Hivi 'No Reform no Election' inapigania na mgombea binafsi?

Hivi 'No Reform no Election' inapigania na mgombea binafsi?

Chadema hawawezi kutaka uwepo wa mgombea binafsi. Wao kama ilivyo tu CCM au vyama vingine vya siasa, wanapenda kutumia udhamini wa chama kama fimbo au kontroo ya kum-monitor mwanachama aliye na uongozi wa cheo cha kisiasa au anayegombea uongozi wa nafasi ya kisiasa serikalini.

Uwepo wa mgombea binafsi utafanya wanachama wao kutokuwa na hofu tena juu ya udhamini wao ikiwa wataamua kutokubaliana na matakwa ya chama, hata kama kutokukubaliana huko ni kwa maslahi ya Taifa au ya watu anaowaongoza
Ni kwa bahati mbaya sana wanaominya uwepo wa mgombea binafsi huwa hawajitokezi kujenga hoja huenda ipo.(kama ilivyo kwa hoja ya uraia pacha).
Tunajikuta mzani umelalia upande mmoja.
Ila ccm wanakuwa hatarin zaidi kwa ueeoo mgombea binafs kuliko cdm.
Sabab kubwa ni CDM wote ilionao ni wake kimwili na kiroho lakin ccm ina wanachama wake kabsa(wanufaika na mbumbumbu) pamoja na wanafiki.
 
Mawazo yangu
CCM wanakataa mgombea binafsi kwa sababu inakuwa vigumu kumdhibiti. Na hili ni zaidi kwa ngazi za chini za mitaa, vitongoji na vijiji ambako pia mgombea mgombea binafsi ana uwezekano zaidi wa kushinda.
 
Mawazo yangu
CCM wanakataa mgombea binafsi kwa sababu inakuwa vigumu kumdhibiti. Na hili ni zaidi kwa ngazi za chini za mitaa, vitongoji na vijiji ambako pia mgombea mgombea binafsi ana uwezekano zaidi wa kushinda.
Hadi ubunge, mgombea binafsi ana nafasi kubwa tu ya kushinda. Mfano jimbo la Iringa mjini uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, Fredrick Mwakalebela alikuwa na upepo wa hatariii, CCM walipokata jina lake na kumteua kibabe Monica Mbega, wananchi walimwambia ahamie chama chochote kile wao watampa kura zao, akaogopa na kubaki CCM. Matokeo yake wapiga kura za hasira kumchagua Msigwa wa Chadema

Hata 2015, Lowassa angesimama kama mgombea binafsi kwenye urais alikuwa anatoboa. Huko Zenju ndio kabisaaa maalim angeshinda asubuhi kabisa
 
Back
Top Bottom