Hivi ni kweli, yule Mzee wa kazi chafu aka MVP Litombo anakwenda Simba?

chase amante

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2018
Posts
5,599
Reaction score
2,115
Habarini za usiku,

Nimeamua niulize ukweli wa tetesi hizi zinazomuhusisha Bangala kutimkia Simba lakini kitu kinachonifikirisha zaidi ni sababu zilizopelekea mpaka zikawepo tetesi hizi.

Je, uongozi wa Yanga umeshindwa kabisa kukaa mezani na bangala wamalize tofauti zao? Je,huduma ya mkongoman huyu imefika mwisho baada ya yanga kumpata nungu nungu master? Je, klabu haina fedha za kutosha kumlipa au kumshawishi aongeze Mkataba?

Jamani mwenye ukweli wa kinachoendelea kati ya yanga na bangala nomba anijuze .
 
Bangala ANAMKATABA WA Mwaka mmoja na yanga.

YANGA WALITAKA kumpeleka SINGIDA akakataa na KUOMBA kuvunja mkataba............

1. Simba walikuwa na uhitaji mkubwa sana WA Bangala., idadi ya Mabeki na Viungo wao ni chache.

2. Simba Inashida sana ya kiungo mkabaji.

3. Wamekosea kwenye usajili kuleta KIPA WA KIGENI na kujaza idadi 12.

4. Hawana mchezaji wa KUMUACHA na kumleta Bangala
 
Wachezaji wa kigeni.

1. Jefferson Luis goal keeper.
2. Ngoma
3. Kramo
4. Malone
5. Onana.
6. MIQUESSON.

7. Inonga
8. Kanute
9. Saido.
10. Baleke.
11 Chama
12. Phili.

13. SACKO.
14 . Banda .

WANGEKUWA NA AKILI WANGEMTOA KAFALA PHILI AJE BANGALA.
 
Bangala ANAMKATABA WA Mwaka mmoja na yanga.

YANGA WALITAKA kumpeleka SINGIDA akakataa na KUOMBA kuvunja mkataba...
Si wamemuacha sakho tayari
Mchukueni tu,kwetu alishaaga 20% tu ya kubaki alisema mwenyewe
Alivimba kichwa sana.

Eti anatuambja kubaki asilimia 80℅.

Pia alikuwa anachochea migomo sana nabi alishaandika ripoti yake kabla hata ya msimu kuwa djuma na bangala waachwe
 
Wachezaji wa kigeni.

1. Jefferson Luis goal keeper.
2. Ngoma
3. Kramo
4. Malone
5. Onana.
6. MIQUESSON.

7. Inonga
8. Kanute
9. Saido.
10. Baleke.
11 Chama
12. Phili.

13. SACKO.
14 . Banda .

WANGEKUWA NA AKILI WANGEMTOA KAFALA PHILI AJE BANGALA.
Banda na Phiri ni "surplus to requirements"
Simba wana wachezaji wengi eneo la mbele ambalo wanacheza hao flop wawili lakini wana uhaba kwenye kiungo ya chini na beki ya kati kwaiyo usajili wa Bangala utakua na faida kubwa kuliko kuendelea kukaa na hao takataka wawili wasiokua na matumizi kwa Robertinho
 
Kwanini umewaita takataka mkuu. Ni mpira tu au una shida nyingine na wao.
 
Aloooooooo.
Kama ni kuondoka na aondoke hakuna mchezaji mkubwa zaidi ya yangA
 
Djuma na Bangala walizingua sana, acha waondoke tu
 
Hivi Mkuu kwa huu moto wa kati wa Mudathir, Mkude anayesambaza mipira mithili ya Paul Scholes au De Bruyne bado unamfikiria Bangala? Yanga imekamilika haswa, bado Striker tu pale.

Kipindi cha mwisho wa msimu Bangala alianza kushuka, kwa Yanga hii ya sasa Bangala anasugua benchi mkuu. Napendekeza nafasi yake izibwe na Striker au mido nzuri ya kati, kiungo mshambuliaji.
 
Si wamemuacha sakho tayari

Alivimba kichwa sana
Eti anatuambja kubaki asilimia 80℅
Pia alikuwa anachochea migomo sana nabi alishaandika ripoti yake kabla hata ya msimu kuwa djuma na bangala waachwe
Aende tu huko Simba.
 
Tatizo huanza pale hawa wachezaji mkiwasifia sanaa wanavimba vichwa na kuanza kiburi
 
Angalia ulichokiandika wewe! yaani moze phiri atolewe kafara eti kaziba nafasi? hujui mpira wewe, yaani bora watimue yule ntibanzonkii
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…