Hivi ni upinzani ukichukua nchi amani itavunjika au CCM ikinyang'anywa madaraka italeta machafuko?

Hivi ni upinzani ukichukua nchi amani itavunjika au CCM ikinyang'anywa madaraka italeta machafuko?

Poa 2

JF-Expert Member
Joined
Jul 7, 2019
Posts
1,317
Reaction score
1,320
Wakuu habari,

Miongoni mwa propaganda iliyopitwa na wakati lakini bado inatumiwa sana na wana CCM ni hii, kwamba upinzani ukichukua nchi utaleta machafuko.

Huwa najiuliza upinzani una nguvu sana na CCM wanalijua hilo ndio maana hutumia mbinu chafu dhidi ya upinzani Ili kujibakisha madarakani.

Wanachama wengi wa upinzani huwa wako tayari kwa lolote kulinda haki zao hata kwa kutumia mbinu chafu kama CCM lakini viongozi wa juu huwatuliza.

Vyama vya upinzani viko toka miaka ya 1990's havijawahi kuvunja amani au kuleta vurugu hapa nchini, bali wao hufanyiwa vurugu na CCM kwa miaka yote.

Sasa itakuwaje siku wapewe mamlaka na wananchi ya kuongoza nchi ndio wavunje amani? Na walete vurugu? Na vurugu hizo watawaletea wakina nani au wananchi waliowapa ridhaa?

Hebu wana CCM jibuni hoja wafafanulieni Watanzania, upinzani utaleta vurugu au uvunjifu wa amani kwa namna ipi?

Nyie CCM ndio mtavunja amani ya nchi hii kwa ubinafsi wenu uliokithiri.
 
CCM wanatumia propaganda ya amani maana wanajua watanzania wengi ni waoga. Kwa taarifa yako hakuna mwanaccm wa kuleta machafuko maana hata wao wanategemea vyombo vya dola. Wakipoteza tu nguvu ya dola wote watageuka kuwa wapole.
 
CCM wanatumia propaganda ya amani maana wanajua watanzania wengi ni waoga. Kwa taarifa yako hakuna mwanaccm wa kuleta machafuko maana hata wao wanategemea vyombo vya dola. Wakipoteza tu nguvu ya dola wote watageuka kuwa wapole.
Hoja hii nayo vyama vya upinzani viipe nguvu kuifafanua Kwa wananchi waelewe vizuri maana wananchi wetu ni waoga hivyo kuiacha bila ufafanuzi inaweza kuwa kete muhimu Kwa ccm
 
CCM wanatumia propaganda ya amani maana wanajua watanzania wengi ni waoga. Kwa taarifa yako hakuna mwanaccm wa kuleta machafuko maana hata wao wanategemea vyombo vya dola. Wakipoteza tu nguvu ya dola wote watageuka kuwa wapole.
Propaganda hizo zilishapitwa na wakati !
 
Wakuu habari

Miongoni mwa propaganda iliyopitwa na wakati lkn Bado inatumiwa sana na Wana CCM ni hii. Kwamba upinzani ukichukua nchi utaleta machafuko...
Mbona majibu yapo kwenye matokeo ya uchaguzi ambao CCM ilishindwa, rejea Mrema alipomshinda Mkapa, balaa tupu kwani waliamua kuufuta uchaguzi na kuurudia kwa mafungu!

Maalim Seifu alipomshinda komandoo asiye na macho, mpaka baisikeli zilipigwa na kusababisha wakimbizi wa Shimoni Mombasa.
 
Wakuu habari

Miongoni mwa propaganda iliyopitwa na wakati lkn Bado inatumiwa sana na Wana CCM ni hii. Kwamba upinzani ukichukua nchi utaleta machafuko...
Upinzani gani wewe hapa kuna kikundi cha kisanii kilichojificha kwenye maridhiano tu , hawezi kupewa nchi

USSR
 
Upinzani gani wewe hapa kuna kikundi cha kisanii kilichojificha kwenye maridhiano tu , hawezi kupewa nchi

USSR
Hivi weye huwa upo kijiji gani hicho ambacho unadhani mwenyekiti wa kitongoji ni rais wa nchi na mtendaji ni waziri "mkubwa"?Kuna kipindi huwa unaandika vitu kama kichwa umekisahau kilabuni.
 
Wala usiwaze hayo mambo maana kizazi hiki kitapita bila upinzani kuchukua nchi
Na kizazi hiki kitapita bila CCM kuondoka madarakani

YAANI WAPINZANI WANAVYODEKA KWELI WACHUKUE NCHI!!? HAIWEZEKANI

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI CCM
 
Upinzani gani wewe hapa kuna kikundi cha kisanii kilichojificha kwenye maridhiano tu , hawezi kupewa nchi

USSR
Kwani hii nchi Kuna mtu ana hati miliki?
 
Upinzani gani wewe hapa kuna kikundi cha kisanii kilichojificha kwenye maridhiano tu , hawezi kupewa nchi

USSR
Upinzani huu huu ambao ccm imelazimika kukaa nao meza Moja kujadiliana, unafikiri kingekuwa kikundi kama unavyodai ccm ingelazimika?
 
anayenyang'anywa tonge ndiye huanzisha vurugu
Uzuri ni kwamba walinda amani watakuwa wale wale jeshi na polisi kama ni maboresho yatafanywa kidogo. Watakapoanzisha vurugu watakutana na vyombo vya dola[emoji1]
 
Wala usiwaze hayo mambo maana kizazi hiki kitapita bila upinzani kuchukua nchi
Na kizazi hiki kitapita bila CCM kuondoka madarakani

YAANI WAPINZANI WANAVYODEKA KWELI WACHUKUE NCHI!!???? HAIWEZEKANI

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI CCM
Hizi fikra za kizamani sana kama hauamini kuwe na tume huru ya uchaguzi na muitishe uchaguzi hata kesho muone upinzani unavyochukua nchi kiulani
 
Hizi fikra za kizamani sana kama hauamini kuwe na tume huru ya uchaguzi na muitishe uchaguzi hata kesho muone upinzani unavyochukua nchi kiulani

Kama za kizama basi wewe chukua nchi

Sijawahi ona nchi wapinzani wanadeka kama Tanzania
 
CCM ilikataliwa ktk majiji karibu yote 2015 na tuliishi Kwa Amani.

CCM wanaweza kuwa chama Cha upinzani vizuri tu.

CCM ni Chama tu kama kilivyo SIMBA sports club, tofauti ni kuwa kinajihusisha na siasa.
 
Bahati nzuri Tanzania hatuna wapinzani tuna matawi ya CCM yanayoitwa vyama vya upinzani
 
Back
Top Bottom