Hivi ni kweli maziwa huharibu dawa?


Nadhani yule mchangiaji aliyesema kuna kosa yeye amezoea ile regimen iliyopo kwenye HELIGO KIT ambayo ni Lansoprazole+ Tinidazole+Clarithromycin. but hata hiyo ya Omeprazole+ Metronidazole+ Amoxycillin or Erythromycin might be used as well.
 
naona mushaingia darasani kwenu muhimbili munatiririsha majibu ya mitihani...ila musisahau sie ni wananchi ea kawaida munayoongea ni mbali na mageni sawa na mbingu na ardhi...ongeeni lugha nyepes tuwaelewe kwa uzuri
 
Duh nimejifunza mengi wakuu.Ahsanteni watoa ushauri na mleta mada.
 
kuna mzee mmoja alinambiaga eti unaeza kunywa bia na dawa zote na ukawa poa. Ila ukinywa flagyl na bia kaa karib na jeneza. Hii story ina ukwel wakuu?
 
kuna mzee mmoja alinambiaga eti unaeza kunywa bia na dawa zote na ukawa poa. Ila ukinywa flagyl na bia kaa karib na jeneza. Hii story ina ukwel wakuu?

Sijui nitumie lugha gani rahisi ili tuelewane maana hapa ni pure pharmacology. Lakini ina nut shell si kwamba kila dawa ukinywa na pombe utakuwa ila kwa hizo nitro imidazole kama metronidazole, tinidazole secnidazole na nyingine it's obvious utapata disulfiram like effect ambayo ni worse ni inaweza kuwa life threatening.
Kwa kifupi dawa ukinywa huwa zina hatua nne kwenye mwili wa mwandamu ambapo ni 1. Absorption (unyonywaji)
2. Distribution (usambazaji)
3. Metabolism(kuichakata dawa )
4. Excretion( utolewaji)
Kuna enzymes ambazo huwa zipo kwenye ini zinahusika kufanya kazi ya metabolism ili kiasi fulani cha dawa kitu mike mwilini na Mabaki ya toke kwa njia ya jasho, mkojo, haja kubwa n.k
Moja ya enzymes hizo kuna kitu kunaitwa Cytochrome P 450 ambayo hutumika kwenye metabolism ya dawa nyingi pamoja na chakula. Na kwa kuwa enzyme huwa zinafanya kazi katika mfumo wa kama kufuri na funguo mara nyingi unakuta kuna kuwa na competition kati ya enzymes na substrate.
Hapa substrates kwetu n dawa husika pamoja na pombe. Zote zinakuwa zinataka kutumia hiyo CYP P450 ili kuwa metabolised. Sasa kunachotokea mara nyingi pombe inakuwa mshindi na kuacha dawa bila kuwa metabolised hivyo kufanya kuwa toxic mwilini .Hivyo basi toxicity inasabishwa na hiyo bio - accumulation. Nimejaribu tu kugusa gusa maana kwa undani wake ni somo refu.
Lakini kwa kifupi ni kwamba USIUMIE POMBE wakati umekunywa dawa. Sio lazima ufe ila unaweza ku impair metabolism ya sawa. Ahsante sijui kama kidogo nimeeleweka
 
kuna kitabu kinaitwa ifahamu pombe sema nimekwama kwenye distribution . hizi baadhi ya dawa zenye muingiliano na pombe.
[TABLE="class: MsoTableGrid"]
[TR]
[TD] NO[/TD]
[TD="width: 204"] JINA/ KUNDI LA DAWA[/TD]
[TD="width: 144"] MATUMIZI[/TD]
[TD="width: 223"] MADHARA IKITUMIKA NA POMBE[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 44"] 1.[/TD]
[TD="width: 204"] Isoniazid[/TD]
[TD="width: 144"] dawa hii hutumika kutibu kifua kikuu. Mara nyingi hupatikana kwenye mchanganyiko wa dawa nne uuitwao RHZE.[/TD]
[TD="width: 223"] Dawa hii inaongeza uwezekano wa kupata matatizo ya ini. Pia ikitumika na divai kuna uwezekano wa kupanda kwa shinikizo la damu (BP)[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 44"] 2.[/TD]
[TD="width: 204"] Metronidazole/fragyl[/TD]
[TD="width: 144"] dawa hii mara nyingi hutumika kutibu matatizo ya tumbo.[/TD]
[TD="width: 223"] Kuharisha,kichefuchefu, kutapika, maumivu makali ya kichwa, kizunguzungu[/TD]
[/TR]
[/TABLE]

[TABLE="class: MsoTableGrid"]
[TR]
[TD] 3.[/TD]
[TD="width: 204"] asprin[/TD]
[TD="width: 144"] Dawa ya maumivu na kushusha homa[/TD]
[TD="width: 223"] Inaongeza uwezekano wa kupata vidonda vya tumbo.[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 44"] 4.[/TD]
[TD="width: 204"] Chlorpropramide tolbutamide tolazamide[/TD]
[TD="width: 144"] Dawa za kisukari[/TD]
[TD="width: 223"] Kuharisha,kichefuchefu, kutapika, maumivu makali ya kichwa, kizunguzungu[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 44"] 5.[/TD]
[TD="width: 204"] metoclopramide[/TD]
[TD="width: 144"] Dawa ya kichaa na kuzuia kutapika[/TD]
[TD="width: 223"] Inasababisha kulewa zaidi[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 44"] 6.[/TD]
[TD="width: 204"] ketaconazole[/TD]
[TD="width: 144"] Dawa ya kutibu fangasi[/TD]
[TD="width: 223"] Kubabuka ngozi,kutapika na kizunguzungu[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 44"] 7.[/TD]
[TD="width: 204"] Cimetidine ranitidine nizatidine[/TD]
[TD="width: 144"] Dawa za vidonda vya tumbo[/TD]
[TD="width: 223"] Ranitidine na nizatidine Zinaongeza kiasi cha pombe kwenye damu, madhara ya cimetidine kwenye ubongo huongezeka.[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 44"] 8.[/TD]
[TD="width: 204"] doxycycline[/TD]
[TD="width: 144"] Dawa ya kutibu maambukizi .
[/TD]
[TD="width: 223"] Unywaji wa pombe kupita kiasi hupunguza nguvu ya dawa hii. Sio lazima unywaji huu uwe pamoja na dawa.[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 44"] 9.[/TD]
[TD="width: 204"] verapamil[/TD]
[TD="width: 144"] Dawa ya kutibu shinikizo kubwa la damu (BP) na maumivu ya moyo.[/TD]
[TD="width: 223"] Dawa hii huongeza kiasi cha pombe kwenye damu na kuzidisha madhara yake. Pia kuna hatari ya madhara kwenye moyo[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[TABLE="class: MsoTableGrid"]
[TR]
[TD] 11.[/TD]
[TD="width: 204"] Valium (diazepam)[/TD]
[TD="width: 144"] Dawa ya usingizi na kutuliza[/TD]
[TD="width: 223"] Dawa hii huongeza madhara yasababishwayo na pombe.[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 44"] 12.[/TD]
[TD="width: 204"] Ascorbic acid (vitamin C)[/TD]
[TD="width: 144"] Dawa ya kuongeza vitamin C mwilini[/TD]
[TD="width: 223"] Inaongeza utokaji wa pombe mwilini , kusaidia kuona na kuongeza balansi baada ya kutumia pombe.[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
Hizo ni baadhi ya dawa tu lakini haishauriwi kwa mtu anayetumia dawa yeyote kutumia pombe. Hata kama hautapata madhara lakini pombe inaweza kusababisha dawa itoke haraka mwilini na hivyo isiue wadudu au kufanya kazi yake ipasavyo. pia kwa kuandika baadhi ya madhara yanaweza kuonekana ni ya kawaida lakini yanaweza kuwa hatari na kuhatarisha uhai wa mtu. Je ni muda gani mtu anatakiwa asubiri kabla ya kunywa pombe?. ukichukulia dawa ya metronidazole (fragyl), tafiti nyingi zinashauri kusubiri saa 24 (siku moja) au zaidi na wengine wanashauri kutumia pombe baada ya saa 72 yaani siku tatu baada ya kutumia dawa hii. Kwa mtu mwenye afya ya kawaida saa 24 zinatosha kabisa lakini kwa wazee au watu wenye magonjwa mengineyo inashauriwa kusubiri zaidi ya saa 24. Ni vizuri pia ukawasiliana na mtaalamu wa dawa kabla haujatumia pombe iwapo utakuwa umetumia dawa. Yeye anaweza kukupangia muda mzuri wa kusubiri kulingana na hali yako.
 
Jibu ni moja tu, usinywe pombe kwa kuwa ni hatari kwa maisha yako.
 
Hivi huwa ni dawa gani mama mjapesi ashauriwi kumeza eti akimeza anaweza kuzaa kiumbe cha ajabu ebu nijuzeni
 
Hivi huwa ni dawa gani mama mjapesi ashauriwi kumeza eti akimeza anaweza kuzaa kiumbe cha ajabu ebu nijuzeni

Ni dawa nyingi tu mjamzito haruhusiwi hasa katika miezi mitatu ya mimba. Sasa sijui ni katika Kundi gani la dawa unataka kufahamu ila kwa antibiotics. All fluoroquinolones including Ciprofloxacin, Levofloxacin Nalidixic
Acid hazirusiwi
Tetracyclines kama Doxycycline, Etc zingine ni kama chloramphenicol pia hai shauri wi.
Ila Anaweza tumia Penicillins kama Amoxycillin, Benzyl penicillin, benzathine penicillin etc
Cephalosporins kama ceftriaxone, cefalexin etc
Microlides kama Erythromycin

Kwa upande wa dawa za maumivu Paracetamol tu ndio iko recommended. Mjamzito asinywe dawa yeyote bila kumuona mtaalamu kwanza ili kuepuka mimba kutoka au mtoto kuzaliwa na ulemavu. Hii ni kwa ufupi sana.
 
naona mushaingia darasani kwenu muhimbili munatiririsha majibu ya mitihani...ila musisahau sie ni wananchi ea kawaida munayoongea ni mbali na mageni sawa na mbingu na ardhi...ongeeni lugha nyepes tuwaelewe kwa uzuri

Daah!!! kweli wanatiririka lugha ngumu kwetu,ila tunapa elimu na sisi.
 
mimi huwa nachanganya maziwa na pombe value yaani inakua poa sana
 
Mim nlikua najua dawa za.minyoo ndo huruhusiw kunywa maziwa ama kitu cha sukari mpaka baada ya 24 hrs sasa kuhusu dawa zingine naona madoctor wametoka nje ya.mada wanaanza kuzungumzia pombe na dawa.
 
Mim nlikua najua dawa za.minyoo ndo huruhusiw kunywa maziwa ama kitu cha sukari mpaka baada ya 24 hrs sasa kuhusu dawa zingine naona madoctor wametoka nje ya.mada wanaanza kuzungumzia pombe na dawa.

Hatujatoka nje isipokuwa mleta mada ni kweli aliuliza kati ya maziwa na dawa. In the course of discussion kuna mleta mada mwingine akawa anataka kujua kati ya pombe na dawa.
 
Nadhani yule mchangiaji aliyesema kuna kosa yeye amezoea ile regimen iliyopo kwenye HELIGO KIT ambayo ni Lansoprazole+ Tinidazole+Clarithromycin. but hata hiyo ya Omeprazole+ Metronidazole+ Amoxycillin or Erythromycin might be used as well.

Kwanin useme ina BASE kwenye CLARITHROMYCIN , ina maana CLarithromycin umeibeba kichwani hutaki hata ibadilishwe na ndugu ze kama azithromycin , erythromycin , ketomycin.. Even amoxicillin can be used when the patient is not allergic to beta lactam antibiotic. Secnidazole, tinidazole can be used interchangeable with METRONIDAZOLE as well..
 

Ni muda gani sasa naruhusiwa kunywa maziwa baada ya kumeza dawa hzo zisizoruhusu maziwa???
 

Mode of action : so it's inhibit production of acid Ok.. So it must be antiacid don't memorized sir .. PPI are all anti acid ok..
 
Mode of action : so it's inhibit production of acid Ok.. So it must be antiacid don't memorized sir .. PPI are all anti acid ok..
You shouldn't stick on CLARITHROMYCIN sir think bigger any microlide can fit: eg azithromycin , telithromycin , erythromycin or even any antibiotic like amoxicillin can be used as well so the guy was correct ...
I don't understand how the strength of regimen can be lowered in absence of CLARITHROMYCIN
 
Mode of action : so it's inhibit production of acid Ok.. So it must be antiacid don't memorized sir .. PPI are all anti acid ok..
kwenye nomenclature ya dawa kuna sababu mbalimbali kama chemical constituents, clinical use au mode of action. kwa hizi dawa za za kupunguza acid tunaziname kutokana na mode of action..
 
kwenye nomenclature ya dawa kuna sababu mbalimbali kama chemical constituents, clinical use au mode of action. kwa hizi dawa za za kupunguza acid tunaziname kutokana na mode of action..


Ni muda gani sasa naruhusiwa kunywa maziwa baada ya kumeza dawa hzo zisizoruhusu maziwa?
 

unachosema ni sawa kwa kiasi fulani. lakini tunapochagua combination ya dawa tunachagua yenye highest cure rate. among macrolide combination yenye clarithromycin ilionekana ndiyo best. kupitia matokeo ya clinical studies ni muhimu sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…