Elimu ya darasani na namna inavyombadilisha mhusika hi vitu viwili tofauti. Ni kweli kuwa elimu husaidia kwa asilimia kubwa sana kumfanya mtu awe na mabadiliko chanya na hasi kwa uchache.
Hoja ambayo sana inatawala ni mtu kuwa na elimu halafu anakuwa sawa na asiye na elimu kama hiyo ktk MAWAZO, MATENDO, MAFANIKIO, BUSARA, UPEMBUZI, UJUZI n.k na hata kufikia sisi kusema AMESOMA ILA ELIMU YAKE HAIJAMSAIDIA.
MFANO:
1. kijana aliyemaliza chuo kikuu kuandika C.V ama barua ya kuomha ajira ni kazi
2. Form six ama hata chuo kikuu kuongea lugha ya kikoloni kwa tabu (zama za wazee wetu lugha ilikuwa kigezo na sense of pride)
3. Kijana wa chuo kikuu atokaye familia maskini na apataye mkopo, huyu hasaidii nyumbani kwao ni kuishia Club, wanawake, mashugadadi, pombe na kununua vifaa vya ki elekroniki vya gharama ( smartphones, flat screens, sub woofers etc) wakati wazee wetu enzi wanasoma ilikuwa kukumbuka nyumbani ni first priority
4. Kijana aliyemaliza degree yake (uchumi, sheria, umakanika, umeme, udaktari,) pale apatapo kazi hajui chochote ktk kazi husika ama anajua kwa sehem ndogo sana ukilinganisha na walio chini yake kielimu, anaanza kuelekezwa na CERTIFICATE HOLDER ama DIPLOMA HOLDER..... ilhali huyu alokuja ana elimu kuwazidi waliopo.
Hiyo ni baadhi ya mifano inayoleta kubezwa kwa wenzetu WASOMI