Hivi ni kweli sikukuu za wenzetu Waislamu siku karibu zote huangukia siku ya pili ya matarajio au huwa kuna namna?

Zingekuwa zinaangukia Ijumaa au Jumatatu, ingekuwa poa sana.
 

"Sikukuu zahawa wenzetu"--- kwa hiyo kauli yako unamaanisha uzi huu umeuandika kwa ajili ya wasiokuwa Waisilamu au ??!!
 
By the way,ndio maana yakaitwa maswala ya imani lakini kimantiki hakuna maana yoyote maana majina ya tarehe,siku na miaka ni watu walikaa chini waka invert.
 
Nakumbuka funga ya ramadhani ya mwaka huu,mufti akiwa anatangaza utasikia anasema tumewasiliana na wenzetu wa ukanda huu wanasema mwezi haukuonekana kwaiyo tutaendelea kumalizia siku 30,sasa katika izo nchi anazozitajaga utasikia Kenya,uganda mpaka comoro tumeongea nao wanasema hawakuuona,ila ramadhani ya mwaka huu 2022 mufti alisema tumewasiliana na wenzetu wa Zanzibar wao wanasema hawajauona ila nchi jirani zetu kama kenya na uganda hakuzitaja aliitaja tu Zanzibar,na mwaka huu Kenya na Uganda wamekula eid kabla yetu sasa sijajua kwanini mwaka huu kawakataa ilihali miaka ya nyuma lazima azitaje nchi jirani,
Ila nilichogundua hapa kuna kama kiushindani kwa sie waislamu kila kundi linajiona bora,nakumbuka ramadhani ya mwaka huu shekhe wa mkoa wa Dsm alialikwa kwenye hafla fulani hapa katika maelezo yake alisema kwa kuwauliza wahudhuriaji mnataka ama mnapenda eid tuisheherekee lini wakajibu basi shekhe wa mkoa akasema ilo limepita akajinasibu si mnajua mie ndio katibu wa mwandano kwa bakwata basi ilo limeisha nitafanya ivyo.....Nilishangaa sana yaani mtu anaamua yeye tu kwa maamuzi na cheo chake kutuamrisha nataka iwe siku fulani ambayo anamaslahi nayo na sio kufuata kama maamuzi ya dini yanavyotaka
 
Mapokeo ni kuandama kwa mwezi ambao haundami siku moja dunia nzima
Pia Kuna kuhitlafiana katika tafsiri ya aya Kama ilivyo kwa dini zote, mfano WaHindu billion moja wanatofautiana mara laki tatu japo kwao wote Krishna Ni Supreme Deity

Hivi hawa wahindu Hii Swastika (Nazi symbol) kwao inamaana gani? Niliiona kwenye temple lao pale karibu na DIT.
 
Acha porojo kwa hiyo umeamini yeye ndo anaficha mwezi na ku uonyesha? Tambua kwamba mwezi ni wa Mungu masiku ya shaka angalia mwenyewe mwezi hujaona uliza walio kuzunguka

Acheni kuwasingizia watu vitu vipo nje kabisa ya uwezo wao
 
Msiokuwa waislamu najua hii itawapa shida Sana lkn haina haja kuteseka kwakuwa kuna mambo ambayo waislamu wao wenyewe wanayaelewa vizur Sana.

Dini hii ilikuwa na utaratibu wake wa namna ya kuyaendea maswala mbali mbali yanayohusu Uislamu,kwahiyo kuna kutafuatiana katika tafsir na uelewa wa mambo.

Kuna baadhi ya ibada zinahusisha mwezi na hizi ndizo ambazo huleta utata Kwa wale ambao wanaenda kidijitali lkn wasichofahamu Dini hii ilikamilika toka zamani hakuna tekinolojia ambayo italeta jipya ktk dini, tangu zamani muandamo WA mwezi huangaliwa ktk maeneo husika au kanda husika,Kwa mfano afrika mashariki tunashirikiana,lkn kwakuwa siku hizi kuna mawasiliano basi kuna watu wanahalalisha kuwa mwezi ukiandama Saud Arabia basi wao wanafuata huko,lkn huu sio utaratibu wa kiislamu, sasa utasikia bakwata wanalaumiwa Sana kuwa wanafuata siasa lkn ukweli ni kwamba bakwata wanafuata mafundisho halisi,kwahiyo bakwata haitakosa lawama Kwa mtazamo huu,lkn wote tunamwabudu mungu mmoja haina haja ya kuchafuana,walio Kula Jana Allah awabariki na wa Leo wabarikiwe pia.

Niuwaulize watu wa kidijitali,Kwa kawaida mwanamke akiachwa hukaa kurui tatu EDA Kwa lengo la kujua kama mwanamke aliyeachwa je ana Mimba au laa,sasa Kwa maendeleo ya tekinolojia baada ya mwanamke kuachwa Tu Leo hii unaweza jua kama ana Mimba au laa,je tufute EDA kwakuwa tuna vyombo vya kisasa vya kujua ujauzito WA mwanamke?

Mfano funga ya Arafa, watu hawafungi swaumu yake kwakuwa watu wamesimama Arafa laa! Bali hufunga kutokana na mwandamo WA mwezi husika WA maeneo mbali mbali. Swali Kwa watu wa kidijitali kama watu wanatakiwa kufunga kwasababu ya kusimama watu viwanja vya Arafa,je mtawazungumziaje watu ambao katika dunia hii hii Mda huo ambao watu wamesimama wao wamelala je hawa waislamu wataipataje funga ya Arafa,kimantiki ya kawaida ni Jambo ambalo haliwezekani,tunatakiwa tufuate maswala ya Dini Kwa dalili na sio kurishwa propaganda kuwa bakwata Wana matatizo,hizo ni hoja za wasio kuwa na elimu ya Dini,lkn tuseme Tu kuwa kutofautiana ni rehma, wewe kama unafuata usasa Sawa fuata na kwani mungu wetu sote,na Yule anayefuata dalili ambazo ndio mtazamo WA bakwata waache wafanye hivyo.

Kwa kifupi Bila ya kwenda ndani Sana,msiokuwa waislamu mjue kwamba waislamu wanafuata hoja ambazo zinakubalika kidini,hatufuati hoja ya mtu kuwa aseme Mimi nimetokewa na roho mtakatifu kaniambia moja mbili tatu laa,Uislamu tunafuata data ambazo ndio msingi wa Dini hii Ila bahati mbaya imeingiliwa siku hizi,lkn narudia tena pamoja na hitilafu mbali mbali kuna mambo ya msingi ambayo waislamu wote wanakubaliana na ambayo ndio msingi wa Dini yenyewe,haya ni mambo madogo madogo wala hayana athari kubwa ktk Dini.

Msio kuwa waislamu narudia mambo ya Ngoswe mwachieni Ngoswe mwenyewe
 
Hata Mimi najiulizaga.
Leo asubuhi mwezi nimeiuona, kwanini waislamu huu hawautaki wanataka mpaka Saudia waseme wameuona ndio na Hawa wa confirm?
Mkuu skukuu ya leo sio ya kuangalia mwezi
 
Mkuu leo ni siku kuu ya kuchinja na sio kubwabwaja vitu za kitoto
 
Chamsingi chinjeni mifugo mle mlale.

#MaendeleoHayanaChama
 
Salary umeanza kuwa na tabia Kama za Jonhbaptist za kuleta nyuzi za hovyo
 
Mwaka huu ilikuwa hivi: Siku mwezi unaandama ili funga ianze Bakwata walitoa excuse kuwa wamewasiliana na jirani zetu Kenya wakaambiwa bado.

Siku ya kufungua Kenya wakatangaza mwezi umeandama ila huku Bakwata wakasema bado hujaandama na wakaelekeza siku inayofuata ndio itakuwa Eid.

Sasa kwanini walishindwa kuwasiliana na jirani zetu tena kama mwanzo?

Ebu tung'amue hili kwanza tunaweza kupata chochote juu ya Bakwata
 
Sasa kama anga ipo VERY CLEAR na mwezi huonekani, kumbe unamuuliza jirani ili iweje?! Hiyo si ndo ile inaitwa "kuandamisha mwezi?

Tunaweza tusiwapende BAKWATA especially kutokana na tabia yao ya kujiingiza kwenye siasa za CCM lakini kwa hili, BAKWATA wanaweza kuwa sahihi zaidi kuliko wanaodhani ndo wapo sahihi!!

Hadithi zote zinazungumzia suala la KUUONA MWEZI, na hakuna popote inaposema ili mradi Saudi Arabia umeonekana, basi dunia nzima inapaswa kufunga ama kufungua kama wafanyavyo Saudi Arabia!

Hebu tafuta online The Book of Fasting... yaani ni sehemu ya Hadith. Au Google "Sahih Muslim 1087 + The Book Fasting". Moja ya hadith inamzungumzia Umm Fadl. Huyu katoka zake Medina kaenda Syria, kule akakuta mwezi umeandama Ijumaa, na kwahiyo Jmosi pale Syria wakaanza kufunga!

Baada ya mwezi kupita, akarudi zake Medina, kwa hesabu zake alitarajia kule akute Ramadhan imeisha na kwahiyo siku inayofuata iwe Eid. Hata hivyo akakuta siku inayofuata watu wa Medina wanaendelea kufunga. Ndipo akasema kule alikotoka, Mwezi wa Ramadhan uliandama Ijumaa!

Akaulizwa na Abdullah bin Abbas ikiwa aliuona huo mwezi yeye mwenyewe kwa macho yake, akajibu YES, na watu kibao waliuona, na ndo maana Jmosi wakaanza kufunga!

Abdullah bin Abbas akasema "sisi, yaani watu wa Medina hatukuona mwezi Ijumaa bali Jmosi, na kwahiyo kesho tunaendelea hadi tutimize siku 30 au tuone mwandamo!"

Dogo akamuuliza Abdullah bin 'Abbas, ikiwa mwandamo wa kule Syria pale Medina hautambuliki?! Abdullah bin 'Abbas akasema, kwa mujibu wa mafundisho ya Mtume, HAPANA! Hapana kwa sababu, according to Sahihi Muslim, Hadith No 2378, AbuHurayrah alimnukuu Mtume Muhammad akisema :-
Allah’s Messenger (peace_be_upon_him) said: Whenever you sight the new moon (of the month of Ramadan) observe fast, and when you sight it (the new moon of Shawwal) break it, and if the sky is cloudy for you, then observe fast for thirty days.
Unaona hapo, hata kufunga siku 30 condition yake ni kwa sababu umeshindwa kuuona mwezi kutokana na mawingu, na kwahiyo huna uhakika kama umeonekana au hapana!

Lakini anga lipo clear, sababu pekee ya kutouona mwezi ni kwavile HUJAONEKANA!! Lakini kwa kuwa hivi sasa tumejiongeza na kuwauliza majirani, basi waulize ikiwa anga lina mawingu lakini kama halina mawingu, unauliza ili iweje?!

That being said, BAKWATA wahukumiwe kwa kutotaka kutumia teknolojia lakini kwa mujibu wa Hadith, BAKWATA wapo sahihi unless kama imewahi kuthibitika Bongo watu wameuona mwezi, na wakatoa ushuhuda kama inavyotakikana na bado BAKWATA wakafinya hizo taarifa... sijui kwa manufaa ya nani au ili iweje.. I DON'T KNOW!!
 
Hii issue inaleta Confusion kila mwaka.

Ilimradi wengine tumepata mwaliko na tumekula pilau nyama na kushiba vizuri basi.... ''Alhamdullilah''
 
Kwani idi ya kuchinja inaenda na muandamo wa mwezi sheikh!???? 🤔
 
Vipi idi hii nayo ni mwezi pia?? 🤔
 
Bakwata janja janja nyingi
 
Vipi idi hii nayo ni mwezi pia?? 🤔
Eid na matukio karibu yote yanatokana na mwandamo wa mwezi. Eid hii huwezi kusikia sana habari za mwandamo kwa sababu, mosi haihusishi funga ya lazima ambayo inakusanya watu wengi na pili, Eid hii husherehekewa siku kadhaa baada ya mwezi kuwa umeshaonekana.
 
Bakwata janja janja nyingi
Kwa mengine lakini sio kwenye hili. Wanachonikera sana BAKWATA ni kujiegemeza zaidi serikalini, na matokeo yake kuwa influenced na siasa za nchi.

Serikali haina maslahi yoyote kwenye mwandamo wa mwezi, na kwahiyo wala hawana sababu ya kuwatumia BAKWATA ku-influence mwandamo wa mwezi.... kwanza ili iweje?!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…