Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kwani hujui kuwa hulka ya binadamu yeyote, anataka kwenye society aonekane yuko kwenye status ya matawi ya juu.
Hebu nikuulize swali moja tu, hivi yule mheshimiwa sana, ambaye hivi sasa yupo kwenye mjengo pale Dodoma, akihudhuria bunge maalum la katiba, ambaye ni mbunge kwa tiketi ya magamba, toka mkoani Tanga, ambaye anaitwa Profesa maji ya kina kirefu, siyo tu tujiulize kama ana Philosophy of Doctorate, bali tujiulize pia hivi kweli, hata hiyo standard seven au eight, alimaliza kweli?!
Wengi wenye midomoo mirefu ndo standard saba sasa kama ujui! Na humu wengi wanatafisri english kama degree! Hawajui wengine tumesomea ugriki nondo tele ila english shida.
Usisahau
Dr. Mengi.
Dr. Mrema.
Dr. Geo Davie Mkuu wa Manabii.
Dr. Manyaunyau.
Dr. Presdent.
Dr. Mama mchungaji Rwa....
Dr. Nape Nauye.
Dr. Ndodi.
Dr. Mchunguzi Huru [phd]
Dr....
Lile kubwa jinga la yule mzee anayegongewa mkewe yule mpare lina degree tatu. Moja ya kivulia kambale.
Shalom wakuu!
Swali hili limekuwa likinitatiza sana tangu miaka 2 iliyopita tangu nilipojiunga na JF,
imekuwa ni kama fashion kwa wanaJF wengi kudeclare elimu zao katika post zao nyingi, ajabu kila mtu anasema sijui alipokuwa chuo mwaka wa pili, mwingine ooh nimejiajiri lakini nina degree yangu, hivi ni kweli wote tumesoma mpaka level hizo? Hakuna hata mwenye diploma au Form4 kabisa? Mbaya zaidi hadi vijana wa BRN wa humu JF naona wameanza taratibu kurithi haka karoho ka kipepo kanakotokana na kutojikubali.
Tubadilike jamani.
mimi sijui kusoma wala kuandika
Sababu wenye degree watakuwa ni form four na six pia, au diploma! !!!
So hizo ni subsets, yaani usitafute sukari wakati unakunywa chai, imo humo tayari huwezi iona tena!!!!!
Ndugu yangu yaani ya humu ndani ukiyafuatilia, utachoka. Yaani;
-Hakuna mwenye vitz, wote wana v8
-Humu JF wote wanapiga bao 5 na kuendelea, sasa haya mabango ya kuongeza nguvu za kiume ni ya akina nani? Labda wana JF hawahusiki!
-Humu wote wapo dsm, wa Mkiu hayumo humu.
-Humu Jf kila mtu amewahi kupanda ndege au amepanda ndege muda huu.
-Mwenye KIBAMIA humu hayumo, humu kila mtu ana Tangopori tu. Chezea JF weyee!
-Humu watu tunajua kila kitu, mpaka dawa ya ebola imo humu.
-halafu kinginee, hakuna mla mihogo hata mmoja humu wakati kila siku tunapanga foleni kwa mama Cha Upepo.
JF iache kama ilivyo.