kweli KUKUWASHA (kuhuisha)ILI UWAKE TENA KWA MFUMO MWINGINE bila ridhaa yako?
Kipi kigumu,KUTENGENEZA KISICHOWAHI KUWEPO au kutengeneza KILICHOWAHI KUWEPO?

Kumbuka wewe ulikuwa HAUPO KABISA na hakuna mtu alikuwa anakutaja,umekuja Duniani kupitia STAREHE walioifanya watu wawili kitandani kati ya mwanamke na mwanaume ambapo wewe ndo unawaita baba mwingine unamwita mama.
Starehe hiyo waliifanya lakin pia walikuwa hawajapanga kabisa na hawajui ndo unakuja wewe...NA HUENDA HATA SIKU ILE MIMBA YAKO INATUNGWA KUNA MMOJA KATI YAO HAKUZIPOKEA VIZURI TAARIFA YA MIMBA YA WEWE KUTUNGWA LKN PIA HUENDA WALILAUMIANA KWANINI WEWE UMETUNGWA ILA KWA VILE NI MPANGO WA MUNGU NA SIO RIDHAA YAO NAO WAKAAMUA TU KUPOTEZEA MAANA HAKUNA JINSI, MAMA AKAKUBALI KULEA MIMBA YAKO KWA SHIDA AFU NDO UKAJA WEWE LEO AMBAYE SASA HV UPO hapa JF na simu yako UNASEMA HAKUNA KUFA NA HUYO MUNGU HAYUPO.
Hivi HUYO aliyefanya yote haya bila ridhaa ya wewe na wazazi hivi ukishakufa ashindwe kweli KUKUHUISHA tena wewe ambaye ulikuwa HAUPO KABISA?

Umekuja huku ukiwa dhaifu wa mwili na akili unajinyea,unakojoa popote tu unatoka udenda muda wote,lakini BILA RIDHAA YAKO tena unakuwa mtu mzima unafanya mabalaa ya kuyafanya,unaiba,unazini, unatukana watu,unadhurumu KWA RIDHAA YAKO mwisho YULE YULE alikuekuleta Anakuzima tena BILA RIDHAA YAKO (unakufa),Hivi huyu MUNGU ashindwe kabisa kukufanya uwe hai tena?

Kipi kigumu,KUUMBA KISICHOKUWEPO au KUUMBA KILICHOWAHI KUWEPO?

Unakufa bila ridhaa yako na kisha anakupeleka kulee wasiporudi lakini kufa kwako huko lengo ni wewe kubadili hali kutoka uhai wa Dunia kwenda uhai wa akhera,huko utaambiwa yote yote uliyowahi kuyafanya kwa sababu sasahv kila unachokifanya kipo RECORDED kuanzia unabalekhe/vunja ungo mpk siku ile UNAZIMWA na kisha akutie motoni kwa mabaya au akutie peponi kwa mazuri uliyofanya,Huyu ndo akuache tu ufe afu iwe ndyo basi?

Tuache kujitoa akili ndugu zangu,Hzo akili ulizopewa angepewa hata mbuzi lakini Muumbaji ameamua akupe wewe binadamu,lakini pia ukumbuke huyo aliyekuleta hajakuleta tu hivihivi amekuleta kwa mpango maalum na uje utii sheria zake na ufuate kile alichokuamuru ufanye kwa kutumia mfumo sahihi ambao ni dini SAHIHI,dini ya mitume wote walioletwa na Mungu muumbaji.

Duniani Hujaletwa kuja kupoteza muda na hapa duniani sio mahali pa kuishi alipopanga Mungu,na hata hzo organs hujapewa tu burbure,hzo organs running hours zipo limited na matendo unayoyafanya yote yapo in records.
Dunia ni sehemu ya kufanya Utii ili atakaefanya vzr huo utii basi kuna mahali Mungu ndo ameandaa maisha yasiyoisha.

Hebu jiulize kitu kimoja,kama hii dunia ni sehemu ya kuishi kwanini watu wanakufa,kwanini watu wanakufa katika umri wa uchanga,utoto,ujana na utu uzima?
Kama dunia ni kutafuta maisha kwanini wengine hawayapati,wanaishi kwa shida lakini mbona ukiyapatia hayo maisha pia unakufa?Kwanini ufe?mbona starehe zote duniani ni za kipindi flan tu hv,mbona majonzi.ndo mengi kuliko furaha?

Kikubwa unachotakiwa kuzingatia ni kwamba YUPO ALIYEKUANZISHA NA KUKULETA DUNIANI KWA MUDA bila ridhaa yako ILI UJE UFANYE MITIHANI (MAJARIBU)ufanye UTII kwa ridhaa yako mwenyewe huku kufanya utii Mungu ametoa maelekezo tafuta uysome na uyafuate ili uanze kutii,

Amekupa nyenzo za wewe kufaulu huo utii na kuishinda hiyo mitihani,amekupa Muongozo wa vitabu kwa zamani (Zaburi,Torati,Injili) na sasa ni QURAN,pia akakupa Akili,kusikia,kuona,kunusa,kuonja nk,anakupa muda flani,baada ya muda huo flan HUYO HUYO ATAKUFISHA bila ridhaa yako tena NA ATAKURUDISHA TENA KTK UHAI WA AINA NYINGINE bila ridhaa yako ....Ni vile vile kama kwenye chumba cha mtihani,unapewa kila kitu cha kufanyia mtihani ikiwemo na Muda,ukiskia msimamizi anasema "PENS DOWN" huko ndiyo KUFA kwamba muda umeisha,na muda unaisha bila ridhaa yako tena,kisha sasa ndo sote tutakutana huko kwenye SIKU YA HUKUMU,siku ambayo kila mtu atabeba alichokipanda kwenye uhai wa Duniani.

Wakati wewe unandelea kuuchezea muda lakini ipo siku na wewe kule mbinguni patasemwa kwa ajili yako "Pens down" .....hapo utapangiwa ratiba na watu kwamba wakakufukie wapi na lini tena wakati huo wewe upo kwingine kabisa unapambana na hali yako huko.

Hzi pumzi zisituhadae ndg zangu,hakuna watu wanaoendelea kujilaumu hivi sasa kama wale marehemu wetu tuliowazika,Mtu mwema kwa mazuri anayoyaona huko saizi anajilaumu kwanini amefanya mema machache,na mtu mbaya ndo analia na kusaga meno kumuomba Mungu awarudishe kidoogo warudi Duniani kuja kusawazisha yale yote waliyokosea jambo ambalo abadani haliwezekani.
Mkuu komenti yako nimei-secreenshoot, ili nijikumbushe pale ninaposahau

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwili unaoza bwana. Kwanza maiti ikikaa muda mrefu bila treatement inaoza na kunuka mpaka funza wanatoka. Watu waliozikwa makaburi yakifukiliwa itakutwa mifupa tu na baadae mifupa huoza na kujimix kwenye udongo.
Hujanielewa. Sijaandika kwamba mwili hauozi, la hasha.

Nimeandika kuwa mwili uliopoteza maisha ndiyo huzikwa na huoza kaburini. Maisha yaliyopotea hayazikwi kaburini. Yamkini yapo mahali fulani pasipojulikana.

Maisha na mwili ni vitu viwili tofauti. Maisha yakitoweka, mwili huoza. Maisha hupokewa kabla ya mwili kuoza.

Kwa hiyo maisha yapo baada ya kifo.
 
Hujanielewa. Sijaandika kwamba mwili hauozi, la hasha.

Nimeandika kuwa mwili uliopoteza maisha ndiyo huzikwa na huoza kaburini. Maisha yaliyopotea hayazikwi kaburini. Yamkini yapo mahali fulani pasipojulikana.

Maisha na mwili ni vitu viwili tofauti. Maisha yakitoweka, mwili huoza. Maisha hupokewa kabla ya mwili kuoza.

Kwa hiyo maisha yapo baada ya kifo.
[emoji848][emoji848]
 
Back
Top Bottom