Huyu ndugu, nakumbuka interview yake moja aliyoifanya baada ya kutoka kutembelea jumba la Big Brother south africa, alilalamika sana namna watanzania walivyokua wakimkejeli kutokana na kukosea kwake kuongea lugha ya kingereza. Jamaa alilalamika kwamba watanzania badala ya kumpa support kwa kazi nzuri aliyokua akiifanya ya kukuza sanaa na jina la nchi, ndio kwanza wanamkatisha tamaa kwa kuendekeza tamaa, akamalizia kwa kusema kwamba " Kama watu hawaoni jitihada anazozifanya, ipo siku miti na mawe vitazungumzia kazi alizokua akizifanya" Ni kweli alijitahidi sana.