Hivi ni mpuuzi gani aliyewaambia ball boys wa Tanzania kufanya ujinga kama huu wa kurusha mipira miwili miwili uwanjani?

Hivi ni mpuuzi gani aliyewaambia ball boys wa Tanzania kufanya ujinga kama huu wa kurusha mipira miwili miwili uwanjani?

Acha iwe ivyo ili Caf waanze kushugulikia, ikishamiri wataona kero watachukua hatua ili na wa kaskazini waache izo mambo za kihuni.
 
Sidhani Kama ni mbinu sahihi katika mpira wetu wakati tuna kikosi kibovu Cha timu ya Taifa (taifa stars).

Ovyo kabisa.
Kwa kweli timu ni mbovu, kocha hovyo na tabia iliyoonyeshwa na ball boys ni aibu sana! Na hatutaweza kufuzu haya mashindano kwa sababu mechi ya mwisho Algeria watatuburuza hadi kwenye kona ya ulingo na ukizingatia tuna tofauti ya magoli mawili tu ya kufungwa na wao Uganda watamaliza mechi yao ya mwisho na Niger! Kwa vyovyote vile Uganda itachapa magoli mengi wakati sisi tutachapwa pia magoli mengi na Algeria. Atakaesonga mbele pamoja na Algeria ataamuliwa kwa magoli kama Bayern na Dortmund maana points tutalingana tu na Uganda!
 
Wanafanya Waarabu sembuse sisi.. Toa upuuzi wako hapa, huoni mbinu ilitusaidia wakati Hali Iko mbaya.. me da zako bhna Wacha Ball boys Wafanye Mambo zao
Waarabu wanafanya hayo na mpira wanaujua,siyo sisi tunafanya upuuzi na mpira ni hovyo kabisa! Na watakaosonga mbele katika kundi i hili ni Uganda na Algeria!
 
Tena wanarusha mipira mingi hadi inaonekana kabisa ni makusudi. Mpira mmoja wa ziada unatosha kusimamisha mchezo.

Na huu uhuni ni kwenye vilabu siyo kwenye timu za taifa. Shenzi kabisa.
Wamejifunza Algeria
 
Waarabu wanafanya hayo na mpira wanaujua,siyo sisi tunafanya upuuzi na mpira ni hovyo kabisa! Na watakaosonga mbele katika kundi i hili ni Uganda na Algeria!
Uganda hasongi mbele.. kama vipi weka hela nami niweke hela, tukutane September 😁
 
waarabu wametufundisha. ila nimeangalia mpira wa uganda na algeria, nimeona uganda wapo mbali sana kimpira hata sijui kwao tuliwafungaje. wanastahili kuwepo nafasi yetu ya pili.
Mechi ijayo Uganda wanarudi nafasi ya pili, Algeria kule ushindi droo,ila hata hiyo droo siioni ikipatikana. Uganda Niger atampiga nyingi.
 
Algeria walikuwa hawarushi mipira mingi vile na ilikuwa inarushwa wakati mpira ukiwa umetoka. Tunakuwa malimbukeni hadi kwenye kufanya uhuni.
CAF imeshindwa kuendesha mpira mechi ya Yanga na USM Alger yalotikea matukio ya ajabu nikadhani watajifunza ndani ya wiki hio hio yakajirudia mechi ya Wydad Vs Al Ahly tena mbele ya Rais wa CAF
 
Acheni kuleta mambo ya ustaarabu kwenye vita. Good job ball boys
Tukitaka vita inabidi tuanze kupigana wenyewe kwanza, tuvizoee ndiyo tuweze kupigana na wengine. Siku ile nilipoona Yanga wanapita jengo la Simba, tena mara ya pili ndani ya wiki moja, halafu wanawasha moshi wakaondoka bila hata mtu mmoja kupigwa mtama nikajua hatuwezi vita vya mpira. Tubaki tu kuviziana kwenye ulozi na labda kuhonga marefa.
 
Back
Top Bottom