Hivi ni lazima Mawaziri wanapoongea kumtaja taja Rais kila baada ya sentensi mbili?

Mawaziri wote ni chawa tu
 
Ni ushamba tu.Na ni utamaduni wa hovyo tu kutukuzana na kujipendekeza.Kama wale wanaotaja wake zao kwenye hotuba
 
Itakuwa hujui kitu. Hao wamejifunza somo kutoka kwenye kung'atuka kwa Job Ndugai.
Kwa jina la Yesu Kristo aliyehai Mimi najua ndo maana umekuja na ukosoaji usivaa nguo.
Hivi ni kitu gani unaweza kujifunza kutoka kwa hawa watu mfano Ndugai kwa ujumla labda uongo na jeuri.
Soma vitabu utajifunza ila sio kwa hao watu kwani unafiki ni laana kubwa kumbuka waliowengi ni wanafiki wa hali ya juu.
 
Hayo ni matunda ya utawala wa Magufuli.

Bashungwa pia kumbuka aliyemuingiza kwenye baraza la mawaziri ni Magufuli kwa hiyo lazima aishi kwa tahadhari sana katika utawala wa Mama Samia.

Hivyo muache amtaje Samia hata mara 100 wahafidhina wasije wakamtengenezea nongwa kuwa na yeye ni SukumaGang.

Unapokuwa kwenye baraza la mawaziri hutakiwa kumfanya Rais akutilie doa hata kidogo.
 
Hiyo tabia inatumiwa kama njia ya kumpumbaza bosi ili awaone wako nae pamoja, ni kama wanapata "psychological relief" fulani kwa hao mawaziri.
 
Ilianzia kwa mwendazake...hawa wanaendeleza alipoishia bwana yule na watu wake...kipindi kile ukisifu sana na kuabudu ililipa kama tulivyoona kwa Mwigulu...

Wakati flani late Ben Mkapa alikemea tabia ya kuita serikali yangu ambayo bwana yule aliipandikiza na kusema iitwe serikali ya ccm...no body paid attention!

Endelea kula mtori....[emoji16]
 
Hata JPM alikuwa akimtaja Kikwete na kumpongeza kwa kusafiri sana kuitafutia nchi pesa.
 

Watu wana ganga njaa... walijifunza hivyo kwa mwendazake, ukisifia sifia kama Kabudi unaendelea kula meza kuu... Ndio tulipofikia ndugu yangu.
 

Mambo ya mheshimiwa raisi ametoa hela hizi....utazani katoa kwenye pochi yake
 
Ndio ni lazima
 
Hii nchi sometimes ina mambo ya ovyo sana! Hili lilishamiri sana wakati wa mwendazake. Kumtaja taja na kumuabudu Rais kila mara. Pathetic!
Yaani mtu hawezi kusema tu serikali ikatosha, mpaka aseme "inayoongozwa na.." Asiyejua nani? Rais anasifiwa hata kwa ujenzi wa matundu ya vyoo shuleni, utadhani ametoa sehemu ya mshahara wake!

Huu 'ujinga' hutaukuta kule watu walikotangulia kujitambua.
 
Siri ya mabeberu ni kukupatia pesa nyingi leo lakini kizazi kijacho kitarudisha pesa nyingi maradufu!! Ni utumwa wa karne ya 21!
 
Basi watakuwa wanamtaja mumeo, maana Rais ndio boss wao na ndio mtoaji wa hizo fedha za baadhi ya miradi mingi nchini,

Sasa Kama wanakukera bibie,Basi watakuwa wanamtaja mumeo,Cha msingi wape jina!!
 
tumeambiwa tuishi nao kwa akili,

YEYE ANAPENDA KUSIFIWA SIFIWA. ACHA NA ASIFIWE!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…