Hivi ni kweli wasanii wengi wa Tanzania baba zao waliwatelekeza?

Hivi ni kweli wasanii wengi wa Tanzania baba zao waliwatelekeza?

Tatizo ni moja, wanawake mkishaachana wanatia chuki mbaya kwa watoto, Kuna siku niligindua hili hivyo nikarudi kwa Mzee Kama kawa, hata nikashangaa yaani kumsogelea tu , kila kitu akanisaidia shule, gharama za chuo, mpaka leo tuko close Sana, simu nikilishwa mapema but NASHUKURU God alinifumbua kwamba so kila Mara wazee hawatupendi but lipo lingine nyuma ya yote
Umeongea kweri tupu
 
Mkuu mama akiwa bint anaweza kumpenda kijana furani wakaanzisha mahusiano.....
Binti akapata mimba,Ila kwakua mama yake na baba yake(babu na Bibi yako) hawajampenda kwa namna moja au nyingine wanamkataa
Bint huyo akaolewa na mwanaume mwingine ........
Wewe mtoto utapewa sumu Kari juu ya baba yako tangu mdogo,utaishi ukimchukia miaka yotee,.



Siku moja mtafute baba yako ongea nae,from there utagundua kama Ni kweri au Ni sumu ulipewa
 
Ni upuuzi wa mwanamke (mama) kuhamisha chuki za ugomvi wao kwa mtoto.
Hakuna mzazi asiyependa kuishi na mwanaye wa kumzaa mwenyewe, narudia tena huyo baba hayupo na hatokuwepo kwa mazingira ya kawaida.
 
Nashukuru wazazi wangu wote wawili wako pa1. Pia wako karibu na mie.
 
Hapa kuna ukweli, wababa tunajisahaulisha na michepuko badae unakuta watoto wametoboa na wewe huna chochote unabaki kulaani tu watoto kwamba wamekutelekeza wakati wewe ndio ulisababisha yote hayo.

Kuna cha kujifunza hapa.
Imekuwa kama fashion, sasa sijuii ni kweli au ndo muendelezo wa kina baba kutengwa kwenyw kula mema ya watoto wao? jana nilikuwa na sikiliza kipindi cha the switch wasafi pale kwenye segment ya cha kijani mama wa msanii mario alikuwa ana hojiwa akasema amemlea mwanae peke yake baba yake alimtelekeza

Diamond naye baba yake alimtelekeza, Ommy dimpoz baba yake naye alimtelekeza, Mwana FA naye baba alimtelekeza, Ney wa mitego kila siku anamuonesha mama ake tu sijawahii kumuona baba, inatia mashaka kweli kama ni tabia zetu kweli wakina baba tuache aise
 
Ni upuuzi wa mwanamke (mama) kuhamisha chuki za ugomvi wao kwa mtoto.
Hakuna mzazi asiyependa kuishi na mwanaye wa kumzaa mwenyewe, narudia tena huyo baba hayupo na hatokuwepo kwa mazingira ya kawaida.


Mkuu labda unatolea mfano huko kwenu Oystersbay, lakini kwetu uswahilini kuna watoto kibao wanataabika baba zao hawajulikani walipo. Utakuta kwenye kibanda umiza wamejazana wanalala kama wapo Big Brother. Kwa hali ile nani anaweza kukataa msaada wa baba?
 
Kama baba yako kakulea vizuri usiongee kwa kauli jumuishi. Kuna wazee ni hatari halafu mbaya zaidi huwa wakifika uzeeni wanatoswa na vimada vyao anabakia kulaumu watoto wamemtelekeza.
Ni upuuzi wa mwanamke (mama) kuhamisha chuki za ugomvi wao kwa mtoto.
Hakuna mzazi asiyependa kuishi na mwanaye wa kumzaa mwenyewe, narudia tena huyo baba hayupo na hatokuwepo kwa mazingira ya kawaida.
 
Kama baba yako kakulea vizuri usiongee kwa kauli jumuishi. Kuna wazee ni hatari halafu mbaya zaidi huwa wakifika uzeeni wanatoswa na vimada vyao anabakia kulaumu watoto wamemtelekeza.
Ukiona mwanaume anatelekeza mtoto wake basi ujue kuna jambo ambalo sio la kawaida.
Achilia mbali kulelewa vizuri, mimi pia ni mzazi najua nacho kiandika mkuu.
 
Ni upuuzi wa mwanamke (mama) kuhamisha chuki za ugomvi wao kwa mtoto.
Hakuna mzazi asiyependa kuishi na mwanaye wa kumzaa mwenyewe, narudia tena huyo baba hayupo na hatokuwepo kwa mazingira ya kawaida.
Kweli asee
 
Mkuu labda unatolea mfano huko kwenu Oystersbay, lakini kwetu uswahilini kuna watoto kibao wanataabika baba zao hawajulikani walipo. Utakuta kwenye kibanda umiza wamejazana wanalala kama wapo Big Brother. Kwa hali ile nani anaweza kukataa msaada wa baba?
Ukifuatilia visa vya hao watoto utagundua nachosema kina mashiko.
Halafu huko Ostersbay ndo wapi mkuu....karibu kwetu Ndono - Uyui ujionee ukarimu wetu.
 
Ukifuatilia visa vya hao watoto utagundua nachosema kina mashiko.
Halafu huko Ostersbay ndo wapi mkuu....karibu kwetu Ndono - Uyui ujionee ukarimu wetu.


Mkuu watoto waliotelekezwa huko uswahilini ni wengi sana, hivyo visa unavyosema sijui kama vinatosha kuwa excuses.
 
Nikitazamaga watu wengi waliofanikiwa mfno ktk utajiri mkubwa, vipaji vya michezo au uimbaji, soccer na wengineo wengi ni watu waliotelekezwa na BABA zao,,

akina mama mtuambie kuna siri gani mtoto akilelewa na mzazi mmoja hasa MAMA uwa ndio vinara ktk sehemu nyingi tofaut tofaut

Hii sio kweli, sema kwa vile ni kesi chache ni rahisi kwako kuhitimisha hivyo... ni sawa na ile kuamini kuwa wenye mashoto (left handed) wengi wao ni mashuhuri.

Hii inakuwa wengi wao kati ya wangapi.?
 
Mimi baba yangu alinitelekeza nikiwa chuo nilipambana still baadae nkampa nafasi yake kama baba..nadhani hii ni same na kinachotokea katika maisha ya hawa wasanii sidhani kama wanawatelekeza from day one kuna kipindi tu cha maisha kinatokea baba kashikwa na mwanamke nje anashindwa kukumbuka familia yake mimi baada ya kugundua hivyo niliamua kusamehe tu maana nkajua mzee hakuwa tena kwenye akili zake
Baba yako kakulea wee kuanzia chekechea mpaka chuo, kwanini akutelekeze wakati tayari anakaribia kula matunda? Lazima kuna sababu sio bure,kuna rafiki jirani yetu amegoma kabisa kumpeleka mtoto chuo,sio kwamba hana uwezo la hasha ,Kijana kaanza kibri anaingilia ugomvi wa wazazi wake halafu anakuwa upande wa mama yake ,unatarajia nini hapo?
Mfano unamwambia baba yako,baba wacha dharau hizo, unamdharau sana mama yangu,yaani unamwonyesha umwamba baba yako,halafu umesikiliza malalamiko ya upande mmoja tu wa Mama yako,je wewe ukiwa baba utaendelea kumthamini huyo mtoto?
 
Tatizo ni moja, wanawake mkishaachana wanatia chuki mbaya kwa watoto, Kuna siku niligindua hili hivyo nikarudi kwa Mzee Kama kawa, hata nikashangaa yaani kumsogelea tu , kila kitu akanisaidia shule, gharama za chuo, mpaka leo tuko close Sana, simu nikilishwa mapema but NASHUKURU God alinifumbua kwamba so kila Mara wazee hawatupendi but lipo lingine nyuma ya yote
Sio wakiachana tu hata baba akioa mke wa pili tu inakuwa shida,Bibi mkubwa anaanza kuwanywesha sumu watoto mwisho wa siku watoto wanamuona baba si lolote wala si chochote,na baba naye akiona hivyo lazima aonyeshe ubaba wake anakata laini,na anaweza akawatamkia kuanzia leo mama yenu ndio baba yenu,tusijuane
 
Tatizo hili kwa kiasi kikubwa linachangiwa na watu kuzaa nje ya ndoa...laiti watu wangefuata misingi ya dini na kuoana kihalili kabisa basi hizi kesi za watoto kutelekezwa na baba zao zingekuwa chache mnoooo...
 
Back
Top Bottom