Hivi ni kweli wasanii wa bongo movies wameshindwa kutunga tamthiliya pendwa itakayopata mashiko nchini?

Hivi ni kweli wasanii wa bongo movies wameshindwa kutunga tamthiliya pendwa itakayopata mashiko nchini?

Victor Mlaki

JF-Expert Member
Joined
May 1, 2016
Posts
4,151
Reaction score
4,277
Tanzania ina wasanii wengi mno lakini cha kusikitisha ubinafsi umewapiga kiasi cha kuua kabisa ubunifu wao. Wazee wenzangu tunakumbuka tamthiliya ya tausi ilivyokuwa na mashiko wakati ule.

Hivi inaingi akilini nchi ya uchumi wa kati tunaangalia tamthiliya za wenzetu zilizofasiriwa kwa Kiswahili cha kubumbabumba badala ya Kiswahili sanifu cha Kitanzania?.

BASATA na BAKITA, Sijui kama wanaona Kiswahili kinavyooza kutokana na tawi la sanaa kuachwa katika ombwe. Hali ni mbaya kwenye sanaa ya ndani licha ya wasanii wengi kuwa na ndoto kubwa ya kutoka nje.

Fuatilieni picha za Kinaijeria " Nigerian movies" utaona namna maarifa ya asili " indigenous knowledge inavyopewa kipaumbele" siyo huku tunajifanya Wazungu na kuharibu usemi Mama.." mother tongue" pamoja na utamaduni zetu.

Isidingo the need na Gangaa zimeisha sasa tunasubiria toleo jingine halafu tunakuwa kuambiana sanaa ya bongo kwenye maigizo imekua.
 
Standard one inayoendana na uchumi wa kati.
 
CCM ndiyo iliyowapumbaza Kwa kuwageuza misukule yao, ndiyo maana hawana jipya zaidi ya majungu na kashfa.
 
Tamthilia zipo kibao. Utakua unatumia kingamuzi cha TING!🤣🤣
soma tena uzi Mkuu ......namaanisha kuwa a tamthiliya Mama acha vurugu na makorokocho ya tamthiliya yaliyopo...kumubuka bongo movie ni industry inayokuza utamaduni wa Taifa.
 
Hawajawahi kuwa wabunifu! Inawezekana na ukosefu wa elimu ya maigizo, nayo itakuwa inachangia.

Wamekuwa ni watu wa kuamini katika uwezo tu binafsi wa kuigiza na siyo ule kwenda shule.
 
Mimi huwa najisikia vibaya sana kuwaona watu wakikimbilia kuangalia season za nje zilizofasiriwa kwa Kiswahili cha kubumba wakati tuna wasanii lukuki wanaoweza kuipaisha sanaa yetu na sisi tukauza...
natamani tupate "Jumong" ya Kitanzania...
 
Mimi huwa najisikia vibaya sana kuwaona watu wakikimbilia kuangalia season za nje zilizofasiriwa kwa Kiswahili cha kubumba wakati tuna wasanii lukuki wanaoweza kuipaisha sanaa yetu na sisi tukauza...
natamani tupate "Jumong" ya Kitanzania...
Kitu kizuri ni ghali hawana pesa hao.
 
soma tena uzi Mkuu ......namaanisha kuwa a tamthiliya Mama acha vurugu na makorokocho ya tamthiliya yaliyopo...kumubuka bongo movie ni industry inayokuza utamaduni wa Taifa.

Hujui hata unalosema. Eti “mother tongue”...kwani umeambiwa tamthilia za Bongo wanaongea Kichina?. Mkuu mi nadhani ungefanya kwanza research!
 
Bongo muvi hakuna kitu,eti shetani anavuka barabara huku anaangalia magari asigongwe? Uliona wapi shetani anagongwa na gari
 
Kitu kizuri ni ghali hawana pesa

Hujui hata unalosema. Eti “mother tongue”...kwani umeambiwa tamthilia za Bongo wanaongea Kichina?. Mkuu mi nadhani ungefanya kwanza research!
Mkuu sijakuelewa unatumia kigezo kipi cha kupima kujua. Uliza nikueleweshe nina uelewa wa lugha ya Kiswahili kuliko unavyofikiri...nimekisomea kama somo ninaelewa ninachokiandija hapa kuhusu sanaa na tafiti. Hapa nilipo ninaendelea pia na utafiti.
 
Bongo muvi hakuna kitu,eti shetani anavuka barabara huku anaangalia magari asigongwe? Uliona wapi shetani anagongwa na gari
Tatizo ni kuiga kila kitu cha utamaduni wa nje na kusahau ubunifu wa ndani ya ulimwengu wetu.
 
Hivi wale wanaosomea maigizo UD wanaishia wapi? Ukiachana na vipaji ila watu waliosomea maigizo huwa vizuri sana kwenye hiyo kazi.
 
Back
Top Bottom