Hivi redio hizi za Kimataifa BBC, DW, VOA na RFI zinanufaika na nini?

Hivi redio hizi za Kimataifa BBC, DW, VOA na RFI zinanufaika na nini?

Kwanini utamani kitu usichoweza kukifanya.acha kuishi kwa ndoto kama uwezo huna.Walioanzisha hivyo vyombo ni watu kama wewe na kizuri zaidi tayari kuna shirika la utangazaji la nchi kwanini usiende ukapeleka hayo mawazo yako ili hicho unachokitamani kifanikiwe.
Hata sielewi unalalamika nini.
 
Hizo ndio ofisi za makachero wa kimataifa.
 
Mabeberu wanazipa ruzuku kusambaza mazuri ya wazungu, na usidhani ni kiswahili tuu wanaidhaa Mpaka za kiausa na kiigbo. Unaposikia hii ni radio DW idhaha ya kiswahili ni sawa na kusema idara ya kiswahili, utakuta wana idhaha hata hamsini za lugha MBALIMBALI duniani mpaka Afghanistan huko kwa warabu
Na China pia wapo..?
 
Kwa wenye kufahamu utararatibu wanaotumia kufanikisha kurusha matangazo yao kutoka hapa Nchini. Nauliza swali hilo kwasababu mwishoni mwa mwaka jana Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) iliagiza kutolewa kwenye orodha chaneli za ndani isipokuwa TBC, katika kampuni zinazotoa huduma za kurusha matangazo ya televisheni.

Mamlaka ilitoa sababu kuwa walipoenda kwenye mamlaka hiyo kuomba leseni ya kurusha matangazo walijisajili watakuwa wanarusha chaneli za nje, hivyo hawakupaswa kurusha chaneli za ndani. Iliendelea sababu endapo wataruhusiwa kurusha chaneli za nje hapo inaweza kutokea hujuma. Kwamba tukio limetokea hapa nyumbani, habari ikatangenezwa hapa nyumbani, halafu itoke hapa iendekwanza nje ya nchi kisha irudi hapo lolote linaweza kutokea.

Hapo ndio naomba tofauti ya huo mtiririko na wanavyorusha hizo redio za kimataifa, tukio linatokea hapa nyumbani, habari wanaitengeneza hapa nyumbani, kwanini wao waruhusiwe kurusha kwenda nje halafu ndio tuipokee tena hapa nyumbani? je inatofauti gani waliokataza kwa hizo kampuni???

#tcra, #PaschalMayalla, #Nyangombali, #Domsel, #gigabyte, #Wissman, #Joshua_ok, #Mpekuzi Tanzania, #shaka-zulu, #Polonium, #mfianchi, #Wile, #Pandagichiza, #Billionea Asigwa, #thinkanyarwele, #Smart911,
 
Hiv Iran au Korea ile ya "Subwoofer" utaipamba kwa lipi?
Mimi na wewe hatujui lakini kuna mazuri mengi tu wanayo ila wananchi wao wanayajua,ndio maana wewe huwezi kuona mazuri ya bwana kiduku wa N korea sababu bbc na wenzake wameshakulisha sumu nawewe unaamini 100% korea,iran na wengineo maisha yakule ni kama haela.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Waafrika tuna matatizo sana, Burundi wanachinjana watu wakisema aaah msituingilie hatutaki mahakama ya the Hague hii ni laana Afrika!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jamani tukubali au tukatae sisi waafrika hatuwezi kujiongoza wala kupeana habari za kweli bila hawa wenzetu mabeberu na kwa kiasi kikubwa wamesaidia kuziondoa serikali kandamizi barani kwetu na nina matumaini makubwa watatusaidia kuziondoa zilizobaki zinazotawala watu kama ng'ombe
 
Wadau naomba kuuliza hivi redio za Kimataifa kama vile BBC, DW, VOA na RFI zinanufaika na nini kwakurusha matangazo hasa kwa hizi nchi za Maziwa makuu, (Kiswahili) kwani hazirushi matangazo ya biashara kama zilivyo redio zetu. Mfano BBC imefungua Studio kubwa naya kisasa nchini Kenya,
Radio hizi ni propaganda machinery na pia ni namna ya kuhakikisha kwamba kunakuwa na narative yao katika kila kinachoendelea huku kwetu.So usipate Presha.Zinafaidika sana
 
Wadau naomba kuuliza hivi redio za Kimataifa kama vile BBC, DW, VOA na RFI zinanufaika na nini kwakurusha matangazo hasa kwa hizi nchi za Maziwa makuu, (Kiswahili) kwani hazirushi matangazo ya biashara kama zilivyo redio zetu. Mfano BBC imefungua Studio kubwa naya kisasa nchini Kenya,
Jifunze siasa ya dunia na propaganda ndo utaelewa, hafu hizo ni radio za serikali

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hongera kwao kwa kutupasha habari za dunia!

Wanaosema wanasambaza utamaduni wao wanataka zibaki redio kama Uhuru FM ambazo zinatangaza mazuri tu ya jiwe?
 
Propaganda tools za mabeberu
Tanzania chini ya ccmilishindwa kujua uwepo wa mauaji ya ALBINO huko kanda ya ziwa mpaka VICKY Mtetema wa BBC alipoutangazia ulimwengu.... hatua zilichukuliwa ikiwemo ya bwana Pinda kulia bungeni. Hawakuitwa Mabeberu wala propaganda wakati huo leo.... wakitoa misaada kugharamia bajeti wanaitwa wabia / wahisani 60% wanatoa wao wakigharamia matibabu ya wengine kina Lisu ni magaidi pumba pumba pumba....... vuuuuuuuu kabisa
 
ukitaka uone umuhimu wa bbc subiri siku upinzani wakifanya tukio uone kama kuna chombo chochote TANZANIA cha tv main stream kitatangaza zaidi ya bbc swahili pekee.
 
Back
Top Bottom