Melki Wamatukio
JF-Expert Member
- May 3, 2022
- 6,156
- 10,974
Aisee, ni uzembe wa hali ya juu sana. Mamlaka ya hali ya hewa ndiyo taasisi pekee iliyotakiwa kuongezwa nguvu na kuwezeshwa kipesa kwa kuwa ndiyo ambayo hushikilia uhai wa watu na wanyama kwa ujumla.
Inasikitisha sana. Mpaka inafikia hatua Mlima Hanang unaleta madhara makubwa kwa watu na mifugo kiasi hiki, uongozi umetulia tu, na hakuna jitihada zozote zinazofanyika ili kuboresha huduma za utabiri wa hali ya hewa, badala yake unaegeshea nguvu nyingi kuwatafuta Geologists ili wafanye tafiti dhidi ya mawe yaliyotoka Mlimani Hanang kama yanaweza kuwa madini. Inauma sana.
Tuseme kwenye volkano na matetemeko ya ardhi tumeshindwa, kwenye mvua je? Au tutaendelea kudanganyana juu ya ujio wa mvua za El Ninho mpaka lini? Ni heri kinga kuliko tiba. Serikali, egesheeni nguvu kwenye mamlaka za hali ya hewa, boresheni huko. Kama huduma hizo zingelikuwa bora, mngetoa taarifa watu waanze kujikataa mapema kutoka kwenye maeneo hayo hayarishi. Mbona nchi za wenzetu tena ndogondogo kama Rwanda zimeweza? Kwani wao waweze wana nini, na sisi tushindwe tuna nini?
Inauma sana.
Inasikitisha sana. Mpaka inafikia hatua Mlima Hanang unaleta madhara makubwa kwa watu na mifugo kiasi hiki, uongozi umetulia tu, na hakuna jitihada zozote zinazofanyika ili kuboresha huduma za utabiri wa hali ya hewa, badala yake unaegeshea nguvu nyingi kuwatafuta Geologists ili wafanye tafiti dhidi ya mawe yaliyotoka Mlimani Hanang kama yanaweza kuwa madini. Inauma sana.
Tuseme kwenye volkano na matetemeko ya ardhi tumeshindwa, kwenye mvua je? Au tutaendelea kudanganyana juu ya ujio wa mvua za El Ninho mpaka lini? Ni heri kinga kuliko tiba. Serikali, egesheeni nguvu kwenye mamlaka za hali ya hewa, boresheni huko. Kama huduma hizo zingelikuwa bora, mngetoa taarifa watu waanze kujikataa mapema kutoka kwenye maeneo hayo hayarishi. Mbona nchi za wenzetu tena ndogondogo kama Rwanda zimeweza? Kwani wao waweze wana nini, na sisi tushindwe tuna nini?
Inauma sana.