Hivi nini kinawamaliza WASANII wetu wa BONGO MOVIE??

Hivi nini kinawamaliza WASANII wetu wa BONGO MOVIE??

Kweli hainiingii akilin jinsi wasaanii wetu wanavyo kufa kwa kasi.Yaani kwa mwaka wa jana(2012) tumepoteza wasaan maarufu wawili(R.I.P Kanumba & Sharo Millionea) Na leo hii tunaupokea mwaka (02/01/2013 siku ya pili kwenye mwaka) tumempoteza msaanii wetu maarufu(R.I.P SAJUKI).Sipati picha hii kasi itatufikisha wapi, anyway Mungu uwalaze mahali pema peponi wapendwa wetu walio tangulia mbele ya mkono wa haki, Mungu ibariki Bongo Movie, Mungu ibariki TANZANIA!! Ameni.

mdau makini, na wewe ni marehemu mtarajiwa,unalijua hilo?usiogope sote tutakwenda na tuko njia moja
 
Kweli hainiingii akilin jinsi wasaanii wetu wanavyo kufa kwa kasi.Yaani kwa mwaka wa jana(2012) tumepoteza wasaan maarufu wawili(R.I.P Kanumba & Sharo Millionea) Na leo hii tunaupokea mwaka (02/01/2013 siku ya pili kwenye mwaka) tumempoteza msaanii wetu maarufu(R.I.P SAJUKI).Sipati picha hii kasi itatufikisha wapi, inauma xaana
 
usikurupuke kijana, mbona wengi wamekufa halafu unataja wawili wasanii? umechemsha
 
Mimi nadhani inabidi uanze kufa wewe kwanza, useless mind huna faida kwenye Dunia hii.
 
Cha kujifunza kwenye vifo hivi ni kuwa wote ni marehemu watarajiwa na pia ni vizuri kujiwekea bima ya afya pindi tuuguapo tuweze tibiwa haraka kabla tatizo halijawa kubwa sana. Refer marehemu Sajuki na John Maganga walivoteseka kwa kukosa fedha za kujitibia. Kingine:

  • dont chat and drive eg marehemu Sharo Millionea
  • Dont date underage eg Kanumba
  • Dont force to drive while you cant eg Marehemu Mtema Regia

Tufate maandako ya dini zetu
 
Wanaokufa sio wasanii tu ni watu wowote au mtu yoyote atakufa siku yake ikifika ,wewe unasema wasanii sababu ndio unaowajua,je unajua ni wanadamu wangapi usiowajua wanakufa?kila nafsi itaonja mauti kwa wakati wake,jua tupo kwenye foleni,hapa twapita tu
 
Kifo hakikwepeki haina ubishi!ila ntazungumzia kwanini vijana wengi na si wasanii pekee yao ndo wanaonekana wanapoteza sana maisha.....nchi yetu ni maskini na vijana wengi wakianza maisha ya kujitegemea wanapata pesa kiaina zinazopelekea hao kujitegemea na kutokuwa katika himaya ya wazazi hivyo kuna vitu wanakuwa na ulimbukeni navyo!kama ana gari na mlevi basi kutakuwa na safari za usiku zisizo na kichwa wala miguu!watu watakaa bar usiku mkali wataamua bata likaliwe mbali na hapo wako bwii!vilevile utakuta dereva si competent kivile ni baada ya kupata kimkopo au kulipwa pesa ya album iwe ya music au katoa movie kanununua gari na hana control kivile!pili ni ulimbukeni wa wanawake,mtu akianza kujitegemea na ana vipesa au umaarufu kibongobongo basi kubadilisha wanawake ndo sifa,umaskini..watoto wa kike wanagongwa ngozi ili wapate pesa hususani hawa maarufu ili waende sawa na umaarufu wao ili wapate kubadili vinguo!kiufupi vijana au wasanii wana hatari ya kuzidi kupoteza maisha kwasababu ya maradhi,ulevi na umaskini!!!!!!!!!!ila ulimbukeni unachangia sana!
 
Usianze kutafuta njia ya waganga bure. Kila aliyezaliwa na mwanamke atakufa bila kujali ni msanii, mwanasiasa, mchungaji, sheh wala ki2 chochote
 
Back
Top Bottom